Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imekagua mradi wa Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida tarehe 15 Machi, 2025.
Mradi huo hadi kukamilika kwake unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 13 na unatarajiwa kunufaisha vijiji 11 vilivyopo katika Halmashauri ya Manyoni.
Pia soma Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo katika kijiji cha Lusilile kilichopo Kata ya Kintinku, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Joseph Kakunda amewaelekeza RUWASA kuhakikisha kuwa asilimia 2 za mradi zilizobaki zinakamilishwa ndani ya mwaka huu wa fedha.
Aidha amewaasa Wananchi waliokuwepo katika eneo wakati wa ukaguzi kuhakikisha kuwa wanauutunza mradi huo ili udumu kwa muda mrefu na uendelee kuwanufaisha.
"Mradi ukiharibika ni hasara kwa Wananchi, kwa hiyo ni jukumu lenu wananchi kuhakikisha mradi huu mnautunza ili nao uweze kuwasaidia," alisema.
Kakunda pia alielekeza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya kuhakikisha wanasimamia ulinzi wa miundombinu ya mradi huo na kuwachukulia hatua kali wale wote watakaojaribu kuihujumu.
Mradi huo hadi kukamilika kwake unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 13 na unatarajiwa kunufaisha vijiji 11 vilivyopo katika Halmashauri ya Manyoni.
Pia soma Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo katika kijiji cha Lusilile kilichopo Kata ya Kintinku, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Joseph Kakunda amewaelekeza RUWASA kuhakikisha kuwa asilimia 2 za mradi zilizobaki zinakamilishwa ndani ya mwaka huu wa fedha.
Aidha amewaasa Wananchi waliokuwepo katika eneo wakati wa ukaguzi kuhakikisha kuwa wanauutunza mradi huo ili udumu kwa muda mrefu na uendelee kuwanufaisha.
"Mradi ukiharibika ni hasara kwa Wananchi, kwa hiyo ni jukumu lenu wananchi kuhakikisha mradi huu mnautunza ili nao uweze kuwasaidia," alisema.
Kakunda pia alielekeza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya kuhakikisha wanasimamia ulinzi wa miundombinu ya mradi huo na kuwachukulia hatua kali wale wote watakaojaribu kuihujumu.