Kama hupendi kelele usioe

Kama hupendi kelele usioe

Kama kuwakosha tu umejua kuwakosha leo.

Mi mwenyewe nina kelele tena hata sio kidogo kwanza kuvumilia jambo likinikera kwa umri huu hata siwezi labda nikiwa mzee huko.
Ndio nyinyi wale mkiona mume yupo kimya bhasi mnatafuta kisa au jambo lolote tu ili ujue hisia zake zimekaa vipi🤣
Mnakuwa kama wanawake wakikurya wasipopigwa na wanaume zao wanajua mapenzi yamekwisha.
 
Kama kuwakosha tu umejua kuwakosha leo.

Mi mwenyewe nikikerwa nina kelele aisee tena hata sio kidogo kwanza kuvumilia jambo kwa umri huu hata siwezi labda nikiwa mzee huko.

Shogaangu, usijibanebane. Presha na ndugu zake huwapata wanaotaka kuishi nje ya uhalisia.

Ukikerwa zungumza kisha achana nalo.
 
Hasa hasa pale mnapo amka kuandaa watoto asubuhi waende shule mnapiga kelele sana mpaka mnasababisha hatusubiri chai zenu kukimbia kelele

Na usipoangalia tunakuchanganya wewe na wanao. Mimi namwambia mtoto avae viatu, anakuja kwako unaanza kucheza nae unamuweka kichwa chini miguu juu mnachekacheka.

Naachaje kufoka?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom