Muuza Kangala
JF-Expert Member
- Jul 21, 2021
- 1,126
- 4,168
Kamishna Hamad alitaja sababu tatu za kutokukubaliana na tendo hilo ndani ya polisi; kinyume cha sheria, maadili na linalomwondolea ukakamavu askari.
Kutokana na mkasa huo, Kamishna Hamad aliyeonekana kukereka nalo, aliiambia Nipashe kwamba ofisi yake ina mpango maalum wa kuwasaka askari wake wote wenye hulka na kujihusisha na matendo ya aina hiyo.
"Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kadhia hiyo ikiwamo kufanyiwa kipimo askari huyo ili kujiridhisha kama kweli anafanya kitendo hicho... ingawa tumeona video katika mitandao ya kijamii lakini hatuwezi kusema moja kwa moja kama ni kweli au sio kweli," alifafanua.
Alisisitiza kwamba, kanuni na mwenendo wa kisheria za jeshi hilo haziruhusu mapenzi ya jinsia moja, na madai hayo yakithibitika, atafikishwa kwenye mahakama ya kijeshi na hatua nyinginezo.
Kamishna Hamad alisema askari anapokuwa shoga, hukosa uaminifu na ukakamavu katika jukumu lake la msingi la kulinda raia na mali zao.
"Hatufai na atashindwa kufanya kazi za polisi, na hata heshima kwa jamii haitakuwapo. Kama unamtuma askari polisi wa aina hii akamkamate mhalifu, akifika huko anaweza hata akaguswa (...). Sasa heshima iko wapi kwa Jeshi la Polisi?" alilalamika katika kauli ya kukereka.
Aliendelea: "Huu si utamaduni wa Jeshi la Polisi na wala hakutumwa hivyo. Matendo ya mtu binafsi lazima yatafautishwe na taasisi.
"Hata hizo picha zinazosambaa hazionyeshi kuwa amevaa sare za polisi au kufanya kitendo hicho kwenye kituo cha polisi, hivyo isitafsiriwe kuwa Jeshi la Polisi ndio limefanya."
Akizungumzia mikakati ya jeshi hilo katika kukomesha ushoga ndani ya Polisi Zanzibar, Kamishna Hamad aliwataka askari wote wenye mwenendo wa aina hiyo, wajisalimishe kwenye uongozi ili warekebishwe waendane na utamaduni wa jeshi hilo.
"Lengo sio kuwafukuza kazi, bali ni kuwarekebisha, kwa sababu huwezi kujua anafanya vitendo hivyo kwa sababu gani. Inawezekana alishafanyiwa kitendo hicho tokea utotoni na hawezi kujitetea na anaendelea kujizuru," alifafanua.
Kuhusu namna ya kuwatambua wenye tabia hiyo, alisema taratibu za polisi wakati wa kuajiri hazihusishi utambuzi wa tabia za ushoga kwa mwajiriwa bali hupimwa afya zao kwa ujumla.
Pia alisema Jeshi la Polisi lina taratibu na sheria zake ambazo zimeainisha makosa yote ambayo askari wa jeshi hilo hapaswi kufanya pamoja na hukumu zake endapo atafanya makosa hayo.
"Humu ndani ya kitabu hiki (sheria za polisi) kuna utaratibu mzima wa jeshi umewekwa. Kwa hivyo, askari anayefanya makosa ambayo yameainishwa humu ikiwamo hayo ya kufanya mapenzi ya jinsia moja, kuna mahakama za kijeshi na hukumu zimewekwa," alisema
Chanzo: Nipashe
---
Kwa jinsi alivyoifedhehesha Jamhuri leo asubuhi mlitakiwa mtupe ukweli
Pia soma
- Video chafu ya askari wa kiume akiingiliwa inaleta picha gani?
Kutokana na mkasa huo, Kamishna Hamad aliyeonekana kukereka nalo, aliiambia Nipashe kwamba ofisi yake ina mpango maalum wa kuwasaka askari wake wote wenye hulka na kujihusisha na matendo ya aina hiyo.
"Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kadhia hiyo ikiwamo kufanyiwa kipimo askari huyo ili kujiridhisha kama kweli anafanya kitendo hicho... ingawa tumeona video katika mitandao ya kijamii lakini hatuwezi kusema moja kwa moja kama ni kweli au sio kweli," alifafanua.
Alisisitiza kwamba, kanuni na mwenendo wa kisheria za jeshi hilo haziruhusu mapenzi ya jinsia moja, na madai hayo yakithibitika, atafikishwa kwenye mahakama ya kijeshi na hatua nyinginezo.
Kamishna Hamad alisema askari anapokuwa shoga, hukosa uaminifu na ukakamavu katika jukumu lake la msingi la kulinda raia na mali zao.
"Hatufai na atashindwa kufanya kazi za polisi, na hata heshima kwa jamii haitakuwapo. Kama unamtuma askari polisi wa aina hii akamkamate mhalifu, akifika huko anaweza hata akaguswa (...). Sasa heshima iko wapi kwa Jeshi la Polisi?" alilalamika katika kauli ya kukereka.
Aliendelea: "Huu si utamaduni wa Jeshi la Polisi na wala hakutumwa hivyo. Matendo ya mtu binafsi lazima yatafautishwe na taasisi.
"Hata hizo picha zinazosambaa hazionyeshi kuwa amevaa sare za polisi au kufanya kitendo hicho kwenye kituo cha polisi, hivyo isitafsiriwe kuwa Jeshi la Polisi ndio limefanya."
Akizungumzia mikakati ya jeshi hilo katika kukomesha ushoga ndani ya Polisi Zanzibar, Kamishna Hamad aliwataka askari wote wenye mwenendo wa aina hiyo, wajisalimishe kwenye uongozi ili warekebishwe waendane na utamaduni wa jeshi hilo.
"Lengo sio kuwafukuza kazi, bali ni kuwarekebisha, kwa sababu huwezi kujua anafanya vitendo hivyo kwa sababu gani. Inawezekana alishafanyiwa kitendo hicho tokea utotoni na hawezi kujitetea na anaendelea kujizuru," alifafanua.
Kuhusu namna ya kuwatambua wenye tabia hiyo, alisema taratibu za polisi wakati wa kuajiri hazihusishi utambuzi wa tabia za ushoga kwa mwajiriwa bali hupimwa afya zao kwa ujumla.
Pia alisema Jeshi la Polisi lina taratibu na sheria zake ambazo zimeainisha makosa yote ambayo askari wa jeshi hilo hapaswi kufanya pamoja na hukumu zake endapo atafanya makosa hayo.
"Humu ndani ya kitabu hiki (sheria za polisi) kuna utaratibu mzima wa jeshi umewekwa. Kwa hivyo, askari anayefanya makosa ambayo yameainishwa humu ikiwamo hayo ya kufanya mapenzi ya jinsia moja, kuna mahakama za kijeshi na hukumu zimewekwa," alisema
Chanzo: Nipashe
---
Kwa jinsi alivyoifedhehesha Jamhuri leo asubuhi mlitakiwa mtupe ukweli
Pia soma
- Video chafu ya askari wa kiume akiingiliwa inaleta picha gani?