Mjanga
JF-Expert Member
- Feb 13, 2011
- 1,238
- 324
Katika Gazeti la Raia Mwema (Dec. 12-Dec. 18 2012) kuna makala "Kwa nini Zitto anafa kuwa rais 2015" mwandishi Ezekiel Kamwaga anayetambulishwa kama msomaji wa Gazeti hilo anapambanua kuwa sifa kuu ya rais anayehitajika kuitawala Tanzania kuanzia 2015 ni yule aliye "mahiri katika uandishi wa makala na machapisho mbalimbali".
Sifa nyingine ni yule anayefahamiana na viongozi maarufu (kwa mtazamo wake). Mwandishi anapambanua na kutabanaisha kuwa huyo mtu kwa hapa TZ ni Zitto pekee. Nimeshindwa kuelewa mwandishi anatumika, au ameamua kupotosha umma kwa makusudi, au aelewi anachokiandika.
Sina hakika kama sifa ya uandishi inatosha kumfanya mtu kuwa rais popote duniani, Ezekiel amesahau kwamba hata yeye ni mwandishi, na tunao wengine wengi tu wanaoandika majarida, makala, na vitabu na kushiriki midahalo mbalimbali yahusuyo mambo ya kiuchumi , kisiasa, na kijamii: kwanini yeye asifae wakati sifa hiyo anayo? kwanini wengine kama akina Dr. Rweitama, Dr. Mkumbo, watu kama Jenerali Ulimwengu na wengine wengi wasifae?? kufahamika na kuheshimiwa na viongozi ni swala la kawaida tu wapo wafanyabihashara, mishen towns na wengine wengi ambao wanafahamika na kuheshimika- sidhani kama hizi hoja zinaweza kumfanya mtu awe rais. Pengine kwa mtazamo wa Mwandishi hili linawezekana hapa TZ tu!
kimsingi waTanzania wanahitaji Rais mwenye sifa zaidi ya hizi zinazotajwa na Mwandishi. Ni kweli tunahitaji rais mwenye kujua matatizo yetu, lakini lazima pia awe na uchungu na utashi wa kuleta mabadiliko katika maisha ya waTanzania kwa ujumla, rais anayeeshimu mamlaka aliyonayo na kuitumia vizuri, rais mwenye uwezo wa kukemea mabaya na kusimamia kauli zake, rais mwenye uchungu na rasilimali za nchi. WaTanzania hawahitaji rais mbabaishaji, rais mshikaji na wenye sifa ambazo tumezichoka!
Naheshimu mawazo ya mwandishi, lakini pia waandishi wetu wasitumie kalamu zao vibaya kwa sababu tu wanafursa ya kupata majukua ya kuandikia, na tuwaogope sana waandishi ambao ni INSTRUMENTAL, wanaoweza kuchukua baadhi ya maneno katika sentensi ya mtu na kuifanya kuwa habari!
Mungu ibariki Tanzania!
Sifa nyingine ni yule anayefahamiana na viongozi maarufu (kwa mtazamo wake). Mwandishi anapambanua na kutabanaisha kuwa huyo mtu kwa hapa TZ ni Zitto pekee. Nimeshindwa kuelewa mwandishi anatumika, au ameamua kupotosha umma kwa makusudi, au aelewi anachokiandika.
Sina hakika kama sifa ya uandishi inatosha kumfanya mtu kuwa rais popote duniani, Ezekiel amesahau kwamba hata yeye ni mwandishi, na tunao wengine wengi tu wanaoandika majarida, makala, na vitabu na kushiriki midahalo mbalimbali yahusuyo mambo ya kiuchumi , kisiasa, na kijamii: kwanini yeye asifae wakati sifa hiyo anayo? kwanini wengine kama akina Dr. Rweitama, Dr. Mkumbo, watu kama Jenerali Ulimwengu na wengine wengi wasifae?? kufahamika na kuheshimiwa na viongozi ni swala la kawaida tu wapo wafanyabihashara, mishen towns na wengine wengi ambao wanafahamika na kuheshimika- sidhani kama hizi hoja zinaweza kumfanya mtu awe rais. Pengine kwa mtazamo wa Mwandishi hili linawezekana hapa TZ tu!
kimsingi waTanzania wanahitaji Rais mwenye sifa zaidi ya hizi zinazotajwa na Mwandishi. Ni kweli tunahitaji rais mwenye kujua matatizo yetu, lakini lazima pia awe na uchungu na utashi wa kuleta mabadiliko katika maisha ya waTanzania kwa ujumla, rais anayeeshimu mamlaka aliyonayo na kuitumia vizuri, rais mwenye uwezo wa kukemea mabaya na kusimamia kauli zake, rais mwenye uchungu na rasilimali za nchi. WaTanzania hawahitaji rais mbabaishaji, rais mshikaji na wenye sifa ambazo tumezichoka!
Naheshimu mawazo ya mwandishi, lakini pia waandishi wetu wasitumie kalamu zao vibaya kwa sababu tu wanafursa ya kupata majukua ya kuandikia, na tuwaogope sana waandishi ambao ni INSTRUMENTAL, wanaoweza kuchukua baadhi ya maneno katika sentensi ya mtu na kuifanya kuwa habari!
Mungu ibariki Tanzania!