Kama si mzee Aboud Jumbe kusingekuwapo na CCM

Napenda hii thread iendelee ili nijifunze mengi kuhusu walau historia za wazee wetu
 
Hivi ni kweli Sheikh Aboud Jumbe Mwinyi alitaka kuvunja muungano?

Nini kilikuwa kiini cha "machafuko ya hali ya hewa" Zanzibar yaliyopelekea kujiuzulu kwake?

Seif Sharif Hamad alimchongea nini kwa Nyerere wakati akiwa waziri kiongozi?

Hamad aliteta nini na Nyerere Butiama baada ya kutoka CCM?

Ndiyo kwa mantiki ya Nyerere na wengi sasa kuwa kudai haki za Zanzibar
ni kutaka kuvunja Muungano.
Si kweli kwa mantiki ya makubaliano ya Muungano. Makubaliano ya Muungano yalitaka baada ya miaka 10 kuangaia iwapo Muungano unaenda kwa mujibu wa makubaliano ya pande mbili. Pia kulitakiwa kuwe na mahakama ya Katiba. Baada ya kupita miaka 20 bila ya kufanyika hayo Wazanzibari walitaka kuishitaki serikali ya Muungano kwa kukiuka makubaliano na hicho ndio kilisababisha purukushani yote hiyo
Swala la pili limwshajibika na kuhuu suala la Seif Sharif kumchongea Jumbe ni chuki binafsi za Seif kwa Aboud Jumbe baada ya kumngowa uwaziri wa Elimu Zanzibar.Wakati wa Jumbe Seif hakuwa Waziri Kiongozi bali alikuwa Mkuu wa secretariate moja katika CCM. Seif na wenzake waliingia mtego wa Nyerere na itikadi kali ya CCM.
Ama la Nyerere na Seif Butiama sina uelewa nalo, pengine MWIBA atatueleza tukimuuomba.
 
Kama kuna binaadamu m-binafsi hapa Tanzania aliyewahi kuishi basi Nyerere anaongoza, si kuwa aliifuta historia ya mashujaa wengine waliotoa mali zao na roho zao kwa nchi hii bali aliwafanya wakaonekana maadui wa nchi hii, na kujigeuza yeye kwa kila sifa inayomstahiki na isiyomstahiki,mbali na Jumbe watu kama Bibi Titi Moh'd, Oscar Kambona,Kasela Bantu n.k waliomtengeneza na Kumpromote Nyerere enzi hizo, walifikia hata kutoa fedha na mali zao kumpeleka Nyerere U.N akawasemee kwa kuwa tu alijua kingereza, wengine walimbeba hata pale alipotaka kupinduliwa (Oscar kambona), shukurani za mtu huyu kwa watu wote hao ni kama za punda, aliwapiga mateke na kuwanyanyasa kama vile hakuwahi kuwajua seuza kupata hisani zao,Manyanyaso aliyomfanyia BB TT, kwa kisingizio cha kutaka kumpindua, yanasikitisha hata leo ukiyasoma tu, lau kama kungekuwa na vyombo vya habari siku hizo kama ilivyo sasa vikapaza sauti zao kwa madhila waliyofanyiwa "mashujaa waliosahaulika" nchi hii na "kufutwa" historia na michango yao ya ujenzi wa taifa hili na Mwalimu Nyerere kwa makusudi, hakuna mtu angelitoa chozi lake kwa kifo chake.

Si wameondowa!!!! Thanks
 
Ama kwa Mzee Jumbe atakumbukwa kwa Mengi, sio Kuiuwa ASP na Kuiunganisha na TANU tu hata na Kwa Mauaji pia aliyafanya, walipokamatwa watu 20 waliotuhumiwa kuwa walikuwa na nia ya Kuipinduwa Serikali ya ASP(KARUME) na Watu wale wakaletwa katika Mkutano wa Hadhara Mzee Karume al;isema kuwa hawa watakaa gerezani na Kuchunga Ngombe na walipelekwa gerezani ni kweli Serikali ya KARUME ilijuwa kuwa wale watu hawakuwa na nia ya kupinduwa Serikali bali walikuwa ni wafanya Biashara ya Magendo ya Karafuu kati ya Pemba na Kenya, inasekana hata Mzee Kenyata aliweaombea kwa Karume wasiuawe na Karume hakuwauwa waliishi gerezani kwa Amri ya Karume kuwa wapewe kazi Ngumu na Chakula Kidogo na Wakiumwa wasitibiwe, mmoja wao alikufa kwa homa bila ya kutibiwa na wakabakia 19. Waliishi hadi pale Jumbe aaalipochukuwa madaraka walikuwa hai lakini la kusikitisha watu wale waliuliwa pale Jumbe alipokwenda katika ziara yake ya Kwanza India na Kurudi hawa WADHULUMIWA Wakiwa wameshauliwa na Kanali Sefu Bakari akishirikiana na Abdalla Natepe, Jumbe hili alilijuwa na hakuchukuwa hatuwa yeyote na kwa kuwa alikaa kimya ni dalili rasmi ya kuwa MAUAJI yale yalipata Baraka zake na hii ndio moja ya Sababu alipoaanza mbinu zake za kuitowa Zanzibar ndani ya Muungano Kisiri siri na Vijana kama akina SEIF SHARIF, SALIMINI AMOUR, ALI AMEIR MWAKANJUKI, Walishirikiana kumuondowa Jumbe katika Madaraka kama vile walivyomuondowa kwa sababu alishaonyesha dalili za kuangamiza kila aliekuwa na mawazo ya Kumpinga huo ndio Ukweli lakini hausemwi. Ijapo kuondolewa kwake hakukufuata taratibu za Kidemokrasia.
 
Junius,
Hivi si kweli kuwa Bibi Titi alishiriki katika mipango ya kumpindua Nyerere? Pamoja na Kambona? Ubinafsi unaousema ni upi? Wa kumsamehe Bibi Titi asiwekwe kitanzi? Aliyetoa fedha zake kumpeleka Nyerere UN alikuwa Mzee Rupia. Kambona naye alibebwa tu na TANU. Aliifutaje historia ya mashujaa? Ni wapi Nyerere ameandika historia ya juhudi za ukombozi? Acheni kupindisha ukweli wakati tunaoujua ukweli bado tupo hai.



Ukweli kawaulize kina Sykes na KK Rupia alichupia gari tu.
 
Kwa wote wana-JF waliochangia mada hii hadi sasa, mnasahau kwamba wakati Jumbe (pamoja na wengine) alipokuwa anajibidiisha kuiasisi CCM, hakujua kwamba yangemkuta yaliyomkuta. Ne mengineyo mengi yanayowakuta Wazanzibari hadfi kufikia majuto kwa wengi wao.

Kwa Wazanzibari, kuanzishwa kwa CCM kulikuwa 'ironical' -- kwani ilikuwa ni mwanzo wa mwisho wa 'sauti' huru ya Wazanzibari, kwani baada ya hapo masuala yote kuhusu mustakabali wa visiwa hivyo yalikuwa yanaamuliwa Dodoma. Hata masuala ya kuchagua viongozi wao.

Matokeo yake ni kwamba CCM imeziduwaza na kuzidumaza fikra za Viongozi wa Zanzibari kiasi kwamba misimamo yao mingine inasikitisha kweli kweli.

Nitatoa mfano. Ktk uchaguzi wa 2005, pamoja na kwamba ilionekana kuwa ni zamu ya Visiwani (ingawa haiko ki-Katiba) kutoa rais, na kwamba walikuwa na candidate ambaye alikuwa very strong, viongozi wa huko, kwa sababu zisizokuwa na msingi kabisa, waliamua kuwa potelea mbali, na kuonekana kuwaambia watu wa bara: "endeleeni tu nyinyi kutoa Rais tena! Sisi hapana."

Halafu hapo hapo wanapiga kelele ya kutaka usawa baina ya pande mbili za muungano!

Na ndio maana hao waliowadumaza viongozi wako tayari kuleta majeshi Zanzibar kuuwa na kudhalilisha juhudi za wananchi za kuleta mabadiliko ya kweli. Na ndio maana Salmini baada ya kushindwa alikimbilia kwa huyo Mzee naye akambeba.
 
Hivi ni vitu vinahitaji kuwekwa wazi wakati huu-kwa manufaa ya historia ya nchi yetu na vizazi vyetu vijavyo. Hivi nini kilijiri. Msituambiue tu -Kuchafuka kwa hali ya hewa ya Kisiasa. Hii ni khushi- haijitoshelezi.

Kilichojiri ni kuwa Aboud Jumbe alijuwa kuwa kwa kutumia nguvu asingefika pahala hivyo alitafuta Mwanasheria ambaye aliitetea ASP wakati wa ukoloni na kumpa kazi ya kutengeneza mashitaka juu ya kuvunjwa kwa makubaliano ya Muungano. Kwa bahati mbaya Jumbe alishajenga maaduwi mipongoni mwao akiwa Sheif Sharifu. Kutokana na uadui huo au pengine kutokana na hesabu zao za kupata madaraka Kina Seif waliuiba Waraka uliotayarishwa na Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi waliotaka vipengele yote vya makubaliano vifuatwe ikiwa pamoja na Katiba mpya, Kuupitia Muungano kila baada ya kipindi cha miaka 10 na kuundwa mahakama ya Katiba itakayotowa uamuzi upande mmoja unapovunja makubaliano.
Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi walobakia katika Wajumbe wa mwanzo walienda kikaoni Dodoma ili kwenda kudai haki ya Zanzibar.
Kwenye Kikao Nyerere kwa hila yake aliwatumia kina Seif kama Wazanzibar na kuutowa waraka ulioibiwa na kilichofuata ilikuwa kama yaliyowapata G55 isipokuwa hapa kulitangazwa uhaini.
Baadhi ya Wanamapinduzi kwa ujasiri wao walimueleza Nyerere usoni mwake kuhusu rangi yake halisi na wakasekwa ndani na wengine ndio hivyo, walifyata mkia na kumuacha shujaa wa JASUSI kuwatukana apendavyo na kuwaambia hawakusoma kwa kuhesabu 1+1=3.
Seif akawa shujaa machoni mw Nyerere eti analinda Muungano,lakini walipokuja kutambuana hali ndiyo hiyo.
 
BABYLON,
Hivi juu ya jitihada zake julias kuweka lugha ya kiswahili iwe ndio ya taifa bado baadhi yetu inatupa tabu ?mimi sijazungumzia zimbabwe hapa .Vereje leo hii kiumbe huyu analeta ya zimbabwe, matatizo ya zimbabwe ni yao wenyewe. mimi nazungumzia yaliyo yetu kila mtu hulia mama yangu na halii mama yetu

Mkuu wangu unalia na Aboud Jumbe kwani yeye mama yako?..unalia kwa kipi haswa wakati huyu mtu ni wa kuchora yaani hakuwa na nafasi yoyote zaidi ya kuwa replacement ya Marehemu Karume..

Waniita KIUMBE... duh ama kweli umenichoka... sema kabisa Bangubangu maanake ndio zenu nyie kuchovya.. Na utaniita majina yote lakini jua moja nazungumza lugha ya KIUME toka sauti bara sibani sauti wala kuashiria kwa kwa vidole..
Hivyo kuwa msikivu na weka heshima mbele
..
Kwa miaka zaidi ya 12 akiwa rais wa Zazibar na makamu wa rais kaifanyia kitu gani Zanzibar na bara kiasi kwamba leo hii akumbukwe!..Binafsi namkumbuka kuwa serikali yake ndiyo aliyewahukumu KIFO kina Abdulrahman Babu na wenzake 32 kwa tuhuma za kumuua Karume..Kama sii Nyerere Jumbe angewaondoa na wapo waliouawa pindi waliporudi au kurudishwa Zanzibar..

Bila shaka kuunganishwa kwa TANU na ASP ni wazo liliotangulia akiwa rais wa Zanzibar na hata kama angeweza kuwa mtu mwingine yeyote ktk nafasi hiyo bado ASP na TANU zingeungana kwa sababu wazo hili lilitokana na Upinzani wa kisiasa ndani ya Zanzibar kuliko huku bara..Bara hatukuwa na sababu ya kuundwa kwa CCM isipokuwa kwa manufaa ya Zanzibar kwani watu kama Seif Sharrif Hamad pia became member of CCM na hilo baraza la Waporaji. Kwanza hao CCM wametupeleka wapi zaidi ya kuwa masikini zaidi..Upuuzi mtupu.

Mkuu wangu kama kuna HERO Zanzibar basi mimi nasema mjamaa mwenzangu Abdoulrahman Babu ndiye anastahiri kwani bila yeye huo Muungano wa nchi na vyama usingekuwepo..Hawa wote wamedandia Mapinduzi ya haki na yaliyokuwa kwa manufaa ya Wazanzibar..
Soma kidogo historia ya Babu hapa
 
- Wakuu labda kwanza muweke CV ya Mzee Jumbe, je alikuwa na qualifications za kutosha kuwa waziri katika ofisi ya Rais wa Zanzibar? Na hatimaye kuwa rais wa Zanzibar?

- Kama hakuwa na qualifications za kutosha, ina maana alipewa pewa sasa hawa waliompa walikuwa wanategemea nini in return kutoka kwake? Je ni nani waliomfikisha juu kwa njia za mkato?

- Kama kweli alikua nazo qualifications basi kweli alionewa, ninasema hivi kwa sababu kuna theories nyingi sana kuhusu kufika kwake juu, kwamba alifikishwa huko juu makusudi ili kuhitimisha muungano wa Tanu na ASP.

Ahsanteni.

William.
 
1. In 1979, Jumbe made history by launching the first democratic institution, the House of Representatives but members were mainly appointed instead of being elected by the people at large.

2. He also opened up his administration for people, who could otherwise have been kept out if the strict revolutionary principles were followed.

3. This move, which he later seemed to regret, was the source of his downfall.

4. He was at odds with, the so called, the committe of fourteen who included most of the people who participated in the revolution. Their influence began to decline and their powers, at times, questioned.

5. In an attempt to remedy the damage he droped most of these new elements in his government and made a radical move of attempting to back down from his support towards one central government for the whole of Tanzania.

6. In 1984, he was forced to resign by the CCM's central committe and Ali Hassan Mwinyi was appointed the new President of Zanzibar.
 
BABYLON,


Mkuu wangu unalia na Aboud Jumbe kwani yeye mama yako?..unalia kwa kipi haswa wakati huyu mtu ni wa kuchora yaani hakuwa na nafasi yoyote zaidi ya kuwa replacement ya Marehemu Karume..

Waniita KIUMBE... duh ama kweli umenichoka... sema kabisa Bangubangu maanake ndio zenu nyie kuchovya.. Na utaniita majina yote lakini jua moja nazungumza lugha ya KIUME toka sauti bara sibani sauti wala kuashiria kwa kwa vidole..
Hivyo kuwa msikivu na weka heshima mbele
..
Kwa miaka zaidi ya 12 akiwa rais wa Zazibar na makamu wa rais kaifanyia kitu gani Zanzibar na bara kiasi kwamba leo hii akumbukwe!..Binafsi namkumbuka kuwa serikali yake ndiyo aliyewahukumu KIFO kina Abdulrahman Babu na wenzake 32 kwa tuhuma za kumuua Karume..Kama sii Nyerere Jumbe angewaondoa na wapo waliouawa pindi waliporudi au kurudishwa Zanzibar..

Bila shaka kuunganishwa kwa TANU na ASP ni wazo liliotangulia akiwa rais wa Zanzibar na hata kama angeweza kuwa mtu mwingine yeyote ktk nafasi hiyo bado ASP na TANU zingeungana kwa sababu wazo hili lilitokana na Upinzani wa kisiasa ndani ya Zanzibar kuliko huku bara..Bara hatukuwa na sababu ya kuundwa kwa CCM isipokuwa kwa manufaa ya Zanzibar kwani watu kama Seif Sharrif Hamad pia became member of CCM na hilo baraza la Waporaji. Kwanza hao CCM wametupeleka wapi zaidi ya kuwa masikini zaidi..Upuuzi mtupu.

Mkuu wangu kama kuna HERO Zanzibar basi mimi nasema mjamaa mwenzangu Abdoulrahman Babu ndiye anastahiri kwani bila yeye huo Muungano wa nchi na vyama usingekuwepo..Hawa wote wamedandia Mapinduzi ya haki na yaliyokuwa kwa manufaa ya Wazanzibar..
Soma kidogo historia ya Babu hapa



Kwetu sisi hapa zanzibar tunasema kuwa sisi i viumbe vyake Mmungu ,au mtu kukwambia wewe ni kiumbe yaani umeumbwa hilo sio tusi kutookea hizo karne mpaka hii leo. Haijatokea neno hili kuwa matusi lakini inaonesha kwa upande wako ni matusi, pia inawezekana waliokufunza kiswahili nao walikuwa na upungufu wa maneno ya undani na maana yake kama nilivyokwisha sema hapo mwanzo inawezekana kwa bahati mbaya tu ikawa baadhi kiswahili sio chimbuko loko kila la kheri (NDUGU)
 
BABYLON,


Mkuu wangu unalia na Aboud Jumbe kwani yeye mama yako?..unalia kwa kipi haswa wakati huyu mtu ni wa kuchora yaani hakuwa na nafasi yoyote zaidi ya kuwa replacement ya Marehemu Karume..

Waniita KIUMBE... duh ama kweli umenichoka... sema kabisa Bangubangu maanake ndio zenu nyie kuchovya.. Na utaniita majina yote lakini jua moja nazungumza lugha ya KIUME toka sauti bara sibani sauti wala kuashiria kwa kwa vidole..
Hivyo kuwa msikivu na weka heshima mbele
..
Kwa miaka zaidi ya 12 akiwa rais wa Zazibar na makamu wa rais kaifanyia kitu gani Zanzibar na bara kiasi kwamba leo hii akumbukwe!..Binafsi namkumbuka kuwa serikali yake ndiyo aliyewahukumu KIFO kina Abdulrahman Babu na wenzake 32 kwa tuhuma za kumuua Karume..Kama sii Nyerere Jumbe angewaondoa na wapo waliouawa pindi waliporudi au kurudishwa Zanzibar..

Bila shaka kuunganishwa kwa TANU na ASP ni wazo liliotangulia akiwa rais wa Zanzibar na hata kama angeweza kuwa mtu mwingine yeyote ktk nafasi hiyo bado ASP na TANU zingeungana kwa sababu wazo hili lilitokana na Upinzani wa kisiasa ndani ya Zanzibar kuliko huku bara..Bara hatukuwa na sababu ya kuundwa kwa CCM isipokuwa kwa manufaa ya Zanzibar kwani watu kama Seif Sharrif Hamad pia became member of CCM na hilo baraza la Waporaji. Kwanza hao CCM wametupeleka wapi zaidi ya kuwa masikini zaidi..Upuuzi mtupu.

Mkuu wangu kama kuna HERO Zanzibar basi mimi nasema mjamaa mwenzangu Abdoulrahman Babu ndiye anastahiri kwani bila yeye huo Muungano wa nchi na vyama usingekuwepo..Hawa wote wamedandia Mapinduzi ya haki na yaliyokuwa kwa manufaa ya Wazanzibar..
Soma kidogo historia ya Babu hapa


Kama una chuki binafsi uwanja uko wazi kuzieleza. Unawezaje kuisemea Zanzibar wakati hujui chote juu yake.
Kama huku Bara Mzee ruksa alikuwa kuopowa watu kutoka kwenye njaa basi kule Zanzibar alikuwa Jumbe baada ya kuchukuwa madaraka baada ya kifo cha Karume. Ni kipindi cha Jumbe ndipo mahakama ya wazi ilifanyika kule Zanzibar. Wahaini waliendeshewa kesi kwa uwazi na kila siku ikitangazwa na kuonyeshwa kwenye TV na hukumu zilipotolewa waliohukumiwa kifo walikata rufaa na wakapunguziwa adhabu na kuwa miaka 18. La kutia maanani ni kuwa hao waliohukumiwa kifo walikiri wenyewe na kesi ya waliobaki ndio iliendelea kwa uwazi. Wacha uongo kusema kuwa Nyerere aliingilia kati kwani kama hujui huo wakati wa Nyerere kulikwishakuwa na kesi za Kubambikiziwa Uhaini mbili na hukumu za Kifo zilitolewa ingawa hazijatekelezwa.
Ni wakati wa Jumbe hii demokrasia ya kuwa na Wawakilishi aliianzisha na ni Rais pekee ukiondowa Karume mkubwa alieweka visiwa vyote viwili kwa usawa.
Kuhusu huku Bara vitu vilivyoagizwa kutoka nje kwa Zanzibarvikiishia huku Bara zikiwemo TV, sabuni na vyakula hasa wakati kabla ya vita vya wahujumu.
Mspojuwa Historia ni bora kukaa chonjo na kusoma.
 
- Wakuu labda kwanza muweke CV ya Mzee Jumbe, je alikuwa na qualifications za kutosha kuwa waziri katika ofisi ya Rais wa Zanzibar? Na hatimaye kuwa rais wa Zanzibar?

- Kama hakuwa na qualifications za kutosha, ina maana alipewa pewa sasa hawa waliompa walikuwa wanategemea nini in return kutoka kwake? Je ni nani waliomfikisha juu kwa njia za mkato?

- Kama kweli alikua nazo qualifications basi kweli alionewa, ninasema hivi kwa sababu kuna theories nyingi sana kuhusu kufika kwake juu, kwamba alifikishwa huko juu makusudi ili kuhitimisha muungano wa Tanu na ASP.

Ahsanteni.

William.

Ninachoweza kukwambia kielimu alistahili kabisa kwani kwa kipindi cha ukoloni mwafrika kusoma na kufaulu MAKERERE Uganda ilikuwa ni kiwango kilichokuwa na hadhi.
 
1. In 1979, Jumbe made history by launching the first democratic institution, the House of Representatives but members were mainly appointed instead of being elected by the people at large.

2. He also opened up his administration for people, who could otherwise have been kept out if the strict revolutionary principles were followed.

3. This move, which he later seemed to regret, was the source of his downfall.

4. He was at odds with, the so called, the committe of fourteen who included most of the people who participated in the revolution. Their influence began to decline and their powers, at times, questioned.

5. In an attempt to remedy the damage he droped most of these new elements in his government and made a radical move of attempting to back down from his support towards one central government for the whole of Tanzania.

6. In 1984, he was forced to resign by the CCM's central committe and Ali Hassan Mwinyi was appointed the new President of Zanzibar.

Guess what 'This move' implies to? It is the appointment of those were taken as opposition of revolution especially those from Pemba Island aong them Seif Sharifu.
In fact he tried to treat all islands at the same level but as it happened that those he trusted wanted more on the pretext of one island wellfare.
 
Mzee Aboud jumbe kama binadamu mwingine ana upungufu wake lakini chakushangaza leo serekali mbili hizi hawataki hata kuyazungumzia yae mazuri aliyowafanyia pande mbili hizi za Mungano .kama asingelikubali kunganisha chama cha ASP ule mwaka 1977 kusengekuwapo na CCM, leo ukiwauliza wanafunzi hawamjuwi Mzee aboud jumbe ni nani wao wanambiwa tu muanzishi wa CCM ni mwalimu nyerere, lakini ikumbukwe historia ipo siku itabainisha hili na mengine.nakumbuka kama leo siku ile ya kunganishwa ASP na TANU mzee wetu shekh Thabit Bin kombo mtumzima alitokwa na machozi machozi yale yalikuwa na maana yake .leo imefika pahala hawa watu hawataki hata kuyaeleza au kulitaja jina la mzee Aboud lakini tusijisahau kuwa hakuna aliyejiumba, hapa wanamsubiria ili waje watueleze ambayo wanataka wao tuyasikie. Mungu ampe afya nzuri mzee wetu baadhi yetu hatuto msahau kwa mazuri aliyotuletea na tupo tayari kumsamehe kwa makosa aliyofanya ambayo leo hii yanatukosesha usingizi.

Babylon, labda tujiulize: who are the founding fathers of our nations? Mfano kwa Marekani, ukiachana na George Washigton kuna wengine wengi wanaheshimiwa kwa kuanzishwa kwa taifa hilo.

Kwa upande wetu (Tanzania), napenda kujua nani wanastahili hiyo sifa ya founding fathers?
 
Kama una chuki binafsi uwanja uko wazi kuzieleza. Unawezaje kuisemea Zanzibar wakati hujui chote juu yake.
Kama huku Bara Mzee ruksa alikuwa kuopowa watu kutoka kwenye njaa basi kule Zanzibar alikuwa Jumbe baada ya kuchukuwa madaraka baada ya kifo cha Karume. Ni kipindi cha Jumbe ndipo mahakama ya wazi ilifanyika kule Zanzibar. Wahaini waliendeshewa kesi kwa uwazi na kila siku ikitangazwa na kuonyeshwa kwenye TV na hukumu zilipotolewa waliohukumiwa kifo walikata rufaa na wakapunguziwa adhabu na kuwa miaka 18. La kutia maanani ni kuwa hao waliohukumiwa kifo walikiri wenyewe na kesi ya waliobaki ndio iliendelea kwa uwazi. Wacha uongo kusema kuwa Nyerere aliingilia kati kwani kama hujui huo wakati wa Nyerere kulikwishakuwa na kesi za Kubambikiziwa Uhaini mbili na hukumu za Kifo zilitolewa ingawa hazijatekelezwa.
Ni wakati wa Jumbe hii demokrasia ya kuwa na Wawakilishi aliianzisha na ni Rais pekee ukiondowa Karume mkubwa alieweka visiwa vyote viwili kwa usawa.
Kuhusu huku Bara vitu vilivyoagizwa kutoka nje kwa Zanzibarvikiishia huku Bara zikiwemo TV, sabuni na vyakula hasa wakati kabla ya vita vya wahujumu.
Mspojuwa Historia ni bora kukaa chonjo na kusoma.
Verdict. Kwa sisi Wazanzibari Mzee Jumbe, mazuri yake ni mengi kuliko yale mabaya. Ni shujaa wetu na hatutomsahau daima. Hata kina Seif na wenzake hawatamsahau Mzee Jumbe.
 
Kama kuna binaadamu m-binafsi hapa Tanzania aliyewahi kuishi basi Nyerere anaongoza, si kuwa aliifuta historia ya mashujaa wengine waliotoa mali zao na roho zao kwa nchi hii bali aliwafanya wakaonekana maadui wa nchi hii, na kujigeuza yeye kwa kila sifa inayomstahiki na isiyomstahiki,mbali na Jumbe watu kama Bibi Titi Moh'd, Oscar Kambona,Kasela Bantu n.k waliomtengeneza na Kumpromote Nyerere enzi hizo, walifikia hata kutoa fedha na mali zao kumpeleka Nyerere U.N akawasemee kwa kuwa tu alijua kingereza, wengine walimbeba hata pale alipotaka kupinduliwa (Oscar kambona), shukurani za mtu huyu kwa watu wote hao ni kama za punda, aliwapiga mateke na kuwanyanyasa kama vile hakuwahi kuwajua seuza kupata hisani zao,Manyanyaso aliyomfanyia BB TT, kwa kisingizio cha kutaka kumpindua, yanasikitisha hata leo ukiyasoma tu, lau kama kungekuwa na vyombo vya habari siku hizo kama ilivyo sasa vikapaza sauti zao kwa madhila waliyofanyiwa "mashujaa waliosahaulika" nchi hii na "kufutwa" historia na michango yao ya ujenzi wa taifa hili na Mwalimu Nyerere kwa makusudi, hakuna mtu angelitoa chozi lake kwa kifo chake.

Kauli hii inaonyesha utumishi wa shetani wa hali ya juu kabisa! Unajua sifa moja kuu ya Shetani ni kubadili uongo kuwa ukweli na ukweli kuwa uongo. Msingi wa anachokisema mheshimiwa huyu ameuficha, lakini alitakiwa awe wazi zaidi......Kama yanakutoka haya kwa hila, utalaaniwa kwa kumtumikia Ibilisi, ila kama hujui na wewe umelishwa ukayabeba hivyo hivyo, unanafasi ya kutafakari upya jambo hilo.
 
Guess what 'This move' implies to? It is the appointment of those were taken as opposition of revolution especially those from Pemba Island aong them Seif Sharifu.
In fact he tried to treat all islands at the same level but as it happened that those he trusted wanted more on the pretext of one island wellfare.

- Mkuu eti Mzee Jumbe alisoma Makerere? Are you serious au unatania mkuu?
 
Jamani myonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Nimeishi Zanzibar kuanzia kipindi cha Mzee Karume, nimesoma huko, ninachoweza kusema ni kwamba Jumbe ameifanyia mengi Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wake. Ndiye kiongozi wa kwanza aliyeipigania demokrasia ya kweli, hawa wote kina Seif wamekuja jua kuongea kipindi cha Jumbe na walipopewa uhuru huo wakautumia kusaliti kupitia Bara.

Jumbe ndiye kiongozi aliyesimika misingi ya demokrasia visiwani, alitoa uhuru wa watu kujieleza baada ya miaka kadhaa ya vugu vugu la mapinduzi ambapo kuikosoa serikali ilikuwa ni uhaini.

Ukweli utabaki pale pale kwamba kama sio Jumbe kusingekuwa na CCM, ni kama ukweli ulivyo kwamba bila Karume kusingekuwa na muungano. Ni Karume aliyerahisisha muungano kwa kumweleza Nyerere "Wewe Rais mimi Makamu, hebu imagine angehitaji yeye kuwa Rais Julius angeridhia kirahisi!

Kila kiongozi anatimiza majukumu yake katika kipindi chake, matokeo huwa ya sura mbili, hasi na chanya.
 
KELA 72
Usiwe mshabiki wakati mambo yaliyojificha enzi hizo yakifichuliwa kwa kuwa wakati huo pengine hukuwapo(sina hakika) au yalifichwa yakawa hayazungumzwi kwa sababu zinazoeleweka pengine ndo ukawa huyajuwi. Historia itayafichua popote yalipo na wale (kama wewe) ambao wanaamini hayakutokea watayaona ya ajabu, waliyoyaficha wanasababu zao za kuvifanya vichwa vya baadhi ya watu kama ww viamini siku zote kuwa wao ni watukufu na si vinginevyo.Mfano ikisemwa kuwa wakati Nyerere alimlazimisha na kumtisha Karume ili akubali kuiunganisha Zanzibar na Tanganyika , ww hauta amini kwa kuwa umezaliwa, ukakuzwa, ukaelimishwa kuwa Nyerere ni Mwadilifu na amepungukiwa na mapungufu mengi ambayo binaadamu wakawaida anayo. sikushangaa wakati anafariki na kuzikwa, walitokea watu pengine wenye maono kama yako ww kuwa Nyerere afanywe "MWENYE HERI". na ndo maana hauta amini hata Yesu arudi kuwa mapungufu aliyokuwa nayo wakati akitawala yaliwaumiza watu na hata waliokuwa wenza wake. Kwa kukusaidia tu rejea katika ile Kesi ya uhaini ya akina bibi titi na wenzake, simulizi za sk Thabiti Kombo na hata maandishi ya Jumbe, hao watu walifanya kazi na Nyerere kwa karibu sana na wanamjua kuliko mimi na ww na hapo utajua hasa "The animal side of J.K.Nyerere" na kama utakuwa na nafasi soma maandishi ya W. E. Smith, na nyaraka (archives) za W. DOURADO. Halafu urejee katika mjadala na mtazamo huo huo uliokuwa nao kwa baba yako wa taifa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom