Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
Great thinkers, nimechoshwa na hizi tabia za polisi kujichukulia sheria mikononi kama hatuna mahakama. Imekuwa ni kitu cha kawaida kusikia jambazi sugu limeuawa na polisi au polisi wameua wamajambazi. Sisi raia tumebaki kushangilia. Ikumbukwe kuwa hata kuua mtu kuna taratibu zake...na hizo taratibu zinasimamiwa na mahakama. Na raia anaposhangilia kuuawa kwa raia mwingine naye pia anashiriki yale mauaji.
Sababu kuu ya polisi kuua raia (wanaoitwa majambazi) ni kuthibitisha kuwa katika nchi hii ya Tanzania hakuana utwala wa sheria. Moja ya wajibu wa serikali ni kulinda raia wake. Wananchi, tunatakiwa tuungane kupinga dhuluma zoooote za jeshi la polisi hasa hili la kuua raia kila kukicha. Polisi anayeua, anatakiwa afunguliwe mashitaka.
Kuna matukio mengi yanayojitokeza kila mara na kuripotiwa kwenye vyombo vya habari ambayo yanathibitisha tabia hii mbaya.
Naomba kuwakilisha
Sababu kuu ya polisi kuua raia (wanaoitwa majambazi) ni kuthibitisha kuwa katika nchi hii ya Tanzania hakuana utwala wa sheria. Moja ya wajibu wa serikali ni kulinda raia wake. Wananchi, tunatakiwa tuungane kupinga dhuluma zoooote za jeshi la polisi hasa hili la kuua raia kila kukicha. Polisi anayeua, anatakiwa afunguliwe mashitaka.
Kuna matukio mengi yanayojitokeza kila mara na kuripotiwa kwenye vyombo vya habari ambayo yanathibitisha tabia hii mbaya.
Naomba kuwakilisha