Kama sio Rais Magufuli, mnamtaka nani?

Kama sio Rais Magufuli, mnamtaka nani?

Kalbandika

Member
Joined
Oct 10, 2010
Posts
40
Reaction score
25
Nakumbuka kamsemo kazamani kidogo pale mtu unapopata kitu kizuri halafu bado unalalamika. Utasikia mtu anakuambia 'Mungu akupe nini, au gunia la chawa?

Hii ni kauli ambayo inatolewa kwa watu ambao hawana shukrani, hawana jema. Kila kitu kwao kibaya. Ukiwa mkali utasikia dah, fulani mkali sana. Ukiwa mpole utasikia dah, fulani mpole sana. Ukiwa kati kati, utasikia dah, fulani haelewiki.

Hakika, tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutujalia kumpata Rais Magufuli. Wengi wasiofikiri vizuri wanaponda kila kitu bila kuangalia uhalisia wa jambo husika.

Mfano mzuri, Mheshimiwa Rais Magufuli amesema wazi juu tetemeko la ardhi lililoharibu vitu na watu Mkoani Kagera. Amesema wazi Serikali haina uwezo wa kusaidia kila kitu. Inabidi jamii na watu wenyewe tufanye kazi na kusaidiana. Haiwezekani mtu nyumba yake imepata ufa anasubiri Serikali ije irekebishe ufa.

Rais wetu ni mkweli, hana ubabaishaji. Nyeupe anasema ni Nyeupe, na nyeusi ni nyeusi.

Watanzania mnataka nini badala ya JPM? Mheshimiwa Waziri Mkuu amepewa kazi ya kusimamia urejeshwaji wa hali ya Mkoa wa Kagera. Ameambiwa wazi kabisa na Mhe Rais juu ya matumizi yenye tija ya michango.

Tumuunge mkono JPM, tuache kufuata maneno ya wanasiasa wa matukio.
 
Nakumbuka kamsemo kazamani kidogo pale mtu unapopata kitu kizuri halafu bado unalalamika. Utasikia mtu anakuambia 'Mungu akupe nini, au gunia la chawa?

Hii ni kauli ambayo inatolewa kwa watu ambao hawana shukrani, hawana jema. Kila kitu kwao kibaya. Ukiwa mkali utasikia dah, fulani mkali sana. Ukiwa mpole utasikia dah, fulani mpole sana. Ukiwa kati kati, utasikia dah, fulani haelewiki.

Hakika, tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutujalia kumpata Rais Magufuli. Wengi wasiofikiri vizuri wanaponda kila kitu bila kuangalia uhalisia wa jambo husika.

Mfano mzuri, Mheshimiwa Rais Magufuli amesema wazi juu tetemeko la ardhi lililoharibu vitu na watu Mkoani Kagera. Amesema wazi Serikali haina uwezo wa kusaidia kila kitu. Inabidi jamii na watu wenyewe tufanye kazi na kusaidiana. Haiwezekani mtu nyumba yake imepata ufa anasubiri Serikali ije irekebishe ufa.

Rais wetu ni mkweli, hana ubabaishaji. Nyeupe anasema ni Nyeupe, na nyeusi ni nyeusi.

Watanzania mnataka nini badala ya JPM? Mheshimiwa Waziri Mkuu amepewa kazi ya kusimamia urejeshwaji wa hali ya Mkoa wa Kagera. Ameambiwa wazi kabisa na Mhe Rais juu ya matumizi yenye tija ya michango.

Tumuunge mkono JPM, tuache kufuata maneno ya wanasiasa wa matukio.

Wanasiasa wetu wamezoea mazingaombwe.

Mara oooh giza nene three weeks baada.ya hapo mkataba wa.richmond kumbe maji yanafunguliwa ovyo mtera.

Mara oooh.nitawaletea mvua toka Thailand...
 
Waache miaukule ilalamike. Sisi tunajenga nchi. Ananchi wanatuelewa sana
 
Wanasiasa wetu wamezoea mazingaombwe.

Mara oooh giza nene three weeks baada.ya hapo mkataba wa.richmond kumbe maji yanafunguliwa ovyo mtera.

Mara oooh.nitawaletea mvua toka Thailand...
Tehetehetehetehe. Ilikuwa nchi ya deal hii. Sasa heshima ya nchi inaanza kurejea
 
Nakumbuka kamsemo kazamani kidogo pale mtu unapopata kitu kizuri halafu bado unalalamika. Utasikia mtu anakuambia 'Mungu akupe nini, au gunia la chawa?

Hii ni kauli ambayo inatolewa kwa watu ambao hawana shukrani, hawana jema. Kila kitu kwao kibaya. Ukiwa mkali utasikia dah, fulani mkali sana. Ukiwa mpole utasikia dah, fulani mpole sana. Ukiwa kati kati, utasikia dah, fulani haelewiki.

Hakika, tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutujalia kumpata Rais Magufuli. Wengi wasiofikiri vizuri wanaponda kila kitu bila kuangalia uhalisia wa jambo husika.

Mfano mzuri, Mheshimiwa Rais Magufuli amesema wazi juu tetemeko la ardhi lililoharibu vitu na watu Mkoani Kagera. Amesema wazi Serikali haina uwezo wa kusaidia kila kitu. Inabidi jamii na watu wenyewe tufanye kazi na kusaidiana. Haiwezekani mtu nyumba yake imepata ufa anasubiri Serikali ije irekebishe ufa.

Rais wetu ni mkweli, hana ubabaishaji. Nyeupe anasema ni Nyeupe, na nyeusi ni nyeusi.

Watanzania mnataka nini badala ya JPM? Mheshimiwa Waziri Mkuu amepewa kazi ya kusimamia urejeshwaji wa hali ya Mkoa wa Kagera. Ameambiwa wazi kabisa na Mhe Rais juu ya matumizi yenye tija ya michango.

Tumuunge mkono JPM, tuache kufuata maneno ya wanasiasa wa matukio.

Sawa ni kweli ukuta umepasuka ziba mwenyewe...lakini ukuta umeanguka na babab na mama...na wengine majeruhi watoto wana lala nje..nao hao watoto wafanayeje?
majanga ni majanga lakini moja ya kazi za serikali ni hili wakati wa maaafa....sasa si zimechangwa zaidi ya mabilioni mangapi sijui...si wape tenda JKT na Mafunzo ...wakawajengee watu kwa hizo pesa zilizo changwa..

badala yake Membe angefaa sana...
 
Hata nchi zilizoendelea kukiwa na maafa serikali inasadia. Lousiana Marekani walipatwa na mafuriko wanajeshi wakaenda kuwaopoa wananchi na magari yao marefu. Italia walikuwa na matetemeko na serikali ilienda kusaidia. Uongozi sio tu kupayuka na kudhibiti upinzani.
 
Hivi kutekelezewa vipaumbele vyetu ni ombi au ? Tunacho taka maisha yaboreshwe, hatutaki kelele na majungu.......
 
Yaani mimi natamani Magu awe Rais kwa miaka 50. Atunyooshe kwanza ndio apumzike
Miaka 50 ya nini!
Hata mwaka haujaisha mafisadi na vibaraka wao wamelia vya kutosha. Miaka 10 inawatosha kabisa!
 
Miaka 50 ya nini!
Hata mwaka haujaisha mafisadi na vibaraka wao wamelia vya kutosha. Miaka 10 inawatosha kabisa!

Sio mafisadi na vibaraka wao tu, hata watumiaji sukari, wahanga wa majanga, wanafunzi wa ualimu, Wanzanzibari au mtu yoyote asiyekuwa Msukuma wa CCM.
 
Sio mafisadi na vibaraka wao tu, hata watumiaji sukari, wahanga wa majanga, wanafunzi wa ualimu, Wanzanzibari au mtu yoyote asiyekuwa Msukuma wa CCM.

Watumiaji sukari - Mimi pia nimtumiaji mkubwa wa sukari. Lakini katika kupambana na ufisadi lazima uwe tayari kujitolea na hakuna tofauti kwa mafisadi wa sukari. Hii ni kwa maisha bora ya siku zijazo.

Wahanga wa majanga - Kama unaongelea tetemeko. Pesa za kuwasaidia zimetafutwa na serikali na Waziri Mkuu anasimamia zoezi la kuwasaidia waathirika.

Wanafunzi wa ualimu - Naomba unisadie hapa, nimepitiwa. Kuna tatizo gani?

Wanzanzibar - Rais wa Zanzibar kapatika wasubiri tena 2020. Wimbo wapinzani wanaoimba leo wameimba tangia vyama vingi vilipoanzishwa, bara na visiwani, hata Mrema alipogombea kupitia NCCR alidai Mkapa alimwibia kura. CUF watumie kipindi hiki kuangalia ni wapi waloshindwa na kujirekebisha badala kuendelea kudanganya la sivyo 2020 wimbo utakuwa ni huo huo!

Msukuma wa CCM - Wacha kuangalia mambo kwa jicho la ukabila au udini. Cha muhimu wawe wachapaka kazi na sio mafisadi.
 
Watumiaji sukari - Mimi pia nimtumiaji mkubwa wa sukari. Lakini katika kupambana na ufisadi lazima uwe tayari kujitolea na hakuna tofauti kwa mafisadi wa sukari. Hii ni kwa maisha bora ya siku zijazo.
Hao mafisadi ni akina nani? Talk is cheap. Haitaji akili nyingi kuimba ngonjera za "mafisadi". Uongozi siyo kuadhibu nchi nzima kwa makosa ya wachache, ambao wengi wao ni wa chama chake. Maamuzi ya kukurupuka siyo dili.

Wahanga wa majanga - Kama unaongelea tetemeko. Pesa za kuwasaidia zimetafutwa na serikali na Waziri Mkuu anasimamia zoezi la kuwasaidia waathirika.
Litachukua muda gani hilo? Je, serikali inaelewa maana ya "dharura"?

Wanafunzi wa ualimu - Naomba unisadie hapa, nimepitiwa. Kuna tatizo gani?
Hukumbuki "vilaza" waliotimuliwa bila huruma utafikiri walijiandikisha wenyewe hapo chuoni.

Wanzanzibar - Rais wa Zanzibar kapatika wasubiri tena 2020. Wimbo wapinzani wanaoimba leo wameimba tangia vyama vingi vilipoanzishwa, bara na visiwani, hata Mrema alipogombea kupitia NCCR alidai Mkapa alimwibia kura. CUF watumie kipindi hiki kuangalia ni wapi waloshindwa na kujirekebisha badala kuendelea kudanganya la sivyo 2020 wimbo utakuwa ni huo huo!
"Rais" wa Zanzibar hakupatikana, ameteuliwa. Kila mtu anajua hakuna tume huru kwa hiyo hata mwaka 2020 wimbo utakuwa huo huo. Lakini madhara yake ni wafadhili kuwanyima misaada, hata kukitokea majanga serikali inabidi ipitishe bakuli kuomba michango.

Msukuma wa CCM - Wacha kuangalia mambo kwa jicho la ukabila au udini. Cha muhimu wawe wachapaka kazi na sio mafisadi.
Sijali mambo ya kabila au dini, kwa sababu hata Kikwete nilikuwa nampinga kwa hiyo. Watu tunajali performance ya kiongozi, siyo mbwembwe zake.
 
Mbona watu hawajibu swali, wanaleta porojo tu? Sawali ni kua je, MNAMTAKA NANI awe mbadala wa JPM?
 
Back
Top Bottom