Kama tuliwaondoa wakoloni, hawa watatushinda?

Kama tuliwaondoa wakoloni, hawa watatushinda?

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
970
Reaction score
1,941
Eti Amani !! amani, amani!!! Hii Tanzania kuna amani au kisiwa cha uvumilivu??? CCM ilipo sasa, kwa udhalimu wake, imetutoa kwenye kisiwa cha amani imetupeleka kwenye kisiwa cha uvumilivu. Je sisi vijana tupo tayari vizazi vyetu vije viishi kwenye kisiwa cha uvumilivu kama sisi??

Tukumbuke wazee wetu walivyojitoa bila kujali silaha za Muingereza, ili tu sisi tupate uhuru. Kwa nini sisi tunashindwa kupambania kizazi chetu kijacho, kisiishi maisha ya kidhalimu yanayoendeshwa na serikali ya CCM ???

CCM inasema vita vita, wao mbona waliandamana kwa Muingereza na vita haikutokea. Muingereza na bunduki zake na mizinga lakini wao waliendelea kuandamana bila kuogopa vitisho vya vifo, mpaka Muingereza akawapatia kile wanachotaka??? Yaani watu wanatekwa, damu zinamwagika, bado tu wananchi tunanyamaza??? Ni kitu gani duniani kina thamani kuliko uhai wa watu ??

Serikali inadidimiza uchumi, inauza rasilimali za taifa kiholela huku anazidi kuongeza deni la taifa ambalo litaathiri mpaka vizazi vijavyo. Tunamuangalia tu ??? Sisi ni wabinafsi kiasi gani mpaka tunashindwa hata kujitoa kwa ajili ya vizazi vyetu?? 29 OKTOBA tudai hatma ya taifa letu. KATIBA MPYA ni sasa. Mwisho wa UFISADI ni sasa. Mwisho wa UTEKAJI na UUAJI ni sasa.
 
Wakoloni walikuwa na chembe ya utu na ndio maana walikubali kuiachia nchi kwa njia ya amani bila vita.

Lakini hawa watawala wetu kukupa hata Katiba Mpya tu hawako tayari.

Hii inafanya ioneshe kuwa mazingira ambayo tupo nayo sasa ni very tight kuliko nyakati za Ukoloni.
 
Wakoloni hawakuwa fungal au kuwanyonga kina Nyerere au Mandela.

Wakoloni wasingepita na Mdude, Soka, Polepole au hata kumtendea Lissu hivi.
Waulize akina Chifu Songea Mbano na Mababu zetu wengine walionyongwa kwenye mibuyu.
 
Bhazungu are genetically More altruistic and humane kuliko watu Weusi na Brown.
Bhazungu hawakuzuia mikutano ya wapinzani wao.
judiciaries zao zilikuwa huru na uhakika wakupata haki yako ilikuwa ni mkubwa.
hawakuwa na tactics za kuua na kuteka wakosoaji wao.hizi ni moja ya vitu vichache vinaonyesha kuwa vita ya mkoloni dhidi ya Mkoloni mweupe ilikuwa ni Rahisi kidogo kuliko vita ya kumkabili Mkoloni Mweusi.
kumkabili mtu mweusi over madaraka unakuwa una face kiumbe katili kabisa Pengine kuliko Race zingine zote duniani.
Jambo likishahusu madaraka,kaa mbali na Mtu mweusi.
Mkoloni Mweusi na incompetent na mpumbavu..yuko radhi nchi nzima mfe abaki yeye na watoto wake na walinzi wake.
 
Wakoloni hii hapa hapakuwa kwao hawa watu hapa ni kwao na wamejiridhisha wanaweza kufanya wanachotaka
 
Aiseee! Umeongea kwa uchungu sana hadi nimehisi kutetemeka maini, wazee wetu kwa kweli walijitoa haswa kwa ajiri yao na vizazi vijavyo, lakini leo hii vijana wa hovyo tumebweteka tu tunapelekwa kama ng'ombe buchani, ccm ni mbwaa kabisa.
 
Waulize akina Chifu Songea Mbano na Mababu zetu wengine walionyongwa kwenye mibuyu.

Nimekuuliza kina Nyerere, Mandela, na wa namna hiyo kwa makusudi mazima kuwa wakipigania haki zao waziwazi kwa amani kama Lissu, Polepole, Soka, Mdude na wengi wao. Majibu yako tafadhali.
 
Nimekuuli za kina Nyerere, Mandela, na wa namna hiyo kwa makusudi mazima kuwa wakipigania haki zao waziwazi kwa amani kama Lissu, Polepole, Soka, Mdude na wengi wao. Majibu yako tafadhali.
Lengo langu ni kueleza kuwa Wakoloni waliua sana, Wajerumani wameacha makaburi ya halaiki kote Tanganyika kwahiyo kusema wakoloni weupe walikuwa wazuri ni upotoshaji.

Sema na hivi vyama vya uhuru navyo vimeanza kuiga mbinu za wakoloni baada ya kuona vimechokwa
 
Lengo langu ni kueleza kuwa Wakoloni waliua sana, Wajerumani wameacha makaburi ya halaiki kote Tanganyika kwahiyo kusema wakoloni weupe walikuwa wazuri ni upotoshaji.

Sema na hivi vyama vya uhuru navyo vimeanza kuiga mbinu za wakoloni baada ya kuona vimechokwa

Lengo langu ni kueleza hawakuwa wema lakini walikuwa na nafuu.

Hawakuwauwa au kuwafunga wapigania haki kwa amani.

Kama siku zile kama leo waungwana waliuzwa na wenzao kama walivyokuwa wakifanya waliokwenda shaumma au wanavyoendelea kufanya masalio yao leo.

Ogopa sana wasaliti na hasa wa ndani!
 
Lengo langu ni kueleza hawakuwa wema lakini walikuwa na nafuu.

Hawakuwauwa au kuwafunga wapigania haki kwa amani.

Kama siku zile kama leo waungwana waliuzwa na wenzao kama walivyokuwa wakifanya waliokwenda shaumma au wanavyoendelea kufanya masalio yao leo.

Ogopa sana wasaliti na hasa wa ndani!
Hakuna unafuu wowote mfano wa Mandela kuachiwa ni pressure kutoka katika mafaifa ya nje.

Lakini waliua sana Steve Bantu Biko,Chris Hani na wengine wengi sana.
 
Hakuna unafuu wowote mfano wa Mandela kuachiwa ni pressure kutoka katika mafaifa ya nje.

Lakini waliua sana Steve Bantu Biko,Chris Hani na wengine wengi sana.


Hata wale waliokwenda shaumma wana mawazo kama wewe. Zaidi sana wanaendelea kuuza watu Tena Kwa bashasha. Vipi mngali mnajuliana nao hali?
 
Eti Amani !! amani, amani!!! Hii Tanzania kuna amani au kisiwa cha uvumilivu??? CCM ilipo sasa, kwa udhalimu wake, imetutoa kwenye kisiwa cha amani imetupeleka kwenye kisiwa cha uvumilivu. Je sisi vijana tupo tayari vizazi vyetu vije viishi kwenye kisiwa cha uvumilivu kama sisi??

Tukumbuke wazee wetu walivyojitoa bila kujali silaha za Muingereza, ili tu sisi tupate uhuru. Kwa nini sisi tunashindwa kupambania kizazi chetu kijacho, kisiishi maisha ya kidhalimu yanayoendeshwa na serikali ya CCM ???

CCM inasema vita vita, wao mbona waliandamana kwa Muingereza na vita haikutokea. Muingereza na bunduki zake na mizinga lakini wao waliendelea kuandamana bila kuogopa vitisho vya vifo, mpaka Muingereza akawapatia kile wanachotaka??? Yaani watu wanatekwa, damu zinamwagika, bado tu wananchi tunanyamaza??? Ni kitu gani duniani kina thamani kuliko uhai wa watu ??

Serikali inadidimiza uchumi, inauza rasilimali za taifa kiholela huku anazidi kuongeza deni la taifa ambalo litaathiri mpaka vizazi vijavyo. Tunamuangalia tu ??? Sisi ni wabinafsi kiasi gani mpaka tunashindwa hata kujitoa kwa ajili ya vizazi vyetu?? 29 OKTOBA tudai hatma ya taifa letu. KATIBA MPYA ni sasa. Mwisho wa UFISADI ni sasa. Mwisho wa UTEKAJI na UUAJI ni sasa.
Mara nyingi katika mijadala ya kisiasa nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla, lawama nyingi hupelekwa kwa vyama tawala kama vile CCM, kana kwamba matatizo yote ya kijamii na kiuchumi yanatokana na uongozi wao. Hata hivyo, hoja ya msingi inabaki kuwa si chama pekee kinachoshikilia mizizi ya matatizo ya bara letu, bali mfumo wa dunia uliojengwa katika msingi wa ukoloni wa kiuchumi unaoendelea hadi leo.

Baada ya uhuru wa kisiasa katika miaka ya 1960, mataifa ya Afrika yalipata kile kinachoitwa uhuru wa bendera — uwezo wa kuinua bendera na kuwa na wimbo wa taifa — lakini hayakupata uhuru wa kiuchumi. Mifumo ya kifedha, kisheria, kielimu na kibiashara ilibaki ikidhibitiwa na taasisi na mataifa yaliyokuwa makoloni. Matokeo yake, tunajikuta bado tukiishi katika “nyumba ya kupanga” — ardhi yetu, rasilimali zetu, na nguvu kazi yetu, lakini hatuna mamlaka kamili ya kuamua namna ya kuzitumia kwa faida ya watu wetu.

Leo hii, Afrika inauza malighafi kwa bei ndogo na kununua bidhaa zilizokamilika kwa gharama kubwa. Bei ya dhahabu, mafuta, pamba, au kahawa inaamuliwa katika masoko ya nje, si katika nchi zinazozalisha. Hata mikopo na misaada inayotolewa kwa mataifa yetu mara nyingi huambatana na masharti yanayolazimisha utekelezaji wa sera zinazolinda maslahi ya watoa mikopo badala ya wananchi wa Afrika.

Wale viongozi wachache waliothubutu kupinga mfumo huu — kama Thomas Sankara, Patrice Lumumba, na Muammar Gaddafi — waliondolewa madarakani au kuuawa kwa mikono ya nguvu za kimataifa. Hii inaonyesha kuwa tatizo la Afrika si uongozi wa mtu mmoja au chama fulani, bali ni mfumo wa utegemezi uliopangwa makusudi kutuacha tukiwa watumwa wa kiuchumi katika ardhi yetu wenyewe.

Suluhisho haliko katika kubadilisha vyama tu, bali katika mabadiliko ya kifikra na kiuchumi: kuwekeza katika uzalishaji wa ndani, elimu bunifu, teknolojia, na umoja wa bara la Afrika katika maamuzi ya uchumi. Ni hapo tu ndipo tutakapoweza kusema tumevuka kutoka katika uhuru wa bendera kwenda kwenye uhuru wa kweli wa kiuchumi na kifikra.
 
Mara nyingi katika mijadala ya kisiasa nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla, lawama nyingi hupelekwa kwa vyama tawala kama vile CCM, kana kwamba matatizo yote ya kijamii na kiuchumi yanatokana na uongozi wao. Hata hivyo, hoja ya msingi inabaki kuwa si chama pekee kinachoshikilia mizizi ya matatizo ya bara letu, bali mfumo wa dunia uliojengwa katika msingi wa ukoloni wa kiuchumi unaoendelea hadi leo.

Baada ya uhuru wa kisiasa katika miaka ya 1960, mataifa ya Afrika yalipata kile kinachoitwa uhuru wa bendera — uwezo wa kuinua bendera na kuwa na wimbo wa taifa — lakini hayakupata uhuru wa kiuchumi. Mifumo ya kifedha, kisheria, kielimu na kibiashara ilibaki ikidhibitiwa na taasisi na mataifa yaliyokuwa makoloni. Matokeo yake, tunajikuta bado tukiishi katika “nyumba ya kupanga” — ardhi yetu, rasilimali zetu, na nguvu kazi yetu, lakini hatuna mamlaka kamili ya kuamua namna ya kuzitumia kwa faida ya watu wetu.

Leo hii, Afrika inauza malighafi kwa bei ndogo na kununua bidhaa zilizokamilika kwa gharama kubwa. Bei ya dhahabu, mafuta, pamba, au kahawa inaamuliwa katika masoko ya nje, si katika nchi zinazozalisha. Hata mikopo na misaada inayotolewa kwa mataifa yetu mara nyingi huambatana na masharti yanayolazimisha utekelezaji wa sera zinazolinda maslahi ya watoa mikopo badala ya wananchi wa Afrika.

Wale viongozi wachache waliothubutu kupinga mfumo huu — kama Thomas Sankara, Patrice Lumumba, na Muammar Gaddafi — waliondolewa madarakani au kuuawa kwa mikono ya nguvu za kimataifa. Hii inaonyesha kuwa tatizo la Afrika si uongozi wa mtu mmoja au chama fulani, bali ni mfumo wa utegemezi uliopangwa makusudi kutuacha tukiwa watumwa wa kiuchumi katika ardhi yetu wenyewe.

Suluhisho haliko katika kubadilisha vyama tu, bali katika mabadiliko ya kifikra na kiuchumi: kuwekeza katika uzalishaji wa ndani, elimu bunifu, teknolojia, na umoja wa bara la Afrika katika maamuzi ya uchumi. Ni hapo tu ndipo tutakapoweza kusema tumevuka kutoka katika uhuru wa bendera kwenda kwenye uhuru wa kweli wa kiuchumi na kifikra.
Wewe ndio akili yako bado imelala kwa Wakoloni. Kuwaondoa Wamasai kwenye ardhi yao ni Mkoloni?? Kuuza bandari kwa muwekezaji uchwara ni Mkoloni?? Kuwabambikia kesi ndugu zako tena wa damu ili tu uwadhoofishe kisiasa ni Mkoloni?? Kuwateja na kuwapoteza raia wa nchi yako mwenyewe ni Mkoloni?? Kujilimbikizia ukwasi wa kutisha kwa fedha za umma kisa madaraka uliyonayo nayo ni Mkoloni??

Hayo yote uliyoyazungumza hayana tija bali ni fikra mgando. Huna tofauti na mtu aliyeambiwa daraja ni bovu asipitishe gari. Yeye akashupaza shingo. Kafika katkati daraja limekwenda pamoja na yeye. Kanusurika kifo, anaulizwa kulikoni eti anamsingizia shetani. Upuuzi mtupu.
 
Back
Top Bottom