Kakobe vs Vyama vya Upinzani?

Kwanza kakobe mwaka 2000 aliahidi kuaacha kuhubiri ikiwa mrema atashindwa Urais,huyu ni hero wa nani?
 
Kwanza kakobe mwaka 2000 aliahidi kuaacha kuhubiri ikiwa mrema atashindwa Urais,huyu ni hero wa nani?

Lakini kwa issue ya Tanesco Vs. Kakobe ameweza kuwaunganisha wafuasi wake kudai madai yake na wafuasi wamemfuata kisawasawa...je upinzani wanaweza kufanya hivyo kwa serikali kwa mambo ya msingi kama katiba na tume huru ya uchaguzi?

Je kuna mwananchi anayemuamini slaa , mbowe tukianzia kwenye department yake hata kitaifa ili kuleta mabadiliko?
 
Tukilinganisha kukubalika kwa viongozi wa dini na siasa tunakosea maana naamini dini mtu akiwa serious inzidi kwenye siasa, viongozi wa dini wanaweza wambia watu wao wajiue na wakajiua lakini kwenye siasa watauliza tunajiua kwanini. Mimi simwamini kakobe hata kidogo lakini namheshimu sana kwani ameshiria maisha ya waumini zaidi ya 300 ambao akiamua kuwateketeza anaweza bila kizuizi, then huyu huwezi mlinganisha na Mbowe ambaye hata akimwambia Zito wajiue kupinga tume ya uchaguzi Zito hawezi fanya.

Swala la dini halina elimu nenda kwa mwingira uone jinsi ambavyo watu wenye elimu zao wanavyopagaishwa na dini.
 
Tukilinganisha kukubalika kwa viongozi wa dini na siasa tunakosea maana naamini dini mtu akiwa serious inzidi kwenye siasa, viongozi wa dini wanaweza wambia watu wao wajiue na wakajiua lakini kwenye siasa watauliza tunajiua kwanini. Mimi simwamini kakobe hata kidogo lakini namheshimu sana kwani ameshiria maisha ya waumini zaidi ya 300 ambao akiamua kuwateketeza anaweza bila kizuizi, then huyu huwezi mlinganisha na Mbowe ambaye hata akimwambia Zito wajiue kupinga tume ya uchaguzi Zito hawezi fanya.

Swala la dini halina elimu nenda kwa mwingira uone jinsi ambavyo watu wenye elimu zao wanavyopagaishwa na dini.

Mandela alikuwa mwanasiasa na watu walikuwa wanamfuata na kumwamwini na walikuwa tayari kufa kwa ajili yake

Raila ni mwanasiasa na wako watu wake nyuma yake mchana na usiku

Tatizo liko pale pale kama watu hawapo tayari kukufuata all the way through basi wewe si kiongozi mzuri hilo la kwanza

La pili inawezekana hujawaelimisha wakaelewa unachodai au madai yako ni feki hayako worth kufa ..mtu

Unachosema ni kwamba madai ya ufisadi, katiba na tume huru inawezekana si kweli au hayana uzito mkubwa kwa wananchi au hakuna aliyewaelimisha wananchi wakaelimika?
 
Kakobe naye tapeli anawadanganya wananchi wanashinda juani, hawafanyi kazi halafu anawataka wampelekee sadaka.
 
Ni rahisi kuunganisha watu wa dini amabo wako kanisa moja kuliko kuunganisha wananchi wenye misimo tofauti na hasa ishu yenyewe ikiwa inahusu siasa.Imani ya dini ni kitu kingine bwana..mkiamua mmeamua hakuna kurudi nyuma.
 
Inabidi msema kweli atuandikie viongozi wa upinzani ambao nia yake ni kuwinda ruzuku. teh teh teh

Natania, mkuu lakini implication ya kuwa na vyeti feki ni kama kuwa na upinzani feki.

That is reality Mkamap, upinzani is another sector that creates employments!
 
Watu walikufa Mwembechai, Watu wanabomolewa Nyumba zao kwa magreda kupisha Ujenzi wa Barabara je unafikri ni kwa nini Serikali haichukui hatua kwa Kakobe? Je Ni sahihi kulinganisha Viongozi wa Dini na Siasa?

Mimi naweza kuwa muumini wa Kakobe au hata wa Pengo at the same time ni Mwanachama wa TLP, lakini Mrema akisema tukaandamane kupinga serikali kupitisha Umeme most likely nikampiga chini but the same kauli ikitolewa na Pengo au Kakobe Naweza kuandamana
 
Japo sikubaliana na msimamo wa kakobe kuhusu kupita umeme au kutopita katika eneo la kanisa lake lakini amenifurahisha kwamba anaweza kuwaongoza waumini wake wakaungana kudai wanachodai na wengi kama sio wote wako naye daima..wanamuamini na wanamfuata...

Ukilinganisha na vyama vyetu vya Upinzani (CUF, CHADEMA etc) wameshindwa kwa miaka mingi kuwaunganisha watanzania kudai vitu vya msingi kama katiba mpya, tume huru ya uchaguzi, kushughulikia mafisadi etc..

My conclusion: Wapinzani hakuna leaders ambao wanaweza kupata watu mia tatu wanaowaamini kama kakobena waumini wake wakadai bila uwoga madai ya msingi????

- With all due respect mkuu wangu T, Kakobe ana-represent ishus ambazo at its core ni spiritual, as opposed na Upinzani ambao wana-represent ishus za politics ambazo basically ni ishus zinazohitaji physical demonstrations, sasa no matter how you try to reconcile hizi ishus mbili huwezi pata balanced au similar results. Kwa sababu ni ishus mbili tofauti, kumbuka Upinzani wa Tanzania ni mchanga sana kuulinganisha na imani za kidini ambazo zimekuwepo years and years sasa kina Kakobe wanaziendeleza tu,

- Sometimes we underestimates sana Wapinzani bila kujali kwamba wametufanyia taifa mengi sana mazuri, lakini tatizo ni sisi wananchi ambao we are at point of no return, yaani masikio ya kufa ambayo hayawezi kusikia dawa! hawa kina Chenge na the likes hawapelekwi bungeni na wapinzani!

- Huu ni wakati wa sisi wananchi kujiangalia na kutafakari kama kweli we deserve Upinzani! Maana the experience inaonyesha we deserve kina Chenges! Ni sisi wananchi ndio hasa part of the problem, labda siku moja tutaamka na kuwa part of the solution!

Respect.


FMEs!
 
- With all due respect mkuu wangu T, Kakobe ana-represent ishus ambazo at its core ni spiritual, as opposed na Upinzani ambao wana-represent ishus za politics ambazo basically ni ishus zinazohitaji physical demonstrations, sasa no matter how you try to reconcile hizi ishus mbili huwezi pata balanced au similar results. Kwa sababu ni ishus mbili tofauti, kumbuka Upinzani wa Tanzania ni mchanga sana kuulinganisha na imani za kidini ambazo zimekuwepo years and years sasa kina Kakobe wanaziendeleza tu,

- Sometimes we underestimates sana Wapinzani bila kujali kwamba wametufanyia taifa mengi sana mazuri, lakini tatizo ni sisi wananchi ambao we are at point of no return, yaani masikio ya kufa ambayo hayawezi kusikia dawa! hawa kina Chenge na the likes hawapelekwi bungeni na wapinzani!

- Huu ni wakati wa sisi wananchi kujiangalia na kutafakari kama kweli we deserve Upinzani! Maana the experience inaonyesha we deserve kina Chenges! Ni sisi wananchi ndio hasa part of the problem, labda siku moja tutaamka na kuwa part of the solution!

Respect.

FMEs!

Mkuu,
Mawazo yangu ni kwamba ikiwa hakuna kiongozi wa upinzani ambaye ataleta mwamko kiasi kwamba watu wake meaning (wananchi) wakamuamini na kumuelewa kama kakobe alivyowaelewesha waumini wake kuhusu umeme wa tanesco? basi hatuna viongozi bado

Wananchi mtawalaumu bure mkuu kama hakuna kiongozi anaweza kutoa elimu au akafundisha watu wakaelewa then tuna problem kwenye leadership (nakumbuka mrema alileta mwamko hadi kijijin alieleweka sivyo?)

Mimi bado naamini Mandela, Raila, Gandhi etc hawakutumia dini yeyote mpaka wakakubalika isipokuwa walikuwa viongozi wenye wafausi wanaowaamini kwa vitendo vyao na kwa maneno yao?

Nimewa challenge viongozi wa upinzani waanze kuwauliza hata kwenye department zao (less than 10 people) kama wote wanamuamini yeye kwa matendo na kauli zake...ili wawakilishe watanzania? kama sample gues what hakuna?

Kiongozi bila wafuasi wenye kuwa tayari kutetea kwa kila hali (mbay na nzuri) just quit ...hicho ndicho kipimo alichonifundisha baba yangu...
 
Maendeleo ya Tanzania hayateletwa na Upinzani wala CCM.
Maendeleo ya kweli yataletwa na watanzania wazalendo ,wenye nia ,sababu ,shauku na hamu ya kutaka kufanya hivyo.

Watu wanapiga kelele upinzani kuongeza wabunge teh teh teh ofcourse wanafanya hivyo maana wanatambua wabunge wakiongezeka dau linaongezeka kituo kikubwa.
 
wapinzani,? ninaowaaminia tu ni cuf-zanzibar, wapinzani bara hamna kitu, kujipa matumaini yasiyokuwepo, we angalia tu, Mbowe, Slaa ...... taja

Hakuna namna ambayo mtu mwenye akili timamu akasema kuna upinzani bara!

wanajitetea kwenye kivuli eti watu hawana elimu!, Tumaini, wakati Mkwawa anawapiga wajerumani alikuwa amesoma shule gani? wafuasi wake walikuwa wanasoma JF?

Simply I hate them!

Watu wengine bana, kama hakuna upinzani kwa nini wewe mwenye akili timamu usianzishe upinzani wa kuaminika? Kukaa tu pembeni na kutegemea wengine wakufanyie kazi.
 
Kakobe anawaumini mia tatu lakini madai yake (japo mimi naamini ame-over state issue yenyewe) lakini ameweza kuonyesha kwamba number is not the issue...

Hizo streotype kwamba watu hawana elimu ina maana wao hawana elimu kabisaa...

Kama una elimu unaweza kumfundisha mtu yeyote akakuelewa na kukuamini, hawaamini kwasababu wao wenyewe hawana elimu/maarifa ya kuwaambia wananchi wanachoelewa au wanachoamini!

Najiuliza hata wafuasi mia tatu jamani then...huko upinzani bado sana...

Wapinzani (esp chadema) waliongoza wananchi wa Tarime kupinga kodi ya maendeleo miaka kibao kabla serikali haijaamua kufuatilia suala la kodi ya maendeleo.

Wewe ulikuwa wapi kujua hili? ahhh nimekumbuka ulikokuwa .......
 
Wapinzani (esp chadema) waliongoza wananchi wa Tarime kupinga kodi ya maendeleo miaka kibao kabla serikali haijaamua kufuatilia suala la kodi ya maendeleo.

Wewe ulikuwa wapi kujua hili? ahhh nimekumbuka ulikokuwa .......

Hivi kodi ya maendeleo imefutwa lini?
 
Watu wengine bana, kama hakuna upinzani kwa nini wewe mwenye akili timamu usianzishe upinzani wa kuaminika? Kukaa tu pembeni na kutegemea wengine wakufanyie kazi.

Mkuu acha kushambulia personal. teh teh teh

Nafikiri watu wenye akili timamu wao hawataki upinzani, wao wanataka maendeleo na maendeleo sio upinzani na upinzani si maendeleo.teh teh
 
Elimu ni msingi wa maendeleo ..... nilifundishwa hili nikiwa darasa la kwanza. Jipatie elimu mkuu kwenye mambo unayojihusisha nayo mara kwa mara (mf jukwaa la siasa la JF).

sawa nimekubali naomba unielimishe kodi ya maendeleo ilifutwa lini? nitajitahidi kutilia maanani ushauri wako.
 
Mkuu acha kushambulia personal. teh teh teh

Kitu gani nilichosema hapo ni ushambulizi personal? Mtu akishasema kuwa watu wenye akili timamu hawaoni kama kuna upinzani Tanzania anamaanisha kuwa wale wanaoona kuwa kuna upinzani Tanzania hawana akili timamu.

Nafikiri watu wenye akili timamu wao hawataki upinzani, wao wanataka maendeleo na maendeleo sio upinzani na upinzani si maendeleo.teh teh

Mimi nafikiri kuwa watu wenye akili timamu wanaelewa kuwa watu wenye wenye akili timamu wana uwezo na kila sababu ya kuchagua kama wanataka upinzani au la.

Mambo ya wewe kusema kuwa watu wenye akili timamu hawataki upinzani (hasa ukichukulia madhira yote yaliyoletwa na chama tawala Tanzania) ni zaidi ya fikara za kawaida.

Nilichomwambia Waberoya ni kitu simple, kama anaona upinzani ni hovyo, kwa nini asianzishe upinzani wake wenye nguvu ili watu waone mfano wa upinzani bora?
 
Kitu gani nilichosema hapo ni ushambulizi personal? Mtu akishasema kuwa watu wenye akili timamu hawaoni kama kuna upinzani Tanzania anamaanisha kuwa wale wanaoona kuwa kuna upinzani Tanzania hawana akili timamu.



Mimi nafikiri kuwa watu wenye akili timamu wanaelewa kuwa watu wenye wenye akili timamu wana uwezo na kila sababu ya kuchagua kama wanataka upinzani au la.

Mambo ya wewe kusema kuwa watu wenye akili timamu hawataki upinzani (hasa ukichukulia madhira yote yaliyoletwa na chama tawala Tanzania) ni zaidi ya fikara za kawaida.

Nilichomwambia Waberoya ni kitu simple, kama anaona upinzani ni hovyo, kwa nini asianzishe upinzani wake wenye nguvu ili watu waone mfano wa upinzani bora?

Kwa hiyo wewe unauona je upinzani uliopo?
 
Back
Top Bottom