nzagambadume
JF-Expert Member
- Apr 9, 2018
- 2,430
- 5,784
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezek la mshahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.We kiboko, mpaka watu wakariri kama msahafu
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezek la mshahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.We kiboko, mpaka watu wakariri kama msahafu
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezek la mshahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.Mi nawashauri wasijaribu kabisa. Maana wasomi wasio na ajira ni wengi kuliko watumishi walioajiriwa. Shauri zao..
kila aliyemo Tanzania amekwamishwa na mtu huyu .Wewe ndiye asemwaye na maandiko haya Mkuu?
Kuna maslahi tuu... Nani anapata nini kwenye niniSiasa ya ujamaa na kujitegemea....
Kwenye siasa hakuna Mahaba, kwaherini.
AaamenOle wake ambaye ni kikwazo kwa walio wadogo.
Mtu huyu ndiye atumiaye maandiko haijawahi kutokea
Kuna maslahi tuu... Nani anapata nini kwenye nini
Bora hata yangekuepo haya ila Mimi nikafanikiwa kumalzia nyumba yangu nikaacha kuishi nyumba za kupangakama asingekuwa mtu huyu vikao vya kifisadi vingekuwa vinafanyika hadi ikulu
kama asingekuwa mtu huyu , watanzania wangekuwa kama ukoo wa kambale kila mtu ana sharubu, hakuna baba wala nani
kama asingekuwa mtu huyu , maneneo kama unajua mimi nani, yangekuwa mengi sana mtaani.
kama asingekuwa mtu huyu, SGR isingejengwa, shirika la ndege lisingefufuliwa, mikataba ya madini isingerekebishwa, wakulima wangeendelea kunyanyasika, dili zingekuwa zinapigwa hadi na ikulu kabisa, watoto wa kitanzania wasingepata elimu bure
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
kama asingekuwa huyu , tanzania ingeendelea kuwa shamba la Bibi
Hapana. Anaesemwa hapa ni MTU HUYU!
Mtu huyu hupenda kunukuu aya za Biblia zinazo mfavaour
kama asingekuwa mtu huyu vikao vya kifisadi vingekuwa vinafanyika hadi ikulu
kama asingekuwa mtu huyu , watanzania wangekuwa kama ukoo wa kambale kila mtu ana sharubu, hakuna baba wala nani
kama asingekuwa mtu huyu , maneneo kama unajua mimi nani, yangekuwa mengi sana mtaani.
kama asingekuwa mtu huyu, SGR isingejengwa, shirika la ndege lisingefufuliwa, mikataba ya madini isingerekebishwa, wakulima wangeendelea kunyanyasika, dili zingekuwa zinapigwa hadi na ikulu kabisa, watoto wa kitanzania wasingepata elimu bure
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
kama asingekuwa huyu , tanzania ingeendelea kuwa shamba la Bibi
Mpaka beberu liungurume ndioGenge la kina bashite haliwezi kukuelewa malalamiko hayo
Tatizo lenu wabongo hamueleweki nini mnachotaka....wakati wa mzee wa kutabasamu (baba riz1)mlisema hafai.... ni bora tupate dikteta ainyooshe nchi ....sasa sala zenu zimesikika mmepewa dikteta mnahara hara hovyo ..mnataka kurudi kwenye kucheka cheka tena...
Duh hapa mfalme jiwe anahusika...Habari wakuu.
Kwa miaka mitatu kama asingekuwa mtu huyu ungekuwa unakiwanja na ujenzi ungekuwa umeshaanza. Lakini si ajabu mpaka sasa huna hata dalili achilia mbali ndoto zako zilizokufa za kumiliki kiwanja hicho.
Kama asingekuwa mtu huyu muda huu ninapoandika ungekuwa upo ofisini unachapa kazi huenda umejiajiri au umeajiriwa. Lakini siajabu mpaka sasa huna ofisi hata ya kuuza karanga achilia mbali kuuza kashata za mia mia. Upo upo tuu na miaka inaenda na unaishi kama mgonjwa wa HIV.
Kama asingekuwa huyu mtu kwa miaka mitatu hii ungekuwa umepanda mshahara zaidi ya laki moja na nusu kulingana na ongezeko la mishahara kila mwaka. Lakini mpaka ninapozungumza muda huu ninauhakika mshahara wako umepungua zaidi ya laki moja na nusu na kama umejiajiri mapato yako kwa mwezi yamepungua kwa 20%.
Kama asingekuwa huyu mtu sasa hivi hapa ungekuwa umeoa au umeolewa lakini cha kushangaza hata yule mchumba uliyemfikiria utakuwa naye umeshaachana naye kwani maisha ni magumu. Mwanamke huenda usingezalia nyumbani kama asingekuwa mtu huyu kwani ungeshaolewa tena kwa harusi kubwa yenye zawadi kede kede. Usimchukie mchumba au mume wako aliyekuacha tatizo si yeye ni huyu mtu.
Kama asingekuwa huyu mtu ninapozungumza sasa hivi hapa usingefunga baadhi ya miradi yako kama si yote na pengine ungekuwa umeongeza miradi chungu mzima. Lakini mtu huyu ameua miradi yako alichobakiza ni roho yako tuu.
Huenda sasa hivi hapa ungekuwa umewajengea wazazi wako nyumba au kuifanyia marekebisho nyumba yao lakini sasa hivi unashindwa hata kuwatumia hata hela ya matumizi. Asingekuwepo mtu huyu ungestawi sana.
Asingekuwepo mtu huyu huenda sasa hivi watoto wako wangekuwa wanasomea shule nzuri ambazo ulipanga lakini amini usiamini kinachokufanya uwapeleke kwenye shule zile usizoridhishwa nazo ni huyu mtu. Na kama umempeleka imegeuka mzigo kwako na ada unatoa kwa kubembeleza na kutia huruma kwa waalimu wakuu.
Kama asingekuwa mtu huyu ninapozungumza hapa mafao yako ewe unayekaribia kustaafu ungekuwa unapewa kama yalivyo lakini picha limegeuka unapinga namna ya kuchukua haki yako.
Kama asingekuwa huyu mtu hapa, wewe usomaye Diploma ya fani fulani huenda ungekuwa unachukua shahada ya kwanza ya fani hiyo hiyo uipendayo lakini kwa vile marks zimeongezwa kimakusudi umeishia kusoma diploma. Mbaya zaidi huenda umeshindwa kusoma kabisa hata hako ka-diploma kako kisa huwezi kumudu gharama za malipo.
Kama asingekuwepo mtu huyu huenda leo hii tungekuwepo na kina Ben saanane, akina Mawazo na wengine wengi. Huenda Tundu Lisu angekuwa yupo Bungeni au jimboni akifanya yake. Huenda Akwilina angekuwa anafanya mahafali yake ya kuhitimu chuo huku ndugu zake na wapenzi wake wakifurahia. Lakini mtu huyu ndiye kasababisha mambo yote haya kutokea.
Kama asingelikuwa mtu huyu sasa hivi watu wangekuwa wanapigana vijembe majukwaani, kwenye mitandao ya kijamii bila woga wala uadui wowote na baada ya hapo hualikana wakicheka kwani lengo si uadui bali kujenga na kufanya maisha yaende. Lakini mtu huyu kafanya mambo haya kuwa ni chanzo cha matatizo ikibidi kifo.
Angalizo: mtu huyu anaweza kuwa mimi au wewe so kuwa makini kwenye Komenti.
JOKAJEUSI