GE2025 Kama mwana CCM sipendi Lissu kuwa gerezani

GE2025 Kama mwana CCM sipendi Lissu kuwa gerezani

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

RUKUKU BOY

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2015
Posts
1,588
Reaction score
1,858
Mimi ni kada mtiifu wa chama Cha mapinduzi. Sio muumini wa kuandika sana humu, ila napenda kutoa ya moyoni.

Sifurahishwi kabisa nchi kwenda kwenye uchaguzi uku kiongozi mkubwa wa upinzani yupo gerezani. Viongozi wangu ata mataifa rafiki wanatucheka kabisa. Hii imesababisha uchaguzi wa mwaka huu kukosa mvuto kabisa, political will ya watu imeshuka mnooo.

Ni dhahiri Mh.Samia atawashinda Kwa kishindo wapinzani wake kina Salumu na Mpina, ila for the sake of national interest nashauri yafuatayo.

1. Lissu aachiwe awe huru.

2.Ni dhahiri nchi imegawanyika, ili mh.Rais aongoze nchi iliyo moja bila kelele za ndani na nje ya nchi, baada ya uchaguzi bunge lifanye marekebisho kidogo ya katiba ,ili kuongeza nafasi za ubunge wa kuteuliwa na Raisi.

3. Samia akutane na Lissu wayajenge,najua wanachukiana,but this is for national interest.

4. Samia awape position kama 10 ,Chadema za ubunge wa kuteuliwa na Raisi.

5. For the national interest Chadema wakubali viti hivyo.

6 Tulidhiane,tupendane,tushauliane nchi yetu isonge mbele.

Mwenyekiti wangu wa chama changu cha mapinduzi, nakuomba sana Mwachie Lissu.

Kidumu chama Cha mapinduzi.
 
Hata mimi sipendi awe gerezani, ila ni makosa yake ya jinai yamemfanya awe huko
 
Sio swala la mtu kupenda au kuvutiwa. Ni swala la kisheria linalotatuliwa kupitia mahakama.
 
Hata Mungu hapendi lisu kuwa gerezani kwa uongo
 
Mwanaume huyo muacheni APAMBANE.mapinduzi yana gharama zake.
 
CCM mtandao hawataki Samia akutane na Lissu - wao wanaamini waende hivi hivi uchaguzi uishe Samia arudi madarakani ili wafanikishe malengo yao.

Kuhusu umoja wa kitaifa, muafaka kabla ya uchaguzi wanaona hakuna tija kuongea na CDM.
Ila ki ukweli Taifa limegawanyika, tuna siku kama 60 kabla ya uchaguzi ila lakini ni kama watu wapo msibani - kumepoaa.
Hata wana CCM hawaoni vuguvugu la uchaguzi ( Vibe) ambalo huwapo kila nyakati hizi.
 
CCM mtandao hawataki Samia akutane na Lissu - wao wanaamini waende hivi hivi uchaguzi uishe Samia arudi madarakani ili wafanikishe malengo yao.

Kuhusu umoja wa kitaifa, muafaka kabla ya uchaguzi wanaona hakuna tija kuongea na CDM.
Ila ki ukweli Taifa limegawanyika, tuna siku kama 60 kabla ya uchaguzi ila lakini ni kama watu wapo msibani - kumepoaa.
Hata wana CCM hawaoni vuguvugu la uchaguzi ( Vibe) ambalo huwapo kila nyakati hizi.
Uchaguzi umedoda kwa kweli
 
Mimi ni kada mtiifu wa chama Cha mapinduzi. Sio muumini wa kuandika sana humu, ila napenda kutoa ya moyoni.

Sifurahishwi kabisa nchi kwenda kwenye uchaguzi uku kiongozi mkubwa wa upinzani yupo gerezani. Viongozi wangu ata mataifa rafiki wanatucheka kabisa. Hii imesababisha uchaguzi wa mwaka huu kukosa mvuto kabisa, political will ya watu imeshuka mnooo.

Ni dhahiri Mh.Samia atawashinda Kwa kishindo wapinzani wake kina Salumu na Mpina, ila for the sake of national interest nashauri yafuatayo.

1. Lissu aachiwe awe huru.

2.Ni dhahiri nchi imegawanyika, ili mh.Rais aongoze nchi iliyo moja bila kelele za ndani na nje ya nchi, baada ya uchaguzi bunge lifanye marekebisho kidogo ya katiba ,ili kuongeza nafasi za ubunge wa kuteuliwa na Raisi.

3. Samia akutane na Lissu wayajenge,najua wanachukiana,but this is for national interest.

4. Samia awape position kama 10 ,Chadema za ubunge wa kuteuliwa na Raisi.

5. For the national interest Chadema wakubali viti hivyo.

6 Tulidhiane,tupendane,tushauliane nchi yetu isonge mbele.

Mwenyekiti wangu wa chama changu cha mapinduzi, nakuomba sana Mwachie Lissu.

Kidumu chama Cha mapinduzi.


Utatekwa na wenzako ccm, shauri yako
 
Ila ki ukweli Taifa limegawanyika, tuna siku kama 60 kabla ya uchaguzi ila lakini ni kama watu wapo msibani - kumepoaa.
Hata wana CCM hawaoni vuguvugu la uchaguzi ( Vibe) ambalo huwapo kila nyakati hizi.
Wanamtandao wanasema hizo siyo shida zao. Kikubwa koti lao liko ikulu na mambo yao yanaenda
 
Kwakweli namchukia sana huyo ushungi alianza vema sana kusamehe madeni ya bodi ya mikopo na ile kumtembelea TL Nairobi kumbe mnafiki tu Yani anapenda kuicha Tanganyika iliyogawanyika halafu kwao kzmkz kuko vema Yani anatuachia Tanganyika yenye makovu ila Zanzibar iliyonawiri. Jwtz na tiss wanaangalia tu.
 
Yaani Leo hii CHADEMA ya kuchukua nchi ipewe viti 10 vya ubunge na sa100 rais kutoka Zanzibar? Upo siriaz kweli wewe
 
Back
Top Bottom