Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,697
- 9,048
Haya ni maswali yanayotakiwa kujibiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge.
Kwamba watu wasiojulikana waliwezaje kupenya mpaka ndani ya Viwanja vya Bunge wakimfuatilia Mhe. Tundu Lissu na dreva wake bila ya kutambuliwa getini au kizuizi chochote?? Lakini pia waliwezaje kupenya mpaka kwenye Makazi ya Waheshimiwa Wabunge bila ya kujulikana au kuonekana na mtu yeyote?
Baada ya kufanya shambulio la mauaji waliwezaje tena kutoroka kwa kupitia milango/mageti au maeneo au njia hiyo hiyo bila ya kizuizi wala kutambuliwa na mtu yeyote? Lakini jambo la kujiuliza pia ni kwamba ilikuwaje SMG ilipokuwa inakohoa(kutoa mlio wa bunduki kwa risasi 38)haikuweza kuwashtua wakazi wa maeneo ya jirani na makazi ya Waheshimiwa Wabunge. Je, hizo Bunduki walizotumia hawa wauaji zilikuwa na viwambo(Silencers)zinazozuia mlio au mwangwi wa risasi....??
Je, hakuna Mtandao wa Kamera (CCTV-Closed Circuit Television)kwenye viwanja vya Bunge na Makazi ya Waheshimiwa Wabunge ambazo zingeweza kuonyesha picha za Watu WASIOJULIKANA?? Kama zipo Je, ni mbovu au zilizimwa? Kama zilizimwa nina nani alizizima na alielekezwa na nani..?
Naomba Waheshimiwa Wabunge wote bila ya kujali itikadi za vyama vyeo waihoji Kamati yao ya Ulizni na Usalama inayohusika na Ulinzi wao ndani na nje ya Bunge. Kama wataingiza ushabiki wa ki-CCM kuna siku Al-Shaabab au Al-Qaeda wataingia viunga vya Bunge la Tanzania na kuwalipua wote kwa Bomu la muhanga mkiwa ndani ya Bunge maana hakuna ulinzi.
Naomba kuwasilisha.
Kwamba watu wasiojulikana waliwezaje kupenya mpaka ndani ya Viwanja vya Bunge wakimfuatilia Mhe. Tundu Lissu na dreva wake bila ya kutambuliwa getini au kizuizi chochote?? Lakini pia waliwezaje kupenya mpaka kwenye Makazi ya Waheshimiwa Wabunge bila ya kujulikana au kuonekana na mtu yeyote?
Baada ya kufanya shambulio la mauaji waliwezaje tena kutoroka kwa kupitia milango/mageti au maeneo au njia hiyo hiyo bila ya kizuizi wala kutambuliwa na mtu yeyote? Lakini jambo la kujiuliza pia ni kwamba ilikuwaje SMG ilipokuwa inakohoa(kutoa mlio wa bunduki kwa risasi 38)haikuweza kuwashtua wakazi wa maeneo ya jirani na makazi ya Waheshimiwa Wabunge. Je, hizo Bunduki walizotumia hawa wauaji zilikuwa na viwambo(Silencers)zinazozuia mlio au mwangwi wa risasi....??
Je, hakuna Mtandao wa Kamera (CCTV-Closed Circuit Television)kwenye viwanja vya Bunge na Makazi ya Waheshimiwa Wabunge ambazo zingeweza kuonyesha picha za Watu WASIOJULIKANA?? Kama zipo Je, ni mbovu au zilizimwa? Kama zilizimwa nina nani alizizima na alielekezwa na nani..?
Naomba Waheshimiwa Wabunge wote bila ya kujali itikadi za vyama vyeo waihoji Kamati yao ya Ulizni na Usalama inayohusika na Ulinzi wao ndani na nje ya Bunge. Kama wataingiza ushabiki wa ki-CCM kuna siku Al-Shaabab au Al-Qaeda wataingia viunga vya Bunge la Tanzania na kuwalipua wote kwa Bomu la muhanga mkiwa ndani ya Bunge maana hakuna ulinzi.
Naomba kuwasilisha.