Kama sanaa ni sawa na kazi nyingine iweje mnafungia wanamuziki? Serikali inakosea

field marshall1

JF-Expert Member
Sep 17, 2017
1,171
2,730
Wakati viongozi waliopo madarakani walivyokuja kuomba kura wanakuja kwa unyenyekevu, heshima na ahadi nyingi zote zikiwa za kutetea wananchi wanyonge. Wakipata ukubwa wanaanza kuja na "decrees" nyingi za kuwapendelea wao wenyewe na kutoa maneno ya kujionyesha wao ndiyo wao hakuna wengine......Wamesahau walichosema wakati wa kuomba kura.

Kumekuwa na wimbi la kufungia wanamuziki na vyombo vya habari kwa "TRIVIAL reasons", mfano hivi karibuni kufungiwa kwa miziki kwa sababu ambazo zinaelezwa kuwa ni kukiuka utamaduni wa Mtanzania. Sijui utamaduni wa mtanzania upoje maana nimeulizia sikupata jibu hadi leo.
Nimesikiliza mahojiano ya Diamond Platnumz, mwanamuziki huo amejieleza vizuri sana nampa pongezi kwa kueleza mawazo yake, Viongozi wetu wapo hapo kwa ajili ya kuadhibu na si kurekebisha au kuelekeza, wanashindwa kuelewa kuwa muziki ni kazi kama kazi nyingine za ofisini hivyo unavyomfungia msanii kama ROMA unamuondolea ajira (employment) yake....je serikali itamlipia "Welfare"? Au kwa vile inafikiria hiyo ajira inahusu "entertainment" hivyo haifai kuwa ajira rasmi....sasa kama serikali inasema SANAA NI SAWA NA KAZI NYINGINE unavyomsimamisha au unamfungia kazi huyo mfanyakazi (msanii) ataishi vipi yeye na familia yake? Ndiyo maana nasema huo ni uonevu.....Kwenye kazi nyingine tunakosea hata kufanya kazi lakini hatusimamishwi, kufungiwa au kunyimwa mshahara...Kazi zote zina utaratibu mmoja!
Waziri kasema kile kituo cha radio kilichomhoji Diamond kitashughulikiwa..KWANI KOSA LA KITUO CHA RADIO HIYO NI NINI? Nikisema serikali hii inakandamiza uhuru wa habari kuna mtu atabisha?
Kuna utaratibu wa vituo vya TV au Radio kucheza muziki au kuonesha filamu zenye "rating R" kuanzia saa tatu na nusu usiku na kuendelea, hii ni systems ya nchi zote duniani. Watoto wanafanya nini kwenye TV saa nne za usiku? Kuna filamu zenye categories: Universal au PG-13 ambazo hazina tatizo kuangaliwa na watoto chini ya uangalizi wa wazazi......sasa haya mambo ya kusema sijui watoto wanafundishwa utamaduni mbovu unatoka wapi?
Kwanini tuwe kisiwa peke yetu wakati majirani zetu wanafanya yale tunayoyaona kwetu hayafai? UTAMADUNI GANI HUO WA MTANZANIA SERIKALI INAYOONGELEA? au ni jinsi ya kurasimisha ukandamizaji wa watu fulani fulani?
Kwa jinsi hii ningemshauri Diamond ahamie nchi kama Kenya au South Africa....nchi hizo au nchi zingine nyingi zinajali kazi za wasanii wake siyo kwetu ambako serikali inapigana na kila mtu...si wafanyabiashara, wafanyakazi, wasanii, viongozi wa dini, na wanasiasa wa upinzani.
Les Wanyika ilihamia, Simba Wanyika ilihamia Kenya, Super Volcano ilihamia Kenya, Patrick Balisidya alihamia Kenya na wengineo wengi, na kazi zao zilithaminiwa na kuinyanyua Kenya kimuziki, Hivyo Diamond akihamia nchi hizo ataendelea kufanya vizuri kwa sababu ana msingi mzuri na wenzetu wanajali, Tanzania ni nchi isiyo na msimamo!
 
Lakini kwa vyovyote vile hao waliofungiwa wako na shida kwa namna moja ama nyingine, jiulize kwanini ni wakina fulani ndio wamefungiwa lakini wakina fulani hawajafungiwa?
 
Ila ule wimbo wa Diamond, ambao mwanadada, anaoneka amevaa, bikini, yupo kwenye bwa la kuogelea, anatingisha makalio, alafu jamaa, anayapigapiga, Ulinitia aibu mbele ya wakwe zangu sebuleni.
 
Lakini kwa vyovyote vile hao waliofungiwa wako na shida kwa namna moja ama nyingine, jiulize kwanini ni wakina fulani ndio wamefungiwa lakini wakina fulani hawajafungiwa?
System ya hii serikali ipo zaidi kionevu, Bunge live imefungwa, siasa zinakatazwa, watu wanatekwa, wananchi wanauawa na kujeruhiwa, wananchi wanabambikizwa kesi ambazo hazieleweki, wananchi wengi (wafanyakazi wasio na vyeti halali wasio na vyeti halali wamefukuzwa lakini wengine wasio na vyeti na waliofoji bado wapo kazini), wananchi wanabomolewa nyumba zao( sikatai kama wamevunja sheria lakini wengine wamevunja sheria kama hao wanaobomolewa lakini wanaambiwa " WASIBOMOLEWE KWA SABABU WALINIPA KURA") kwanini kuwe na "double standard" kama ni haki, haki iwe kwa kila mtu. Mpaka hapo bado huamini tu kwamba kuna kitu hakipo sawa?
 
Ila ule wimbo wa Diamond, ambao mwanadada, anaoneka amevaa, bikini, yupo kwenye bwa la kuogelea, anatingisha makalio, alafu jamaa, anayapigapiga, Ulinitia aibu mbele ya wakwe zangu sebuleni.
Sasa wewe unaangaliaje video za bongo flavor ukiwa na wakwezo? Mimi kama nina watu kama hao muda wote ni kanda za dini tu au kanda nyingine yoyote niliyokwishaiona kabla.
 
Eti PhD holder anasema Diamond platnumz sio msemaji wa wasanii. Kwani yeye amezungumzia upande na wasanii kwa hasira mtu ametumia Mamilioni kuwekeza wewe unafungia tu pia huyu huyu ndio alizunguka kwenye kampeni kupitia umaarufu wake na pia Unafungia Waka waka na Hallelujah huku umeiacha If na Anaconda ya Nick minaj inaonyeshwa ngoma zetu za asili zenyewe miuno na maziwa njee.
 
System ya hii serikali ipo zaidi kionevu, Bunge live imefungwa, siasa zinakatazwa, watu wanatekwa, wananchi wanauawa na kujeruhiwa, wananchi wanabambikizwa kesi ambazo hazieleweki, wananchi wengi (wafanyakazi wasio na vyeti halali wasio na vyeti halali wamefukuzwa lakini wengine wasio na vyeti na waliofoji bado wapo kazini), wananchi wanabomolewa nyumba zao( sikatai kama wamevunja sheria lakini wengine wamevunja sheria kama hao wanaobomolewa lakini wanaambiwa " WASIBOMOLEWE KWA SABABU WALINIPA KURA") kwanini kuwe na "double standard" kama ni haki, haki iwe kwa kila mtu. Mpaka hapo bado huamini tu kwamba kuna kitu hakipo sawa?
Upo sawa mkuu, lakini ndio ujue hakutakuja tokea wakati ambao dunia nzima iwe na haki au usawa.
Hata angekua nani alie madarakani lazima angeonekana hatendi haki.

Nini tufanye sasa? Tukubali yaliopo yawe maana yapo, ukitaka yasiwepo maana yamesha kusudiwa yawepo basi uwepo wako utakua mashakani, ndio kutekwa ,kusingiziwa kesi, kufungiwa, nk nk. Acha yawepo maana ndio wakati wake ipo siku hayatakuwepo.
 
Wakati viongozi waliopo madarakani walivyokuja kuomba kura wanakuja kwa unyenyekevu, heshima na ahadi nyingi zote zikiwa za kutetea wananchi wanyonge. Wakipata ukubwa wanaanza kuja na "decrees" nyingi za kuwapendelea wao wenyewe na kutoa maneno ya kujionyesha wao ndiyo wao hakuna wengine......Wamesahau walichosema wakati wa kuomba kura.

Kumekuwa na wimbi la kufungia wanamuziki na vyombo vya habari kwa "TRIVIA reasons", mfano hivi karibuni kufungiwa kwa miziki kwa sababu ambazo zinaelezwa kuwa ni kukiuka utamaduni wa Mtanzania. Sijui utamaduni wa mtanzania upoje maana nimeulizia sikupata jibu hadi leo.
Nimesikiliza mahojiano ya Diamond Platnumz, mwanamuziki huo amejieleza vizuri sana nampa pongezi kwa kueleza mawazo yake, Viongozi wetu wapo hapo kwa ajili ya kuadhibu na si kurekebisha au kuelekeza, wanashindwa kuelewa kuwa muziki ni kazi kama kazi nyingine za ofisini hivyo unavyomfungia msanii kama ROMA unamuondolea employment yake....je serikali itamlipia Welfare? Au kwa vile inafikiria hiyo ajira inahusu entertainment hivyo haifai kuwa ajira rasmi....sasa kama serikali inasema SANAA NI SAWA NA KAZI NYINGINE unavyomsimamisha au unamfungia kazi huyo mfanyakazi (msanii) ataishi vipi yeye na familia yake? Ndiyo maana nasema huo ni uonevu.....Kwenye kazi nyingine tunakosea hata kufanya kazi lakini hatusimamishwi, kufungiwa au kunyimwa mshahara...Kazi zote zina utaratibu wake!
Waziri kasema kile kituo cha radio kilichomhoji Diamond kitashughulikiwa..KWANI KOSA LA KITUO CHA RADIO HIYO NI NINI? Nikisema serikali hii inakandamiza uhuru wa habari kuna mtu atabisha?
Kuna utaratibu wa vituo vya TV au Radio kucheza muziki au kuonesha filamu zenye "rating R" kuanzia saa tatu na nusu usiku na kuendelea, hii ni systems ya nchi zote duniani. Watoto wanafanya nini kwenye TV saa nne za usiku? Kuna filamu zenye categories: Universal au PG-13 ambazo hazina tatizo kuangaliwa na watoto chini ya uangalizi wa wazazi......sasa haya mambo ya kusema sijui watoto wanafundishwa utamaduni mbovu unatoka wapi?
Kwanini tuwe kisiwa peke yetu wakati majirani zetu wanafanya yale tunayoyaona kwetu hayafai? UTAMADUNI GANI HUO WA MTANZANIA SERIKALI INAYOONGELEA? au ni jinsi ya kurasimisha ukandamizaji wa watu fulani fulani?
Kwa jinsi hii ningemshauri Diamond ahamie nchi kama Kenya au South Africa....nchi hizo mbili zinajali kazi za wasanii wake siyo kwetu ambako serikali inapigana na kila mtu...si wafanyabiashara, wafanyakazi, wasanii, viongozi wa dini, na wanasiasa wa upinzani.
Les Wanyika iliyogawanyika ikazaa Simba Wanyika ilihamia Kenya, Super Volcano ilihamia Kenya, Patrick Balisidya alihamia Kenya na wengineo wengi na kazi zao zilithaminiwa na kuinyanyua Kenya kimuziki, Hivyo Diamond akihamia nchi hizo ataendelea kufanya vizuri kwa sababu ana msingi mzuri na wenzetu wanajali, Tanzania ni nchi isiyo na msimamo!

Sijasoma huko juu wengine wamesema nini(naamini wapo wenye mawazo kama yangu), lakini Mkuu Field Marshal1 nikiri, mimi (sijui nawe uko hivyo) au sielewi au sijui kama naona mazingaombwe, lakini naamini kuna kitu hakipo sawa kabisa na sirikali ya "Mungu". Watawala wamekuwa kama vile wemelogwa vile!!! yaani we acha tu.

Anyway umetoa somo zuri sana, tena sana.... ila bahati mbaya nakuhakikishia hili sikio sio la dawa tena.... Hahahaha... nacheka kwa uchungu sana Mkuu.
 
Wakati viongozi waliopo madarakani walivyokuja kuomba kura wanakuja kwa unyenyekevu, heshima na ahadi nyingi zote zikiwa za kutetea wananchi wanyonge. Wakipata ukubwa wanaanza kuja na "decrees" nyingi za kuwapendelea wao wenyewe na kutoa maneno ya kujionyesha wao ndiyo wao hakuna wengine......Wamesahau walichosema wakati wa kuomba kura.

Kumekuwa na wimbi la kufungia wanamuziki na vyombo vya habari kwa "TRIVIA reasons", mfano hivi karibuni kufungiwa kwa miziki kwa sababu ambazo zinaelezwa kuwa ni kukiuka utamaduni wa Mtanzania. Sijui utamaduni wa mtanzania upoje maana nimeulizia sikupata jibu hadi leo.
Nimesikiliza mahojiano ya Diamond Platnumz, mwanamuziki huo amejieleza vizuri sana nampa pongezi kwa kueleza mawazo yake, Viongozi wetu wapo hapo kwa ajili ya kuadhibu na si kurekebisha au kuelekeza, wanashindwa kuelewa kuwa muziki ni kazi kama kazi nyingine za ofisini hivyo unavyomfungia msanii kama ROMA unamuondolea employment yake....je serikali itamlipia Welfare? Au kwa vile inafikiria hiyo ajira inahusu entertainment hivyo haifai kuwa ajira rasmi....sasa kama serikali inasema SANAA NI SAWA NA KAZI NYINGINE unavyomsimamisha au unamfungia kazi huyo mfanyakazi (msanii) ataishi vipi yeye na familia yake? Ndiyo maana nasema huo ni uonevu.....Kwenye kazi nyingine tunakosea hata kufanya kazi lakini hatusimamishwi, kufungiwa au kunyimwa mshahara...Kazi zote zina utaratibu wake!
Waziri kasema kile kituo cha radio kilichomhoji Diamond kitashughulikiwa..KWANI KOSA LA KITUO CHA RADIO HIYO NI NINI? Nikisema serikali hii inakandamiza uhuru wa habari kuna mtu atabisha?
Kuna utaratibu wa vituo vya TV au Radio kucheza muziki au kuonesha filamu zenye "rating R" kuanzia saa tatu na nusu usiku na kuendelea, hii ni systems ya nchi zote duniani. Watoto wanafanya nini kwenye TV saa nne za usiku? Kuna filamu zenye categories: Universal au PG-13 ambazo hazina tatizo kuangaliwa na watoto chini ya uangalizi wa wazazi......sasa haya mambo ya kusema sijui watoto wanafundishwa utamaduni mbovu unatoka wapi?
Kwanini tuwe kisiwa peke yetu wakati majirani zetu wanafanya yale tunayoyaona kwetu hayafai? UTAMADUNI GANI HUO WA MTANZANIA SERIKALI INAYOONGELEA? au ni jinsi ya kurasimisha ukandamizaji wa watu fulani fulani?
Kwa jinsi hii ningemshauri Diamond ahamie nchi kama Kenya au South Africa....nchi hizo mbili zinajali kazi za wasanii wake siyo kwetu ambako serikali inapigana na kila mtu...si wafanyabiashara, wafanyakazi, wasanii, viongozi wa dini, na wanasiasa wa upinzani.
Les Wanyika iliyogawanyika ikazaa Simba Wanyika ilihamia Kenya, Super Volcano ilihamia Kenya, Patrick Balisidya alihamia Kenya na wengineo wengi na kazi zao zilithaminiwa na kuinyanyua Kenya kimuziki, Hivyo Diamond akihamia nchi hizo ataendelea kufanya vizuri kwa sababu ana msingi mzuri na wenzetu wanajali, Tanzania ni nchi isiyo na msimamo!
yani juliana shonza awe wazir? seriously?.
 
Sijasoma huko juu wengine wamesema nini(naamini wapo wenye mawazo kama yangu), lakini Mkuu Field Marshal1 nikiri, mimi (sijui nawe uko hivyo) au sielewi au sijui kama naona mazingaombwe, lakini naamini kuna kitu hakipo sawa kabisa na sirikali ya "Mungu". Watawala wamekuwa kama vile wemelogwa vile!!! yaani we acha tu.

Anyway umetoa somo zuri sana, tena sana.... ila bahati mbaya nakuhakikishia hili sikio sio la dawa tena.... Hahahaha... nacheka kwa uchungu sana Mkuu.
Ni kweli, Haki huinua Taifa. Ni muhimu kupigania haki kwa kupaza sauti....Tukiogopa tutaonewa zaidi, Nyerere alipigania uhuru akafungwa, the same for Kenyatta, Mandela, Martin Luther King etc. "Freedom always come with Price" Mahatma Ghandi alitumia muda wake wote wa maisha yake kupigania alichokiamini, Waingereza na nguvu zao zote wakasalimu amri, South Africa waliwakandamiza weusi lakini wamepigana wananchi kwa nguvu zote, ubaguzi umeisha na leo tunafurahia matunda ya walichokifanya. Ni nafuu ukasimama kwenye haki ukafa ukiwa umesimama kuliko kupiga magoti.....TUNAKOELEKEA SIYO.
 
Back
Top Bottom