Kama una mpenzi ambaye yupo mbali yataka moyo sana

Hata hizo video call sio lazima, mahusiano ya mbali ukionesha kujali sana umeisha.
Ninaposema kuwasiliana simaanishi kupigiana simu kila sekunde na kila dakika hapana, ninamaanisha kile mnachokifanya mnapopigiana simu na kubwa namna mnavyokifanya.

Kwabahati nzuri siku hizi kuna teknolojia hivyo mnaweza kujikuta mkijiona kama mko chumba kimoja.
 
Ni kipengele sana mkuu
 
Huwa nashangaa watu wanao shangaa mahusiano ya mbali na kusema haiwezekani,Haiwezekani kama hakuna Upendo wa kweli.
Huwa natumia muda mwingi kuongea kuhusu mapenzi na si migogoro.

Kuna mengi ambayo yatasemwa hata yeye anasikia mengi lakini mkiamua kusema hapana, mimi najiamini wewe jiamini hivyo tuaminiane na tuache kuzungumza wivu tuzungumze mapenzi.
 
Watu mbona wana miaka sita na mahusiano yao.
yako poa kikubwa ni kumwamini mwenzako tu na kudumisha mawasiliano
Si kwamba haiwezekani kabisa mahusiano ya mbali ila tunaokataa ni baada ya kupigwa matukio na sababu ikiwa ni umbali.

Unakaa na mtu kwa mwaka mnaonana mara mbili ama tatu hii inataka sana watu wenye subira, msimamo thabiti na upendo wa kweli lkn ni wangapi wanaweza? Wangapi waaminifu? Labda uwe na bahati sana kupata wa kufanana nae ikiwa tu na wewe uko na hivyo vitu vinginevyo ukweli ni kwamba mahusiano ya mbali ni mizinguo.
 
nadra sana!shida tamaa zimewazid watu na hivyo wanashindwa kuhimili umbali nakuamua kuanza mahusiano mapya
 
.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…