Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 34,080
- 79,467
KAMA HUJAWAHI, BADO HUJUI
Na, Robert Heriel
Kama hujawahi kusalitiwa bado huyajui mapenzi
Kama hujawahi kupigana bado huijui vita
Kama hujawahi kufanya dhambi kubwa bado huujui msamaha.
Kama hujawahi kupenda bado huujui wivu
Kama hujawahi kuwa masikini bado hujui kudhalilika
Kama hujawahi kudhulumiwa bado huijui haki
Kama hujawahi kufiwa na umpendaye bado hukijui kifo
Kama hujawahi pata ajali bado hujawa dereva
Kama hujawahi kufeli bado huyajui mashindano
Kama hujawahi kuchepuka bado huujui uongo
Kama hujawahi kufungwa bado huujui Uhuru
Kama hujawahi kupata shida bado huujui upweke.
Kama hujawahi kuota ukilala bado huujui Usingizi
Kama hujawahi kutoa sadaka bado hujui ibada
Kama hujawahi kutoa msaada bado huyajui mafanikio
Kama hujawahi kutunza bado hujui kupenda
Kama hujawahi kuishi na mwanamke bado huujui uanaume wako
Kama hujawahi kuishi na mwanaume bado huujui uanamke wako
Kama hujawahi kutapeliwa bado hujui uaminifu
Kama hujawahi kusoma bado hujui maarifa
Kama hujawahi kuwa uchi basi huujui uchi wenyewe
Kama hujawahi kuwa kiongozi bado huijui lawama
Kama hujawahi kufeli mtihani bado hujui kujifunza
Kama hujawahi kusafiri bado hujui kuishi, hujui maisha
Kama hujawahi kuheshimu wazazi wako bado hujui kuheshimiwa
Kama hujawahi kukopwa pesa na mtu bado hujui namna ya kumuomba Mungu
Kama hujawahi kumtii mume wako bado hujui kupendwa na mumeo
Kama hujawahi kumpenda mkeo bado hujui/hujawahi kuheshimiwa naye
Kama hujawahi kuchimba shimo bado hujui kutumbukia
Kama hujawahi kupanda juu bado hupajui chini
Na kama hujawahi kushuka chini bado hupajui juu
Kama hujawahi kulogwa bado huujui uchawi
Kama hujawahi kufanyiwa muujiza bado humjui Mungu
Ukiona mambo yako yanakuendea tuu pasipo shida yoyote
Ukiona kila mtu anakusaidia hata kama hujamuomba
Ukiona kila mtu anakupenda na kukujali
Ukiona kila mtu anakuhurumia na kubeba matatizo yako kama yake.
Ukiona mambo yote hayo jua umekufa. Hiyo ndio maana halisi ya Kifo.
Lakini ukiona unapata hekaheka, unapanda na kushuka, husaidiwi hata unapohitaji msaada, unapendwa kwa sababu, hauonewi huruma basi jua kuwa bado unaishi. Hiyo ndio maana halisi ya kuishi.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Na, Robert Heriel
Kama hujawahi kusalitiwa bado huyajui mapenzi
Kama hujawahi kupigana bado huijui vita
Kama hujawahi kufanya dhambi kubwa bado huujui msamaha.
Kama hujawahi kupenda bado huujui wivu
Kama hujawahi kuwa masikini bado hujui kudhalilika
Kama hujawahi kudhulumiwa bado huijui haki
Kama hujawahi kufiwa na umpendaye bado hukijui kifo
Kama hujawahi pata ajali bado hujawa dereva
Kama hujawahi kufeli bado huyajui mashindano
Kama hujawahi kuchepuka bado huujui uongo
Kama hujawahi kufungwa bado huujui Uhuru
Kama hujawahi kupata shida bado huujui upweke.
Kama hujawahi kuota ukilala bado huujui Usingizi
Kama hujawahi kutoa sadaka bado hujui ibada
Kama hujawahi kutoa msaada bado huyajui mafanikio
Kama hujawahi kutunza bado hujui kupenda
Kama hujawahi kuishi na mwanamke bado huujui uanaume wako
Kama hujawahi kuishi na mwanaume bado huujui uanamke wako
Kama hujawahi kutapeliwa bado hujui uaminifu
Kama hujawahi kusoma bado hujui maarifa
Kama hujawahi kuwa uchi basi huujui uchi wenyewe
Kama hujawahi kuwa kiongozi bado huijui lawama
Kama hujawahi kufeli mtihani bado hujui kujifunza
Kama hujawahi kusafiri bado hujui kuishi, hujui maisha
Kama hujawahi kuheshimu wazazi wako bado hujui kuheshimiwa
Kama hujawahi kukopwa pesa na mtu bado hujui namna ya kumuomba Mungu
Kama hujawahi kumtii mume wako bado hujui kupendwa na mumeo
Kama hujawahi kumpenda mkeo bado hujui/hujawahi kuheshimiwa naye
Kama hujawahi kuchimba shimo bado hujui kutumbukia
Kama hujawahi kupanda juu bado hupajui chini
Na kama hujawahi kushuka chini bado hupajui juu
Kama hujawahi kulogwa bado huujui uchawi
Kama hujawahi kufanyiwa muujiza bado humjui Mungu
Ukiona mambo yako yanakuendea tuu pasipo shida yoyote
Ukiona kila mtu anakusaidia hata kama hujamuomba
Ukiona kila mtu anakupenda na kukujali
Ukiona kila mtu anakuhurumia na kubeba matatizo yako kama yake.
Ukiona mambo yote hayo jua umekufa. Hiyo ndio maana halisi ya Kifo.
Lakini ukiona unapata hekaheka, unapanda na kushuka, husaidiwi hata unapohitaji msaada, unapendwa kwa sababu, hauonewi huruma basi jua kuwa bado unaishi. Hiyo ndio maana halisi ya kuishi.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro