Kamanda Kova anastaafu lini?

Kamanda Kova anastaafu lini?

Camilo Cienfuegos

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2015
Posts
19,228
Reaction score
68,246
Alitakiwa kustafu Oktoba mwaka jana, tukaambiwa ameongezewa mwaka mmoja na Mkulu aliyepita kwamba watastafu wote.

Sasa tunauliza ni lini kamanda wetu huyu atastafu, maana amekuwa na utumishi uliotukuka ndani ya jeshi letu la polisi, mwaka alioongezewa ushatimia.

Wenye kujua karibuni mtujuze
 
Wajihi wake umeanza kukunjamana kuashiria uzee.....
 
Aongezewe tena mwaka amalizie kazi ya kupunguza majambazi .Nafurahi kumwona mara kwa mara kwenye TV
 
ASTAFU ILI WAPUMBAVU WAANDAMANE? hakuna hilo itabidi aongezewe miaka 2 tena
 
Alitakiwa kustafu Oktoba mwaka jana, tukaambiwa ameongezewa mwaka mmoja na Mkulu aliyepita kwamba watastafu wote.

Sasa tunauliza ni lini kamanda wetu huyu atastafu, maana amekuwa na utumishi uliotukuka ndani ya jeshi letu la polisi, mwaka alioongezewa ushatimia.

Wenye kujua karibuni mtujuze


Hata KOVA akiondoka.... Maji ya washa washa bado yapo.... MANYUMBU yatafute route nyingine za kuandamana!
 
Binadam wasipoweza kumhukumu atahukumiwa na Mungu. Watu wengi hapa nchini wakipewa vyeo huwa wanakuwa vinara wa kutenda dhambi. Yaani hujitenga na uso wa Mungu, sijui kamanda kova kama umesalimika au lahh!!!!!!!!!!!!!!
 
namkubal sana kamanda,hajawahi kutokea kamanda kama kova katika jiji la dar.
 
maisha ya maaskari baada ya kustaafu huwa ni ya mateso,regrets na upweke,hakuna kazi mbovu kama upolisi
 
Hivi huwa amuogopi kuhoji habari za hao jamaa ??
 
maisha ya maaskari baada ya kustaafu huwa ni ya mateso,regrets na upweke,hakuna kazi mbovu kama upolisi
Sidhani kama ni kweli,ipo mifano mingi sana wa karibu zaidi ni Adad Rajab,wewe na yeye nani mpweke?
 
Tibaigana alikuwa kamanda tosha wa Dar; pengine kwavile alisomea degree ya sheria ambayo nadhani Kova hana!! Maadam mama Salma yuko Msoga na yeye ataondoka!!
 
maisha ya maaskari baada ya kustaafu huwa ni ya mateso,regrets na upweke,hakuna kazi mbovu kama upolisi

Ni kweli yaani hata nami baba mdogo kastaafu na cheo ACP alikuwa OC FFU ila kwa ana hali ngumu,hadi namhurumia.
 
Huyu jamaa tutammiss sana kwny runinga kila siku yeye
 
Ni kweli yaani hata nami baba mdogo kastaafu na cheo ACP alikuwa OC FFU ila kwa ana hali ngumu,hadi namhurumia.

Hakujipanga,alizoea vya bure,ACP nyumba anapata bure,fenicha usafiri.akajua ni vya milele
 
Back
Top Bottom