Kamanda Mpinga: Taarifa kuhusu tochi Mpya (Speed Radar)

Kamanda Mpinga: Taarifa kuhusu tochi Mpya (Speed Radar)

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,163
Reaction score
11,230
KUHUSU TOCHI MPYA(SPEED RADAR)

Ndugu wanahabari,
Ninapenda kuwatarifu uwepo wa vifaa vipya vya kisasa vya kupima mwendo wa magari. Vifaa vinauwezo wa kurekodi mwendo wa gari na wakati huo huo kuchukua picha ya mnato au video ya gari husika. Ili kuongeza ufanisi wa vifaa hivi, tumeelekeza askari wanaoshika vifaa hivyo wasivae sare ili wakishapata mwendo na picha za magari yaliyokiuka mwendo watoe taarifa kwa wenzao wenye sare wafanye ukamataji. Utaratibu huu unasaidia kuondoa dhana ya askari kujificha na kusimamisha magari kwa kushtukiza na kwa upande mwingine itapunguza tabia ya madereva kupeana ishara kuonyesha mahali walipo askari.

Ndugu wanahabari,
Jeshi la Polisi linawakumbusha Madereva na watumiaji wote wa barabara kuziheshimu sheria na kanuni za usalama barabarani. Aidha nachukua nafasi hii kuwakumbusha askari wote kusimamia sheria na kanuni za usalama barabarani bila woga au upendeleo kwa kuzingatia maadili mema ya kazi.

Aidha nawajulisha watumiaji wote wa barabara hususani madereva kuwa askari wataendelea kuwa wakali sana katika kipindi hiki kwa kusimamia sheria kikamilifu ambapo hatua kali za kisheria zitachuliwa kwa yeyote atakayekamatwa akivunja sheria za usalama barabarani.

Ndugu wanahabari,
Mwisho napenda kuwaasa wananchi na wadau wa usalama barabarani kwa ujumla, watupe ushirikiano zaidi kwa kutoa taarifa za uhalifu wa usalama barabarani, kufuata sheria, kanuni na maelekezo kwa ajili ya usalama wao watumiapo barabara.

Kila mmoja atambue haki na wajibu wake awapo barabarani ikiwa ni kuwa na subira na kujali watumiaji wengine wa barabara kwani kila mmoja anayo haki sawa ya kutumia barabara. Watoto wasiachwe kutembea barabarani bila ya uangalizi wa watu wazima.

ENDESHA SALAMA - OKOA MAISHA.

Imetolewa na:
MOHAMMED R.MPINGA – DCP,
KAMANDA WA POLISI,
KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI (T)
 
nikweli lakn hapo kwenye kuwaambia wavae nguo za kiraia ili wasijulikane ndo sijaelewa.
 
hizo speed rafar mpya usiombe ukutane nazo. nishapigwa 30,000 tayari.
 
Nimezipenda sana, leo mesafiri dar-moro, ABC bus kapigwa tatu njiani kapasuliwa 210,000/= mazima kilka moja 70 elfu
 
Nishasema na nikashauri jeshi hizi tochi hazisaidii bali ni mradi wa watu, maana wenye magar hupeana taarifa penye trafik na pasipo trafik wanatembea kama kawaida, wakipigwa bao walipishwa bila risit na wanaruhusiwa
 
Duu safari ya Tunduma,Songea,Sumbawanga,Bukoba,Musoma ishakua tabu
 
Kamanda Mpinga, tizama jinsi polisi unaowasimamia wanvyotumia hizi mashine kwa kumkomoa dereva,
Nilisimamishwa nikaambiwa nime-over speed from 50 to 57 nikajitetea nipewe uthibitisho, baada ya dakika 4 akaja askari amevaa kiraia na kipima mwendo kweli kina picha ya gari na mwendo kasi, ILA mahali nilipompita huyu askari hapakuwa kabisa kabisa karibia na ishara ya 50km/hr. nilikuja kupata kibao baada ya kumpita, sasa kwa kweli hata sasa hakuna haki maana hawasimami kwenye alama matokeo yake ndipo umeongeza rushwa na ugandamizaji.

Nadhani umenielewa
 
Najua uletaji wa tochi mpya ni kujaribu kupunguza ajali za barabarani kwa maderewa kutii amri za barabarani. Lakini kujihusisha tuu kwa polisi kukaa mabarabarani nchi nzima kila mahali kumdhibiti dereva anayekiuka amri naona haina tija. Barabara zetu zimefuatwa na wananchi kupenda kukaa karibu na barabara, kufanya biashara barabarani, hata kama barabara itapitishwa nje ya mji , wananchi wataifuata kama pale manyoni. na hivyo kila pahara penye makazi ya watu kuna udhibiti wa 50km/hr. SWALI, msafiri anatoka Dar kwenda Mwanza na kila baada ya km chache kuna 50km/hr atafika baada ya saa ngapi? Licha ya 50km/hr kuna matuta na polisi pia. Mfanya biashara ili apate faida ni muhimu kwenda haraka na kurudi haraka. Ningependa kuona madereva wote wafunzwe maadili zaidi ya kutii kwa mkandamizo wa polisi. Matuta yote yatolewe. Leseni zitolewe kwa madereva waliofuzu na timamu tu. Dereva huru na mzuri ni kama mfanyakazi yoyote hahitaji na kama atahitaji ni uangalizi kidogo - minimum supervision. Ikitokea ajali bahati mbaya ndipo polisi aende kupima.
 
Njia ya mwenge tegeta, pale IMTU wapo na camera yao.....wamenilamba sasa hivi
 
Nimezipenda sana, leo mesafiri dar-moro, ABC bus kapigwa tatu njiani kapasuliwa 210,000/= mazima kilka moja 70 elfu

Duh! Sipati picha dereva alivyokasirika....Itasaidia sana kupunguza ajali kwa namna hii
 
Najua uletaji wa tochi mpya ni kujaribu kupunguza ajali za barabarani kwa maderewa kutii amri za barabarani. Lakini kujihusisha tuu kwa polisi kukaa mabarabarani nchi nzima kila mahali kumdhibiti dereva anayekiuka amri naona haina tija. Barabara zetu zimefuatwa na wananchi kupenda kukaa karibu na barabara, kufanya biashara barabarani, hata kama barabara itapitishwa nje ya mji , wananchi wataifuata kama pale manyoni. na hivyo kila pahara penye makazi ya watu kuna udhibiti wa 50km/hr. SWALI, msafiri anatoka Dar kwenda Mwanza na kila baada ya km chache kuna 50km/hr atafika baada ya saa ngapi? Licha ya 50km/hr kuna matuta na polisi pia. Mfanya biashara ili apate faida ni muhimu kwenda haraka na kurudi haraka. Ningependa kuona madereva wote wafunzwe maadili zaidi ya kutii kwa mkandamizo wa polisi. Matuta yote yatolewe. Leseni zitolewe kwa madereva waliofuzu na timamu tu. Dereva huru na mzuri ni kama mfanyakazi yoyote hahitaji na kama atahitaji ni uangalizi kidogo - minimum supervision. Ikitokea ajali bahati mbaya ndipo polisi aende kupima.

Asante kwa kuliona hili mkuu!angetuondelea na kero ya kusimamishwa every 30-50 km just kuulizwa kadi ya gari sijui fire what what and leseni...huko ni kupotezeana muda tu!!
 
nikweli lakn hapo kwenye kuwaambia wavae nguo za kiraia ili wasijulikane ndo sijaelewa.
kutokuvaa sare hiyo ni mbinu ya kuongeza mapato kuliko kupunguza ajali. Kama faini jan -june ni zaidi ya 4 bn sioni sababu ya traffic polisi kutokubuni mbinu za kuongeza mapato
 
Hapa hesabu ya trafiki wa barabara kubwa lazima iongezeke maradufu
 
Asante kwa kuliona hili mkuu!angetuondelea na kero ya kusimamishwa every 30-50 km just kuulizwa kadi ya gari sijui fire what what and leseni...huko ni kupotezeana muda tu!!

Nakumbuka tulikua tunasafiri kuwahi mazishi Tabora
Yaani ni kero kubwa mmno aisee yaani njia nzima unasimamishwa na maswali ya ajabu ajabu tu
 
Someni Vizuri Muelewe.Kuna Askari Aina Mbili Mwenye Sare Ndiye Mwenye Camera Na Mwenye Uniform Atakukamata Baada Ya Mawasiliano Baina Yao.Imetulia Sana Hiyo!
 
Back
Top Bottom