Kamanda Sirro atakuwa bonge la IGP

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,244
4,469
Nimekuwa nikimsikiliza huyu jamaa, akiwa anafanya mahojiano mbalimbali. Iwe na BBC, DW, na pia vyombo vya habari vya hapa nyumbani. Uongeaji wake huwa wanikosha sana.

Jamaa ametulia, anaongea 'point' tu, kila mtu hutamani kumsikiliza. Ninaamini haya matukio ya ujambazi Dar es Salaam yataisha kabla hakujacha.

Watu kama hawa tukiwa CCP walikuwa wana pass out angalau na kirungu kimoja, hususani cha ukakamavu.

Ukiwaacha Thobias Andengenye na Diwani Athumani, Sirro atakuwa Bonge la IGP.


Aliwahi sifiwa hadi na Gazeti la Mwanahalisi, kwa kuzima mapigano ya wakulima na wafugaji huko Ikwiriri.


Historia ya Sirro

 
Hivi mangu amekosa nini fasta,nadhani Mangu si mbaya sana ila wana siasa hasa ccm wamemyumbisha sana na kupelekea kuchuja ghafla na ma rpc makada wamelifanya jeshi kuchukiwa sana
 
Akiwa Mwanza alifanya kazi yake vizuri sana hata kuletwa Dar kusaidia intelijensia, baada ya Kova kuwa kovu na kuondoka na Siro kupewa nafasi ya Kova naona kama ule uweledi wake ameanza kuuweka pembeni na kuwa na muhemko wa kisiasa zaidi, Siamini kama atastahili kuwa IGP maana ameonekana sasa yeye kuwa kada wa chama fulani na kufuata amri za wana siasa.
Tabia pia ya kukimbilia press kila saa nayo inampunguzia heshima anatakiwa awe na msemaji wake sio kila jambo kwenye press ni kamanda Siro, aende site, atumikie Wananchi na sio kuwatisha kwamaba atawashughulikia. Sio kauli nzuri kwa msomi kama Kamanda Siro.
 
Jamaa yuko vizuri sana.
 
mfumo uliopo si mzuri watumishi wa umma wana jihusisha na siasa katika masuala ambayo hayahitaji siasa kuwe na utengano kazi za chama zibaki kwa wanachama na siasa zibaki kwa wanasiasa .
 
I hope so too
Simoni Siro ni performer yule hategemei kuteuliwa alipo sasa anaridhika anachotaka ni kutumikia nchi na kuacha legacy. Amekulia shule zenye heshima kuu ya kinidhamu hapa nchini(mmeelewa), hawezi kuwa na tamaa alichofundishwa ni OBIDIENCE AND PERSEVERANCE
 
Na kuongoza Polisi kuwakamata wabunge wa CDM kwa zuio feki la mahakama? kwenda kumsearch Mdee home kama kibaka? kumsafirisha Bulaya mpaka Dar toka Mwanza nadhani navyo vyapasa kumpa credit
 
HUYUUU WA SASA ANAITWA KIRAHISIII N A MSTAAFU NYUMBANII KWA HOMESOPPING CENTRE WANAPIGA PICHA NA DOGO KAMA WATOTO WADOGO AISEE NI SHIDAAAA AEND E NA MWENZAKE KOVA
 
Hivi kuna IGP ambaye huwa haegemei upande wa CCM? Hilo la kuegemea upande wa CCM imekuwa ni tabia ya Ma- IGP wetu utadhani kama ni sifa ya ziada ndani ya Jeshi la Polisi inayotakiwa ili mtu apande vyeo haraka haraka!!
 
Na kuongoza Polisi kuwakamata wabunge wa CDM kwa zuio feki la mahakama? kwenda kumsearch Mdee home kama kibaka? kumsafirisha Bulaya mpaka Dar toka Mwanza nadhani navyo vyapasa kumpa credit
Hayo makandokando ni ya kawaida. Tupime mazuri na mabaya.
 
Hivi kuna IGP ambaye huwa haegemei upande wa CCM? Hilo la kuegemea upande wa CCM imekuwa ni tabia ya Ma- IGP wetu utadhani kama ni sifa ya ziada ndani ya Jeshi la Polisi inayotakiwa ili mtu apande vyeo haraka haraka!!
Nadhani ukiacha udhaifu wao, lakini nadhani katiba ya sasa ni ya mfumo wa chama kimoja katika vyama vingi. Taratibu tutafikatu.
 
Uko sahihi kabisa mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…