Kama milo 3 bado na kura bado

Kama milo 3 bado na kura bado

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Hata kama mwanasiasa afanye nini lakini kama hatabuni mbinu ya kuwafanya wananchi wamudu kula milo mitatu kwa siku bado kazi itakuwa kubwa sana kwake 2020.

Chakula lazima kitangulie mambo yoooote ya wananchi la sivyo usitegemee kitu. Nijuavyo mimi chakula, maji, matibabu na kodi ya nyumba haviwi nyuma ya kitu chochote, kama bado na kura bado pia
 
Unajidanganya.

Pambana, na hali yako acha udhaifu na ugoigoi.
 
U nail it

"You nailed it"
Shule ulienda kosomea ujinga!?

By the way, pambana na hali yako ya kiuchumi acha porojo na ugoigoi!

Je, ulimsikia mwanasiasa yeyote anakuahidi kuwa ukimchagua atakuletea ugali na dagaa mezani!?
 
Unajidanganya.

Pambana, na hali yako acha udhaifu na ugoigoi.
Hapo mkuu umetugeuka wapiga kura wako. Ulipotuomba kura hukutuambia hayo unayoyasema sasa ya kupambana sijui nini. Ulisema maisha yatakuwa mazuri sana na tutatoa misaada hata kwa nchi nyingine ndio maana nikapiga kura.
 
Hata kama mwanasiasa afanye nini lakini kama hatabuni mbinu ya kuwafanya wananchi wamudu kula milo mitatu kwa siku bado kazi itakuwa kubwa sana kwake 2020. Chakula lazima kitangulie mambo yoooote ya wananchi la sivyo usitegemee kitu
Hahahahaaa! Mkuu, pamoja na kununua "mandege, matreni, kujenga mabarabara na madaraja yake, kuondoa mahewa kazini, kutumbua majipu na hangine na hangine"! Bado tu unararamika?
 
"You nailed it"
Shule ulienda kosomea ujinga!?

By the way, pambana na hali yako ya kiuchumi acha porojo na ugoigoi!

Je, ulimsikia mwanasiasa yeyote anakuahidi kuwa ukimchagua atakuletea ugali na dagaa mezani!?
Hizi kauli hutolewa na viongozi baada ya kuchaguliwa ila wakashindwa kufanya majukumu yao. Sasa hiv mmekuja na kamsemo ka kupambana na hali yako. Sasa 2020 na wao wapambane na hali yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi kauli hutolewa na viongozi baada ya kuchaguliwa ila wakashindwa kufanya majukumu yao. Sasa hiv mmekuja na kamsemo ka kupambana na hali yako. Sasa 2020 na wao wapambane na hali yao.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hakuna serikali ama kiongozi atakayekuletea hela kwenye wallet ukiwa umekaa. Au chakula mezani.

Pambana na hali yako acha porojo.
 
Hapo mkuu umetugeuka wapiga kura wako. Ulipotuomba kura hukutuambia hayo unayoyasema sasa ya kupambana sijui nini. Ulisema maisha yatakuwa mazuri sana na tutatoa misaada hata kwa nchi nyingine ndio maana nikapiga kura.


Haaaaaa haaaaaa haa teeeh teeeh. Pole sana , mkuu
 
Hahahahaaa! Mkuu, pamoja na kununua "mandege, matreni, kujenga mabarabara na madaraja yake, kuondoa mahewa kazini, kutumbua majipu na hangine na hangine"! Bado tu unararamika?
Njaa haijui sheria wala haki. Fanya yoooote lakini njaa kiboko chao. Njaa inaweza kumfanya mtu ayang'oe mataruma ya reli, matairi ya bombadieee, vyuma vya madaraja na minara ya simu akauze kama chuma chakavu akanunue ugali maharagwe.
 
Hizi kauli hutolewa na viongozi baada ya kuchaguliwa ila wakashindwa kufanya majukumu yao. Sasa hiv mmekuja na kamsemo ka kupambana na hali yako. Sasa 2020 na wao wapambane na hali yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Waseme na kufanya yoote kwa wananchi wao lakini 2020 itakuwa zama ya wananchi nao kusema na kufanya yoote kwa wanasiasa wao watakaokatiza mbele yao. Nijuavyo mimi chakula, maji, matibabu na kodi ya nyumba haviwi nyuma ya kitu chochote, kama bado na kura bado pia
 
Kuna watu inawezekana hamjui hata majukumu yenu kama binaadam.

Eti mtu akuwezeshe kula milo mitatu,sijui ni kwa namna gani??

Kama uongozi ni sababu ya umasikini wa mtu mmoja mmoja basi wote tungekuwa na hali moja kiuchumi,embu jitafakari kama unalingana na jirani yako hapo.
 
Kuna watu inawezekana hamjui hata majukumu yenu kama binaadam.

Eti mtu akuwezeshe kula milo mitatu,sijui ni kwa namna gani??

Kama uongozi ni sababu ya umasikini wa mtu mmoja mmoja basi wote tungekuwa na hali moja kiuchumi,embu jitafakari kama unalingana na jirani yako hapo.
Jirani yangu wa upande wa Mashariki ni fisadi na anakwepa kodi sifanani nae kabisa lakini jirani yangu upande ya Kaskazini ni fundi ujenzi analalamika kuwa kazi hakuna siku hizi, watu hawajengi siku hizi, jirani yangu wa upande wa Kusini ni Mwalimu, analalamika kodi ya nyumba imekwisha anadai malimbikizo ya kupandishwa madaraja kazini kwake yule wa upande wa Magharibu ana mtoto wake amemaliza chuo cha udaktari mwaka 2015 hajapata ajira. Hivyo mimi na majirani zangu hatufanani kila mmoja analalamikia kitu fulani.
 
Jirani yangu wa upande wa Mashariki ni fisadi na anakwepa kodi sifanani nae kabisa lakini jirani yangu upande ya Kaskazini ni fundi ujenzi analalamika kuwa kazi hakuna siku hizi, watu hawajengi siku hizi, jirani yangu wa upande wa Kusini ni Mwalimu, analalamika kodi ya nyumba imekwisha anadai malimbikizo ya kupandishwa madaraja kazini kwake yule wa upande wa Magharibu ana mtoto wake amemaliza chuo cha udaktari mwaka 2015 hajapata ajira. Hivyo mimi na majirani zangu hatufanani kila mmoja analalamikia kitu fulani.

Kazi inayoitwa ufisadi siijui,Ila kodi hata wewe ni mkwepaji mzuri tu.

Inawezekana kabisa hata mchonga jeneza naye anamlaumu rais wa awamu ya tano,kwamba biashara hamna.

Malalamiko hayajawahi kumuacha binaadamu.
 
Back
Top Bottom