Kamati ya kuwalinda waandishi wa habari CPJ, yaitaka Serikali ya Tanzania kutoa ufafanuzi zaidi kuhusu kifo cha Azory Gwanda

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Wito umeendelea kutolewa kutoka sehemu mbalimbali duniani kwa serikali ya Tanzania kutoa ufafanuzi kamili kuhusu hatma ya mwandishi habari Azory Gwanda baada ya waziri ya mambo ya nje nchini, Profesa Palamagamba Kabudi, kusema katika mahojiano na BBC kwamba 'Azory Gwanda aliyetoweka ameshafariki'.

Kamati ya kuwalinda waandishi wa habari CPJ imeeleza kwamba tangu kutoweka kwa mwandishi huyo wa kujitegemea, serikali ya Tanzania haijatoa taarifa zaidi baada ya kuahidi kuchunguza mkasa wa kupotea kwake.

"Kwa mwaka mmoja na nusu familia ya Azory Gwanda na vyombo vya habari Tanzania, wameiomba serikali kufafanua kilichomfika mpendwa na mfanyakazi mwenzao bila mafanikio, halafu ghafla, Waziri wa Mambo ya Nje anataja kwamba mwandishi huyo amefariki. Hili kwa jumla haliridhishi na linatia wasiwasi. Ni lazima serikali itoe taarifa nzima kwa umma kuhusu hatma ya Gwanda." amesema Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa CPJ Robert Mahoney, New York.

Gwanda alitoweka mnamo Novemba 21 2017, baada ya uchunguzi kuhusu maujai ya kiholela na yasioeleweka na kupotea kwa watu katika pwani ya wilaya ya Kibiti.

 
Nairobi, July 10, 2019 --

The Committee to Protect Journalists CPJ, today called on the Tanzanian government to provide a detailed public account of the fate of freelance journalist Azory Gwanda after the country's foreign minister, Palamagamba Kabudi, said in an interview that the journalist is dead.

In an interview with the BBC's "Focus on Africa" program today, Kabudi said that Gwanda had "disappeared and died" in the country's eastern Rufiji region, and said that the government has since "been able to contain that kind of extremism" in the region. Gwanda went missing on November 21, 2017, after investigating mysterious killings and disappearances in his community, and the Tanzanian government has never delivered a promised investigation into his case, according to CPJ research.

"For a year and a half, Azory Gwanda's family and the Tanzanian media have pleaded with the government to explain what happened to their loved one and colleague," said CPJ Deputy Executive Director Robert Mahoney from New York. "Then suddenly the foreign minister mentions, almost in passing, that the journalist is apparently dead. This is wholly inadequate and distressing. The government must immediately share publicly all information it has about Gwanda's fate."

Kabudi told the BBC that the Tanzanian government is not "proud" of the disappearances and killings in Rufiji, which he said also took the lives of police officers and ruling party officials, and said that the government was taking measures to make sure that citizens and journalists are safe. However, CPJ research shows that impunity in journalists' deaths or disappearances contributes to an environment that fosters violence against journalists.

CPJ's phone calls today to Kabudi and Tanzanian government spokesperson Hassan Abbassi went unanswered.
 
Mbona wanapoteza mda tu. Wafanye mengine ya kuimalisha usalama wao. Yaliyopita yamepita.

Kagashoki hadi leo anafamika aliuwawa kwenye jingo la ubalozi lakini hadi sasa haki yake imejifia.
 
Kabudi kaingia cha kike,issue hii aliyoongea inazidi kuipaka matope serikali!
.... kwa maelezo yale ya Kabudi, in short ni kwamba Azory Gwanda alishakufa. Swali la msingi, nini kilimuua? Kwa sababu ipi? Hayo ndiyo ya msingi kuyajua kwa sasa; otherwise, kauli ya waziri mwandamizi kama Kabudi imehitimisha wasiwasi uliokuwepo kwamba Gwanda yu hai au kafa.

Ni muhimu sasa walinzi wa raia na mali zao (IGP na timu yake) watoke hadharani walieleze taifa mkasa mzima badala ya kujificha kwenye kivuli cha "wasiojulikana". Vinginevyo, IGP kashindwa kazi!
 
.... kwa maelezo yale ya Kabudi, in short ni kwamba alishakufa. Swali la msingi, nini kilimuua? Kwa sababu ipi? Hayo ndiyo ya msingi kuyajua kwa sasa; otherwise, kauli ya waziri mwandamizi kama Kabudi imehitimisha wasiwasi uliokuwepo kwamba Gwanda yu hai au kafa.

Ni muhimu sasa walinzi wa raia na mali zao (IGP na timu yake) watoke hadharani walieleze taifa mkasa mzima badala ya kujificha kwenye kivuli cha "wasiojulikana". Vinginevyo, IGP kashindwa kazi!
Wawape mwili ndugu na jamaa wakazike!
 
Mtoto mtiifu anaye kunya kinyesi kikubwa na bahati mbaya au nzuri kanyea sebuleni mwa mabeberu kachemka sana eti sio Azory pekee kapotea na kufa ,kumbe wako wengine ? Ni kina nani hao ?

Uzuri ni kwamba ndugu sasa wataweka matanga baada ya kuambiwa ndugu yao kafariki na bwana Palamaganda John Aidan Mwaluko Kabudi
 
Lakini serikari ina maslahi gani ya kumteka mtu alieenda kupeleleza mauaji ya Kibiti, kwani wao ndio walikuwa wanaua wajumbe wa CCM.

Hapa watuhumiwa ni wahuni wa Kibiti kuliko serikari. Na ni kesi kama nyingine sioni interest ya serikari au watu wasiojulikana kwa huyo mwandishi, unless kama kuna maswala mengine alikuwa anachunguza.
 
Back
Top Bottom