Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,875
WARAKA WA ELIMU NA.I WA MWAKA 2022 KALENDA YA MIHULA KWA SHULE ZA AWALI MSINGI NA SEKONDARI MWAKA 2022
Tafadhali rejea kichwa cha habari.
Katika muktadha huo, Kalenda iliyoanza kutumika kuanzia tarehe 17/01/2022 itatumika kama Mwongozo wa Jumla katika utekelezaji wa Mitaala ya Elimu kwa ngazi hizo za elimu nchini.
Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule ambao ndio wasimamizi wakuu wa utekelezaji wa Kalenda ya Mitaala ya Elimu katika shule mbalimbali wanatakiwa kutekeleza mitaala kwa kuzingatia hali halisi na mazingira husika katika maeneo yao ili kuongeza tija katika ufundishaji na ujifunzaji na kuleta mafanikio ya kitaaluma nchini.
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia kwa Kamishna wa Elimu itaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau kwa nia ya kuboresha Kalenda ya utekelezaji wa Mitaala ya mwaka 2022.
Aidha, Kalenda ya Mihula ya Masomo kwa Shule za Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari kwa mwaka 2022 itakuwa kama ifuatavyo:
Tanbihi:
Siku za Masomo kwa mwaka ni 194.
Wanafunzi wote watapumzika kuanzia tarehe 29/07/2022 hadi 04/09/2022 kwa Muhula wa Kwanza ili kupisha Zoezi la Kitaifa la Sensa mwezi Agosti, 2022 na mwezi Disemba, 2022 watapumzika kwa Muhula wa Pili baada ya kufunga shule tarehe 08/12/2022.
Mashindano ya UMITASHUMTA yatafanyika tarehe 30/07/2022 hadi 08/08/2022, na UMISSETA yatafanyika tarehe 09/08/2022 hadi 19/08/2022.
Mashindano ya Michezo ya Shule za Sekondari za Afrika Mashariki (FEASSSA) yatafanyika tarehe 10/09/2022 hadi 24/09/2022.
Waraka huu unaanza kutumika tarehe 18 Februari, 2022.
Nawatakia utekelezaji mwema.
Dkt. Lyabwene M. Mtahabwa
Tafadhali rejea kichwa cha habari.
Kutokana na changamoto zilizobainika katika utekelezaji wa Kalenda ya Mitaala ya Elimu kwa Shule za Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari nchini mwaka 2022, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeona kuna umuhimu wa kufafanua na kutoa maelekezo shirikishi ili kuweza kwa pamoja kutatua changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa awali wa Kalenda husikaKatika muktadha huo, Kalenda iliyoanza kutumika kuanzia tarehe 17/01/2022 itatumika kama Mwongozo wa Jumla katika utekelezaji wa Mitaala ya Elimu kwa ngazi hizo za elimu nchini.
Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule ambao ndio wasimamizi wakuu wa utekelezaji wa Kalenda ya Mitaala ya Elimu katika shule mbalimbali wanatakiwa kutekeleza mitaala kwa kuzingatia hali halisi na mazingira husika katika maeneo yao ili kuongeza tija katika ufundishaji na ujifunzaji na kuleta mafanikio ya kitaaluma nchini.
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia kwa Kamishna wa Elimu itaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau kwa nia ya kuboresha Kalenda ya utekelezaji wa Mitaala ya mwaka 2022.
Aidha, Kalenda ya Mihula ya Masomo kwa Shule za Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari kwa mwaka 2022 itakuwa kama ifuatavyo:
|
Siku za Masomo kwa mwaka ni 194.
Wanafunzi wote watapumzika kuanzia tarehe 29/07/2022 hadi 04/09/2022 kwa Muhula wa Kwanza ili kupisha Zoezi la Kitaifa la Sensa mwezi Agosti, 2022 na mwezi Disemba, 2022 watapumzika kwa Muhula wa Pili baada ya kufunga shule tarehe 08/12/2022.
Mashindano ya UMITASHUMTA yatafanyika tarehe 30/07/2022 hadi 08/08/2022, na UMISSETA yatafanyika tarehe 09/08/2022 hadi 19/08/2022.
Mashindano ya Michezo ya Shule za Sekondari za Afrika Mashariki (FEASSSA) yatafanyika tarehe 10/09/2022 hadi 24/09/2022.
Waraka huu unaanza kutumika tarehe 18 Februari, 2022.
Nawatakia utekelezaji mwema.
Dkt. Lyabwene M. Mtahabwa