Kama dini ni utapeli, sasa watu wamuabudu Mungu Muumba kwa njia ipi?

mimiamadiwenani

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
5,411
7,016
Jumatano nzuri!

Nina tafakuri hapa. Kama dini ni utapeli, nikimaanisha Ukristo na Uislamu zote, sasa Mungu aabudiwe kwa njia gani? Ni kwamba watu wasiende makanisani? Misikitini?

Na je, dini zililetwa hasa kwa lengo lipi? Na hao waliozileta dini wanafaidikaje?
Au walifaidikaje? Je, wanaendelea kufaidika?

Unaamini Mungu wa kweli anakutaka uende kanisani au msikitini kumuabudu?

Unamuabudu Mungu kipofu au aonaye?
Babu zetu waliabudu Mungu aliyejibu... kwamba watu waliomba na mvua zilinyesha kwa WAKATI.

Watu waliomba na dawa za matatizo mbali mbali zilipatikana. Watu walipewa vipawa mbali mbali ikiwemo kuwa hodari kwenye miti ya dawa nk!

Mungu alijibu maombi ya wazee wetu. Siku hizi ukuomba unajibiwa na Mungu? Usijilishe mawazo na imaginations zako ukadanganya watu umejibiwa. Acha utaahira!

Nina kila sababu ya kusema dunia ya leo 99% ya Mungu anayeabudiwa na wengi hajibu maombi ya watu wake. Hali inapelekea watu wengi kuwa kama vichaa wa imani.

Jiulize! Kwa nini wazee wetu walijibiwa na sasa hivi WEWE na wenzako hamjibiwi???

Watu wengi wanasingizia wakati wa Mungu haujafika, pale ambapo wanaomba na hawajibiwi.

Mawasiliano ni two way basis. Unaomba, unapewa, au unaelezwa kusubiri kidogo, au unakataliwa kwa sababu a, b, c! Sasa wengi leo wanadanganya wamejibiwa kumbe si kweli.

Dalili za uongo kwenye dini ni Mungu kutojibu maombi ya watu wake. Hakuna impact chanya kwa watu, ambayo inaweza kudhihirika.

Yote haya yalianza baada ya ujio wa Ukristo kutoka kwa Wakoloni, pamoja na Uislamu.

Nafikiri ni njama za kuwatenga weusi na Miungu yao yenye nguvu SANA. Leo hii kijana kuchinja ng'ombe au mbuzi na akagawa nyama kwa wahitaji, anaona ni ushirikina.

Kuwanunulia wazee pombe wanywe wafurahi, kijana anaona ni DHAMBI, ni ushirikina.

Huwaheshimu wazee wa kwenu ila unawaheshimu wazee wa Rome na Oman.

Kijana kufanya tambiko kwa wazee wako waona ni ushirikina. Huko ndiko kwenye kuwakumbuka wazee na kwenye majibu mengi.

Usiogope kusimamia haki!

Dini zililetwa kutupumbaza, tena kwa makusudi. Uongo???

Mungu alikuwa Afrika hata kabla ya ujio wa Ukristo na Uislamu. Kutembea na mke wa mtu haikukubalika enzi za babu zetu. Kudhulumu(udhulmati) haukukubalika, uonevu, wivu, husuda, vijicho nk!

Kipi kipya dini zimeleta?

Mungu Muumba wa Afrika ni wakati sasa aanze kupewa heshima yake. Hizi dini koloni tuzitupe kule. Hazina faida.

Dini ya kweli ni kumpenda mwenzio kama nafsi yako na kuwajali yatima na wajane. Mambo haya yote yalikuwa kwetu hata kabla ya kuja kwa dini za Wakoloni.
 
Kwasababu Mungu hayupo.

Dini ni hatua ya maendeleo ya binadamu, kuna vitu binadamu alishindwa kuvielewa mfano kifo, ndo akatengeneza nadharia ya dini.

Lakini sasa tuna uwezo wa kuchanganua mambo kupitia sayansi, umuhimu wa dini unapungua taratibu....

Hakuna Mungu, iwe ni Mungu wa wazungu, Mungu wa watu weusi, hakuna!
 
Jumatano nzuri!

Nina tafakuri hapa. Kama dini ni utapeli, nikimaanisha Ukristo na Uislamu zote, sasa Mungu aabudiwe kwa njia gani? Ni kwamba watu wasiende makanisani? Misikitini?

Na je, dini zililetwa hasa kwa lengo lipi? Na hao waliozileta dini wanafaidikaje?
Au walifaidikaje? Je, wanaendelea kufaidika?

Unaamini Mungu wa kweli anakutaka uende kanisani au msikitini kumuabudu?

Unamuabudu Mungu kipofu au aonaye?
Babu zetu waliabudu Mungu aliyejibu... kwamba watu waliomba na mvua zilinyesha kwa WAKATI.

Watu waliomba na dawa za matatizo mbali mbali zilipatikana. Watu walipewa vipawa mbali mbali ikiwemo kuwa hodari kwenye miti ya dawa nk!

Mungu alijibu maombi ya wazee wetu. Siku hizi ukuomba unajibiwa na Mungu? Usijilishe mawazo na imaginations zako ukadanganya watu umejibiwa. Acha utaahira!

Nina kila sababu ya kusema dunia ya leo 99% ya Mungu anayeabudiwa na wengi hajibu maombi ya watu wake. Hali inapelekea watu wengi kuwa kama vichaa wa imani.

Jiulize! Kwa nini wazee wetu walijibiwa na sasa hivi WEWE na wenzako hamjibiwi???

Watu wengi wanasingizia wakati wa Mungu haujafika, pale ambapo wanaomba na hawajibiwi.

Mawasiliano ni two way basis. Unaomba, unapewa, au unaelezwa kusubiri kidogo, au unakataliwa kwa sababu a, b, c!

Yote haya yalianza baada ya ujio wa Ukristo kutoka kwa Wakoloni, pamoja na Uislamu.

Nafikiri ni njama za kuwatenga weusi na Miungu yao yenye nguvu SANA. Leo hii kijana kuchinja ng'ombe au mbuzi na akagawa nyama kwa wahitaji, anaona ni ushirikina.

Kuwanunulia wazee pombe wanywe wafurahi, kijana anaona ni DHAMBI, ni ushirikina.

Huwaheshimu wazee wa kwenu ila unawaheshimu wazee wa Rome na Oman.

Kijana kufanya tambiko kwa wazee wako waona ni ushirikina. Huko ndiko kwenye kuwakumbuka wazee na kwenye majibu mengi.

Usiogope kusimamia haki!

Dini zililetwa kutupumbaza, tena kwa makusudi. Uongo???

Mungu alikuwa Afrika hata kabla ya ujio wa Ukristo na Uislamu. Kutembea na mke wa mtu haikukubalika enzi za babu zetu. Kudhulumu(udhulmat) haukukubalika, uonevu, wivu, husuda, vijicho nk!

Kipi kipya dini zimeleta?

Mungu Muumba wa Afrika ni wakati sasa aanze kupewa heshima yake. Hizi dini koloni tuzitupe kule. Hazina faida.

Dini ya kweli ni kumpenda mwenzio kama nafsi yako na kuwajali yatima na wajane. Mambo haya yote yalikuwa kwetu hata kabla ya kuja kwa dini za Wakoloni.
Hivi dini ni ukristo na uislamu tu eti!?? Ndio kila nyuzi Kristo Islam Kristi Islam...
 
Dini ni utapeli kwa wasiojitambua, haiwezekani Mtu uishi kwa kutegemea miujiza ilihali Mungu alishasema "asiyefanya kazi na asile"

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
Tunategemea kwenye kufanya kazi, pia abariki kazi zako, sasa asipokusaidia hata kwenye hizo kazi, ana msaada gani kwako? Uongo wa dini unajidhihirisha hapo.
 
Kwasababu Mungu hayupo.

Dini ni hatua ya maendeleo ya binadamu, kuna vitu binadamu alishindwa kuvielewa mfano kifo, ndo akatengeneza nadharia ya dini.

Lakini sasa tuna uwezo wa kuchanganua mambo kupitia sayansi, umuhimu wa dini unapungua taratibu....

Hakuna Mungu, iwe ni Mungu wa wazungu, Mungu wa watu weusi, hakuna!
Haya bhana Chuga!
 
Naongelea Mungu wa kwenye Biblia sio wa kwenye dini kwasababu wa kwenye dini kachakachuliwa! Pia, naongelea Mungu wa wakristo ndie ninayemjua! Watu kukusanyika pamoja kwa ajili ya kumwabudu Mungu ni vema kabisa! Watu kutenda mema kudhibitisha imani yao ni vema kabisa!

Watu kujenga taasisi za kupambana na changamoto za maisha huku wakidhihirisha uwezo wa Mungu wao pia ni vema kabisa.

Sasa wanadamu wakaunganisha hayo mahudhui matatu niliyoyataja na kutengeneza utaratibu wanaouona watafaidika katika nyanja za kijamii, kisiasa, kiuchumi, kiutanaduni. n.k na kutengeneza kitu kinaitwa DINI! Mungu hakuleta dini! Mungu alileta ushirika kati yake na mwanadamu!

Shetani kaleta dini! Pakiwepo ushirika kati yako na Mungu hata kama utakuwa katika dini lakini hutapigwa (hutaibiwa na kutapeliwa fedha yako kwasababu eti unamtolea Mungu sadaka, hutatapeliwa muda wako wa kazi eti unatakiwa uwe kanisani unasali, hutatapeliwa nguvu zako kwa kuaminishwa mambo ambayo hayako kwenye biblia). Mtu anaweza kudhihirisha imani yake kwa Mungu bila hata kwenda kanisani! Mfano Daniel wa kwenye Biblia
 
Kama dini ni utapeli, nikimaanisha Ukristo na Uislamu zote, sasa Mungu aabudiwe kwa njia gani
Umeshasema dini ni utapele. Hakuna wakuabudiwa
Na je, dini zililetwa hasa kwa lengo lipi
Hapa unataku kuwa brainwashed na mawazo ya watu.. tafuta ukweli na utakuweka huru
Na hao waliozileta dini wanafaidikaje?
Au walifaidikaje
Kila kitu kipo hapo unapokiona si kasababu kipo tuuu bali kina sababu ya kuwapo hapo
 
Naongelea Mungu wa kwenye Biblia sio wa kwenye dini kwasababu wa kwenye dini kachakachuliwa! Pia, naongelea Mungu wa wakristo ndie ninayemjua! Watu kukusanyika pamoja kwa ajili ya kumwabudu Mungu ni vema kabisa! Watu kutenda mema kudhibitisha imani yao ni vema kabisa!

Watu kujenga taasisi za kupambana na changamoto za maisha huku wakidhihirisha uwezo wa Mungu wao pia ni vema kabisa.

Sasa wanadamu wakaunganisha hayo mahudhui matatu niliyoyataja na kutengeneza utaratibu wanaouona watafaidika katika nyanja za kijamii, kisiasa, kiuchumi, kiutanaduni. n.k na kutengeneza kitu kinaitwa DINI! Mungu hakuleta dini! Mungu alileta ushirika kati yake na mwanadamu!

Shetani kaleta dini! Pakiwepo ushirika kati yako na Mungu hata kama utakuwa katika dini lakini hutapigwa (hutaibiwa na kutapeliwa fedha yako kwasababu eti unamtolea Mungu sadaka, hutatapeliwa muda wako wa kazi eti unatakiwa uwe kanisani unasali, hutatapeliwa nguvu zako kwa kuaminishwa mambo ambayo hayako kwenye biblia). Mtu anaweza kudhihirisha imani yake kwa Mungu bila hata kwenda kanisani! Mfano Daniel wa kwenye Biblia
Tuambie tu tuelewe,
Haya Mungu alileta biblia,
Na shetani kaleta Dini,
Je!! Mungu aliletwa na nini na shetani aliletwa nani??

Haya mambo huwa mnayaongelea kiwepesi tu hamjui au huenda mnajua ila mnafanya makusudi, kuwa hizi dini zimetuweka kifungoni zimetuweka katika gereza kubwa mnoo ,, tumeshafungiwa halafu waliotufungia alishaondoka na ufunguo maaana alishafanikisha chake, hivi tukikaa tunasimuliana habari za akina israel na yakobo mambo ya akina Muhammed na Ismael, si vyema zaidi tungekaa kujadili mambo ya mila na desturi za mtanzania, mambo ya akina mwananalundi si heri zaidi tungekaa kuwasifia akina mkwawa,akina kinjekitile nawengineo wengi waliojitahidi angalau kuutetea uafrika? Si makosa yenu ila ninawalaumu na najlaumu kuwa katika hizi imani za akina yakobo na yesu ..

Okay ujue tu huyo mungu aliletwa na biblia na huyo shetani aliletwa na biblia,
Huo moto uliletwa quran na huyo allah aliletwa na quran
Over...
 
Back
Top Bottom