Wakati nipo kidato cha nne miaka kadhaa iliyopita nilimwambia mamangu nataka kwenda iringa kwa babu nikamwone ila naomba hela nimchukulie zawadi. Mamangu alisema nitakupa hela ukampe baba inatosha nikamwambia nataka nikampe zawadi mimi kama mimi. Nakumbuka mamangu kwa kuwa familia yetu ilikuwa ahueni alinipa hela nikamnunulia babu viwalo vya maana sana na nilifanya hivyo lengo kuu ni kuomba anipe shamba.
Nilipofika kwa babu nilitoa zawadi zangu na dagaa kama kilo 2 hivi na babu alinogewa sana na mjukuu wake wa kwanza kumuonyesha upendo ule. Babu aliniambia mjukuu wangu naona umekua naomba tuzunguke kwenye miliki zangu za ardhi nikuonyeshe mipaka nikasema haina shida babu, tulizunguka sana karibia masaa 4 maana alikuwa anamiliki mashamba/ mapori zaidi ya eka 500. Mwishoni mwa mizunguko nikaomba shamba akasema unataka kiasi gani nikasema hata eka 25 au 50 zinatosha babu.
Baada ya kuomba alisema nakupa kadri ulivyoomba na ntawambia wajomba zako na mama zako ili baadae wasikusumbue kama ntakufa karibuni. Akanionyesha mwisho wa shamba langu na kuanzia hapo kila likizo nilirudi iringa kuchimba mashimo ya miti na kupanda miti ya mbao na ikumbukwe sikuwashirikisha wazazi hivyo nilitumia mikono yangu na niliombea niwe na afya njema na hakika Mungu akabariki mwili, roho na nafsi vikawa katika usalama.
Hadi sasa namiliki shamba la miti zaidi ya eka 20 na nilianza kupanda mwaka 2009 na sijawahi kutumia kibarua yoyote labda kwa sasa kwa vile nafanya kazi serikalini.
Vijana tuna mda mwingi sana na nyumbani ardhi zipo ila hatujashituka na mda unaenda. TURUDI NYUMBANI YAJAYO YATAFURAHISHA