Kalipie Benki

Mlenge

R I P
Oct 31, 2006
2,125
2,291
Awali ya yote naipongeza serikali kwa kuimarisha mfumo wa malipo ya kielektroniki serikalini.

Kinachokera ni pale unapoenda afisi ya serekali na kuambiwa kalipie benki: wanakulazimisha uende benki, ujaze fomu ya makaratasi na kulipia hapo benki ili upate 'slipu' ya kurudisha afisi ya serekali, ambako utakutana na urasimu mwingine kabla ya kupewa risiti.

Zama hizi za kutumia 'App' za simu ya kiganjani, au kutumia mfumo wa USSD kukamilisha malipo, utaratibu wa kulazimisha makaratasi unaonekana ni wa kizamani mno, unaofaa kubadilishwa. Afisi za umma zingeshauriwa zifungue mifumo ya kielektroniki ambayo inaongea na mifumo mingine, hususan ule wa malipo ya serikali.

Hii itapunguza kero nyingi na kuondoa urasimu usio na tija wala ulazima.
 
Mlenge hii inatokana na dhana ya kufanya jambo bila kuwa na plan

Ni pale kunapokuwepo na project bila kuanisha limitations na kuzitafutia ufumbuzi
Pili, inatokana na pressure hivyo kuathiri namna ya kufikiri na hilo ndilo linazaa hoja ya kwanza

Mfumo wa kielektoniki ni mzuri sana. Lengo ni kurahisha shughuli za malipo na kujenga uwezo wa kufuatilia malipo. Elekroniki inapunguza urasimu ambao ni sehemu ya wizi, kukokoa muda na kurahisha kazi

Wakati wa kuandaa mfumo huo hakuna aliyeuliza swali, je, malipo yanafanywaje katika taasisi
Swali hilo lingekuwa na jibu la kuwa na mfumo uliounganishwa kati ya taasisi na taasisi za fedha

Kwa kuanzia ni mfumo ghali, mbele ya safari gharama zinajilipa na kinachoendelea ni faida tu

Kinachofanyika sasa hivi ni kukwepa cash, lakini urasimu umeongezeka. Teknolojia haijatusaidia na imeongeza mzigo wa watu kutembea kwenda bank, kupoteza muda wa foleni na kurudi na makaratasi. Hili lingefanywa na mashine ndogo sana ambazo nchi za wenzetu zipo dukani tu

Moja ya vitu vinavyokwamisha miradi mingi mikubwa au ya watu binafsi ni overlook ya limitations
Mtu ananunua trekata alime shamba kubwa sana kwa matarajio ya kilimo cha kisasa
1. Hajiulizi kama spea za trekta zinapatikana na wapi atazipata
2. Hajiulizi kama trekta ni la kulimia au linaweza kupalilia na kuvuna
3. Hajiulizi kukiwa na kiangazi atapata wapi maji ya kumwagilia na kwa utaratibu gani
4. Hajiulizi, ikiwa kuna nguchiro na ngedere atakabiliana nao vipi

The fact ana trekta kubwa, mbele ya safari ni mkwamo. Ndio haya ya nchini kuwa tuna mkongo za taifa na wataalam wa IT, hatukufikiria tunaunganishaje huduma kuleta urahisi, kuondoa urasimu na kurahisha kazi. Yote hayo ni kutokana na pressure, kwamba, imeamriwa
 
Nguruvi3 , ni kweli mazoea yanaleta taabu. SMS ya malipo haikubaliki kama risiti halali. Au vema zaidi, mifumo kwa mifumo iongee. Ukishafanya malipo, hadithi iishie hapo.

Wengine wanaenda mbele zaidi kutaka ulete slipu wakati wameshaprinti stetimenti ya banki.

Mbaya zaidi, hata sekta binafsi imekuwa na changamoto hii.

"Kalipie benki, leta slipu tukupe risiti". Yaani mambo ya usumbufu unaoepukika.
 
Nguruvi3 , ni kweli mazoea yanaleta taabu. SMS ya malipo haikubaliki kama risiti halali. Au vema zaidi, mifumo kwa mifumo iongee. Ukishafanya malipo, hadithi iishie hapo.

Wengine wanaenda mbele zaidi kutaka ulete slipu wakati wameshaprinti stetimenti ya banki.

Mbaya zaidi, hata sekta binafsi imekuwa na changamoto hii.

"Kalipie benki, leta slipu tukupe risiti". Yaani mambo ya usumbufu unaoepukika.
Mlenge sidhani kama ni mazoea, ninaweza kusema ni uvivu wa kufikiri na kuvia kwa ubunifu

Jirani zetu haya mambo wameweza kuyamaliza kwasasa ni eletroniki

Viongozi wengi wametoka nje na kuona mambo yanakwendaje. Tatizo la watu wetu hawana uwezo wa ku tranform knowledge katika mazingira yetu, wanaishia shopping

Sekta binafasi ilipaswa kuongoza sijui nini kimetokea kwakweli. Kuna umuhimu wa kwenda na wakati. Nchi za wenzetu kubeba pesa na kichekesho, I mean mtu binafsi

Kinachosumbua akili, makampuni kama Wewstern union, World-remit na hata local kama za Wasomali 'Adabshil' wanaweza kufanya vitu secured, eti serikali ya Tz haiwezi

Hakuna 'seriousness' tunapeleka kila jambo kwa misuli
 
Kinachokera ni pale unapoenda afisi ya serekali na kuambiwa kalipie benki: wanakulazimisha uende benki, ujaze fomu ya makaratasi na kulipia hapo benki ili upate 'slipu' ya kurudisha afisi ya serekali, ambako utakutana na urasimu mwingine kabla ya kupewa risiti.
Sijajua ulienda ofisi ipi ya serikali( nadhani neno serikali ulimaanisha serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania), lakini kama ni ofisi inayohusiana na wizara ya ardhi, tatizo ulilosema halipo. Unaweza kufanya malipo ama kupitia benk ama simu za mkononi. Labda ungekuwa specific ni ofisi gani ulikumbana na kadhia hii, ili tuanzie hapo kujadili.
Asante kwa kusoma post yangu.
 
Mlenge sidhani kama ni mazoea, ninaweza kusema ni uvivu wa kufikiri na kuvia kwa ubunifu

....

Kinachosumbua akili, makampuni kama Wewstern union, World-remit na hata local kama za Wasomali 'Adabshil' wanaweza kufanya vitu secured, eti serikali ya Tz haiwezi

Hakuna 'seriousness' tunapeleka kila jambo kwa misuli

Pengine ni suala la maamuzi tu. Hata serikali inaweza kuweka mifumo salama -- mfano hivi sasa LUKU tunanunua kupitia mfumo wa malipo wa serikali. Taasisi nyingi za serikali zimeshajiunga na mfumo huo. Kinachokosekana ni mfumo wa kujihudumia (self-service).

Kama najua deni langu, na ofisi husika imenipa invoisi, kwa nini nisiweze kujipatia namba ya kumbukumbu ya malipo (control number) mimi mwenyewe, badala yake lazima niende kwenye ofisi fulani, na kupoteza muda na rasilmali zengine, ili tu kupatiwa namba ya kumbukumbu ya malipo?

Baadhi ya taasisi zimeanza kuwawezesha wananchi kujihudumia:

Mfano: 1. WCF https://portal.wcf.go.tz/storage/app/public/guide/WCFePG - USER MANNUAL.pdf
2. Hazina https://salaryslip.mof.go.tz/Account/Login?ReturnUrl=/
3. Wizara ya Ardhi Ardhi- Kadiria kodi ya pango la ardhi
4. TFDA TFDA Trader Portal

Japo baadhi uwezo huo wa kujihudumia ni kwa maeneo machache kwa baadhi ya mifano hio, hata hivyo ni mwanzo mzuri.

Pengine ipo haja ya kuwepo kwa ulazima fulani kwa kila taasisi ya UMMA kuupatia umma uwezo wa kujihudumia 24/7/365
 
Sijajua ulienda ofisi ipi ya serikali( nadhani neno serikali ulimaanisha serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania), lakini kama ni ofisi inayohusiana na wizara ya ardhi, tatizo ulilosema halipo. Unaweza kufanya malipo ama kupitia benk ama simu za mkononi. Labda ungekuwa specific ni ofisi gani ulikumbana na kadhia hii, ili tuanzie hapo kujadili.
Asante kwa kusoma post yangu.

Nisingependa kuitaja taasisi wala muamala husika. Wizara ya Ardhi, kwenye tozo la pango la ardhi ya ardhi, ni mfano wa kuigwa. ilikuwa ni mlolongo mrefu kwenda kulipia ardhi. Lakini sasa unaweza kujikadiria mwenyewe mtandaoni na kufanya malipo. Mwanzo mzuri kuelekea kupata huduma zingine za Wizara mtandaoni kwa mtindo huohuo wa kujihudumia. Mf. kununua (au vema zaidi, bila gharama) kupakua Ramani za aina zote; Kufanya search; kuweka Caveat emptor na huduma nyingine).

Kwenye halmashauri ndiko changamoto zaidi. Unaweza kwenda kuilipa halmashauri wakakwambia msururu mrefu wa kufuata mpaka wakwambie Kalipie Benki. Na ukilipa benki, msururu mwingine wa mpaka upewe risiti ya halmashauri. Ukipata risiti, msururu mwingine mpaka ofisi inayohusika ijiridhishe kwamba kweli umelipia. Ni vigumu kuelewa.
 
Kwenye halmashauri ndiko changamoto zaidi. Unaweza kwenda kuilipa halmashauri wakakwambia msururu mrefu wa kufuata mpaka wakwambie Kalipie Benki. Na ukilipa benki, msururu mwingine wa mpaka upewe risiti ya halmashauri. Ukipata risiti, msururu mwingine mpaka ofisi inayohusika ijiridhishe kwamba kweli umelipia. Ni vigumu kuelewa.
Kwa maneno mengine siku inaishia katika foleni badala ya shughuli za kikazi au maendeleo binafsi. Halafu watu wanalalamika foleni ya magari bila kujua upotevu wa muda wa foleni. Mkuu unajua hata 'bank' inapaswa kuwa online, kiasi kwamba unalipia bili zote au kufanya miamala bila kuondoka nyumbani, tena katik simu.Siyo kitu kigumu , ugumu ni watu wanaofikiri.

Kwa mfano, ni rahisi Bank X ikaorodhesha taasisi muhimu za shughuli za kila siku, kama shirika la umeme, maji, vyuo, wizara kama ardhi, halamshauri n.k. Mteja anapaswa kupata account number ya taasisi husika, malipo yote yanafanyika katika simu ya kiganjani. Huko ndipo walipo wenzetu na wala si rocket science , yaani ni vitu vya kawaida kabisa, vinaokoa muda na vina uhakika wa malipo

Ni kweli wizara ya ardhi wamejitahidi sana, si kwa malipo bali mfumo mzima unaonekana kufanana fanana !!

Kuunganisha mifumo kuna faida nyingi sana. Mathalani mfumo wa leseni za udereva unatisha
Hakuna mfumo, dereva anasababisha ajali hakuna kumbu kumbu zozote. Dereva anahamia kwingine hakuna anayejua historia yake. Mwisho wa siku dereva huyo analipa Bima sawa na yule mwangalifu wa miaka 30. Hakuna kumbu kumbu, akihama kila kitu kinabaki alipotoka

Hizi wanazosema National ID, zinapaswa kuwa linked na mifumo mingine. Hapo ndipo tutaweza kuwa na Credit bureau ya mtu. Bank wanaweza ku-access credit ya mtu na kumpa mkopo kutokana na credit score yake. Sasa hivi interest ni flat rate bila kujali credit score na ni ya juu kwasababu ya risk, hakuna instrument ya kufanya risk assessment

Hivi ni vitu visivyo na gharama na vinawezekana hata level ya halmashauri, tatizo watu hawafikiri kwa zama zilizopo ni bora liende bora kumekucha.

Kwa upande mwingine hatuna kizazi chenye curiosity. Hawa wanafunzi wa elimu ya juu mbona mambo kama haya yanawezekana na kujenga CV? Inawezekana , idea zipo ! njooni tujadiliane kuna opportunity za kufanyia kazi hasa ninyi vijana. Inawezekana
Tatizo la vijana kila mmoja anatengeneza app, hakuna anayefikiri namna ya ku solve simple problem kwa simple solution.

Ahsante Mlenge kwa mada hii
 
Pamoja mkuu Nguruvi3 .
Kwa maneno mengine siku inaishia katika foleni badala ya shughuli za kikazi au maendeleo binafsi. Halafu watu wanalalamika foleni ya magari bila kujua upotevu wa muda wa foleni. Mkuu unajua hata 'bank' inapaswa kuwa online, kiasi kwamba unalipia bili zote au kufanya miamala bila kuondoka nyumbani, tena katik simu.Siyo kitu kigumu , ugumu ni watu wanaofikiri.
...

Hivi ni vitu visivyo na gharama na vinawezekana hata level ya halmashauri, tatizo watu hawafikiri kwa zama zilizopo ni bora liende bora kumekucha.

Kwa upande mwingine hatuna kizazi chenye curiosity. Hawa wanafunzi wa elimu ya juu mbona mambo kama haya yanawezekana na kujenga CV? Inawezekana , idea zipo ! njooni tujadiliane kuna opportunity za kufanyia kazi hasa ninyi vijana. Inawezekana
Tatizo la vijana kila mmoja anatengeneza app, hakuna anayefikiri namna ya ku solve simple problem kwa simple solution.

Ahsante Mlenge kwa mada hii


Pamoja mkuu Nguruvi3 .

Yaani ukitaka kwenda kuilipa serikali inabidi ujipange haswa :( Mara nyingi inabidi "uue siku" kabisa kwenye mipangilio yako ndipo uweze kwenda kuilipa. Baadhi ya mifumo inayoweza kutatua hayo ipo -- lakini ni suala la maamuzi kuitumia vipi kikamilifu. Ndio maana tupo kwenye kutumia muda mwingi kufanya malipo. Katika jitihada za serikali kuimarisha mapato, eneo hili ndilo la muhimu pengine kuliko yote. Hata ukihamasisha watu kufanya malipo, siku ya kulipa ifikapo ni tafrani tupu. Mpaka unaweza kudhani taasisi unayotaka kuilipa haihitaji hela unayotaka kulipa.

Kwa sisi vijana :D shida ni mimbari ya kutolea fumbuzi za matatizo, hasa matatizo hayo yanapokuwapo kwenye baadhi ya afisi zenye mamlaka waliyokabidhiwa na Jamhuri. Ndio maana utaona apps na blogu tu :)

Nadhani serikali itakusanya malipo mara tano ya inavyokusanya sasa kwa kuboresha tu ufanisi wa kupokea malipo.

Kwa mfano, Auric Air ( Auric Air Services Ltd ) wameweka mfumo mzuri sana wa kujihudumia kufanya booking na kulipia huduma zao. Wanatumia DirectPay ( Online & Mobile Payment Services in Tanzania | DPO Group ) . Mifumo kama hii ikitumika itasaidia sana kuwezesha wananchi kujihudumia. Itapunguza wage-bill kwa serikali, kuongeza ufanisi na kuleta tija kwa taifa.
 
Mlenge
Kuhusu vijana, kuna tatizo kidogo la ku-navigate au ku-infiltrate into the system

Siku zote serikali hasa za nchi masikini ni bureaucracy tu inayoendelea.

Kijana atengeneze mfumo utakaotumika na private sectors au individuals, pressure italazima urasimu ubadilike. Zamani cellphone haikuwa katika malipo ya serikali, pressure imeruhusu mfumo huo

Kuhusu malipo kwa mabunda ya pesa a risti za benki, pamoja na kupoteza muda mwingi sana kwa jambo la dakika 10 kuna hasara nyingi sana zinazopatikana.

Mfano, ni rahisi sana kujua senti imeingia wapi na imetokaje ukiwa na mfumo wa elektroniki

Kijana wa kizungu alikuwa anaiba senti 5 ya dola kutoka account za wateja kwa njia elektroni, kwamba kila saa 6 usiku account zinaingiza pesa kwake.

Wateja hawakujua kwasababu senti 5 ilionekana kama charges za benki. Walifuatilia account baada ya kuona imeona hakikuchukua saa, walimbaini. Ndivyo wanavyoweza kubaini monye laundering etc

Kwa sisi Tanzania tumerudi nyuma sana. Kwa wale wa miaka iliyokwenda lol, zamani malipo yalifanywa kwa money order. Unakwenda posta yoyote unalipa unafikisha kopi. Yaani miaka hiyo kumbuka!

Katika wakati wa teknolojia eti watu wanatumia siku nzima utafuta risiti.
Yaani ni rahisi kutibiwa kuliko kupata risiti ya malipo.

Huko bank nako teknolojia imebaki gizani. Hivi mtu anasimamaje bank kwa dakika 10?
electronic chip zinafanya nini. Bado watu wanafungua makaratasi kubaini account ya mtu!

Baada ya kutoka jasho bank unapanga foleni ya kuwasilisha risiti.

Hivi kwanini katika ubutu wetu wa kufikiri kwanini usipowepo mfumo wa copier machine lango la kuingilia, mtu anapigiwa copy na mhuri anaondoka. I mean pamoja na udwanzi/uzezeta wetu hata hilo halituwezi!

Foleni kuanzia kwa mhasibu, wakati mwingine amekwenda kula chapati na maarage, imepita mbele ya ofisi ya mkurugenzi wa fedha, naibu katibu mkuu hadi afisa tawala kwenda nganzi za chini karibu na choo cha akina baba mkabala na ofisi ya afisa maduhuli

Ukiuliza ni ya nini unaambiwa watu wanawasilisha risiti kutoka bank. Mwaka 2018!!!
 
Back
Top Bottom