Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,250
- 113,636
Kwenye siasa za kidemokrasia, kuongelewa vibaya ni jambo la kawaida sana. Ni jambo la kutegemewa.
Kama kuna ambao hawaridhishwi na utendaji wako wa kazi, basi watu hao wana haki zote za kukuzungumzia vile wapendavyo, ikiwemo kukudhihaki, kukutukana, kukucheka, kukuzudoa na ‘kuku’ kivingine vyovyote waonavyo ni sawa.
Kwenye demokrasia watu wote hawapaswi kufikiri na kuzielezea fikra zao kwa namna moja.
Hivyo basi, kama huwezi kustahimili maoni ya watu juu ya utendaji wako wa kazi, yawe ni maoni ya kukusifia au kukukosoa, [1] usigombee nafasi yoyote ile ya kisiasa na [2] kama wewe tayari ni kiongozi wa kuchaguliwa, basi acha kazi ili uendelee na maisha yako binafsi kwa amani na utulivu.
Tulimsema Rais Magufuli na wapambe wake alipokuwa hai na sasa tutamsema Rais Samia.
Rejea hili bandiko langu toka 2017.
Naungana na wote wanaomsema Rais Samia, akiwemo Wakili Mwabukusi.
Narudia tena kusema kuwa, hii ni Tanzania na siyo Korea Kaskazini.
Wapambe wa Samia kama hamtaki mama yenu asemwe, mwambieni aache kazi. Kama hawezi kuacha kazi, basi atende vyema kwenye kazi zake.
Zaidi ya hapo, ni mwendokasi wa kumsema tu.
All gas no brakes. Gun barrel straight.
Kama kuna ambao hawaridhishwi na utendaji wako wa kazi, basi watu hao wana haki zote za kukuzungumzia vile wapendavyo, ikiwemo kukudhihaki, kukutukana, kukucheka, kukuzudoa na ‘kuku’ kivingine vyovyote waonavyo ni sawa.
Kwenye demokrasia watu wote hawapaswi kufikiri na kuzielezea fikra zao kwa namna moja.
Hivyo basi, kama huwezi kustahimili maoni ya watu juu ya utendaji wako wa kazi, yawe ni maoni ya kukusifia au kukukosoa, [1] usigombee nafasi yoyote ile ya kisiasa na [2] kama wewe tayari ni kiongozi wa kuchaguliwa, basi acha kazi ili uendelee na maisha yako binafsi kwa amani na utulivu.
Tulimsema Rais Magufuli na wapambe wake alipokuwa hai na sasa tutamsema Rais Samia.
Rejea hili bandiko langu toka 2017.
Kama huna ngozi nene usigombee urais!
Kuna mambo yanayoendelea sasa hivi hapa nchini ambayo siyaelewi kabisa. Inapotokea mtu maarufu anapomkosoa huyu rais wetu hadharani au inapotokea hata mtu tu wa kawaida akafanya au kusema kitu fulani ambacho kinaonekana kama kinamkosoa Rais Magufuli basi mtu huyo ataanza kuandamwa andamwa na...
www.jamiiforums.com
Naungana na wote wanaomsema Rais Samia, akiwemo Wakili Mwabukusi.
Narudia tena kusema kuwa, hii ni Tanzania na siyo Korea Kaskazini.
Wapambe wa Samia kama hamtaki mama yenu asemwe, mwambieni aache kazi. Kama hawezi kuacha kazi, basi atende vyema kwenye kazi zake.
Zaidi ya hapo, ni mwendokasi wa kumsema tu.
All gas no brakes. Gun barrel straight.