kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Katika kuzitokomeza tamaduni za nchi za magharibi, serikali ya Iran imesambaza jeshi maalumu la watu 70,000 watakaokuwa wakiwatia mbaroni wanaume wote watakaokamatwa wakiwa wamevaa chini au hereni. |
Ili kuzitokomeza tamaduni za nchi za magharibi nchini Iran, sheria kali imetolewa ya kupiga marufuku wanaume kuvaa cheni au hereni au kukata nywele katika fasheni za watu wa magharibi. Ili kuisimamia sheria hiyo mpya, jumla ya polisi maalumu 70,000 watakuwa mitaani kuwatia mbaroni wanaume watakaonekana wanakiuka sheria hiyo mpya ambayo imeelezewa kuwa inazuia uvamizi wa tamaduni za magharibi. Wanawake wanaovaa nguo za kubana, suruali fupi au wanaovaa viremba vyenye kuonyesha sehemu ya nywele zao nao watatiwa mbaroni na jeshi hilo maalumu la kurekebisha tabia. Sheria hii imetoka wakati, bunge la Iran likijadili sheria ya kupiga marufuku umilikaji wa mbwa nchini humo. Shirika la habari la Iran, lilisema kuwa sheria hizi mpya zimelenga kuzuia uvamizi wa kitamaduni wa nchi za magharibi na ili kusimamia utekelezaji wa sheria hizo, polisi 70,000 wataingia kwenye mitaa ya Tehran na miji mingine kusaka watu watakaozivunja sheria hizo. |