Kali ya kiteto

Lekanjobe Kubinika

JF-Expert Member
Dec 6, 2006
3,020
577
Source: WAPO FM RADIO

Leo tena asubuhi katika kipindi cha PATAPATA, imetoka mpya tokea Kiteto kule Manyara. Mzee mmoja alioa na kubahatika binti mmoja na kijana wa kiume mmoja kwenye miaka 14 -17 iliyopita. Kijana kwa sasa yupo darasa la Saba. Miaka saba iliyopita mama alitwaaliwa mbele ya haki (Mungu amrehemu).

Mzee hakuoa tena, akaamua kulea tu watoto alioachiwa na marehemu. Kwa kuwa ngono haina adabu, alipomwangalia binti yake akamtazama kwa jicho la tamaa (Husda???), akataka kuanza kumkomalia amlee kiutu uzima. Binti alishituka, (sijui kama alifanikiwa angalau mara moja), akaingia mitini moja kwa moja na hajulikani alipo hata leo hii. Akamwacha kaka yake anaishi na mzee. Ili kuua nyoka anayemsumbua, baba aliamua kumpatia "tuition" ya matumizi ya TIGO kijana wake kwa kumlazimisha mpaka kilipoeleweka.

Baadaye ukawa mchezo wa kila siku. Giza likiingia mtoto akawa anaona anaingia kikaangoni kwa baba tena kama anabisha alikuwa anaonyeshwa kisu, ili akubaliane na kumruhusu baba atumie TIGO yake. Akachanika vibaya kijana yule na akawa anaenda hospitalini kutibiwa lakini asiseme chanzo cha tatizo ni nini, asije akamalizwa na baba kwani alionywa asisikie kitu kama hicho kinasemwa nje ya chumba kile.

Kijana akalazimika jioni ikikaribia akitoka shule anaenda kwa ndugu au marafiki kulala, akiulizwa hasemi kitu, kesho asubuhi anaenda kuchukuwa daftari zake nyumbani na kwenda shuleni (sijui kama shule ilikuwa inapanda). Maji yakazidi unga miaka saba ya shuruba za kila siku baada ya kujikuta sasa maumivu yanazidi maana jamaa hasubiri paalipochanika papone, anendelea tu! Akaenda kwa mjumbe na kuyaweka bayana.

Mjumbe anadai kwamba alikuwa anamwona kijana hata mwendo wake ulibadilika, akifyeka kwanja ya miguu lakini pasipo kujua sababu. Mjumbe akampeleka hospitali na walipomwangalia wakakuta ameharibiwa vibaya sana. Waganga wakamkumbuka kijana huyo. Hapohapo mjumbe akafanya mpango kumwapeleka polisi wakamsalimie yule mzee ambapo walimnasa, lakini baada ya wananchi kuwa wamepata habari mapema na kumbamiza kisawasawa kumshikisha adabu. Tunavyozungumza sasa mzee yule amelazwa hospitali na pingu mikononi, kijana wake anatunzwa na wasamaria wema akiendelea na matibabu.

Jamani!!! Mzee alinogewa na hata hakutaka tena kuoa mke, maana majipu anayatumbua kila siku na wembe wa ndani aliotengeneza mwenyewe!!!! Sijui tumwiteje huyu bwana. Hao watu wapo kibao pia anaanikwa mmoja mmoja.

Tumwombee kheri kijana asiye na kosa. Angejuwa angeingia mitini na dadake. Dada mtu hakutaka kumwadhiri baba yake, labda kwa vitisho pia, na nadhani baada ya kuitumia ama voda yake au tigo pia, asingeweza kukimbia hivi hivi tu. Inadaiwa mzee yule anatembea na visu kila anakokwenda.

Wahini jioni saa moja na robo na kusikiliza wenyewe WAPO FM marudio ya kipindi. Maneno mengine hapa yametumiwa kulainisha maelezo tu kufikisha ujumbe.​
 
inabidi kuwa na sheria kama mtu anatumia kiungo chake vibaya ni kuondoa tu, mbaya sana hii.
 
Huyu mzee hata mimi nampiga shoka kabisa nini kinyongo akitakuwa sawa. Shoka kadhaa za kichwa kwisha kazi. Watu kama hawa sijui watoka wapi kwenye jamii yetu. Inabidi kila mmoja achukue jukumu la kuwaelemisha vijana wetu maana huyu mtoto ni kutokujua nini cha kufanya na wapi pa kukimbilia angekuwa na mafunzo mazuri angeweza kutoa taarifa mapema bila woga na akapata msaada mapema.
 
babu seya wa kiteto,sheria ichukue mkondo wake! Pole kwa kijana!
 
Dah nimesikia hasira ya huyu mzee natamani kulia kabisa unamwaribia mtoto maisha namna hii jamaniiii??

Wanawake wote waliojaa mtaani unashindwa kuwaoa unamharibu kijana wako dunia kweli imekwisha kha???

Kijana pole sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom