Kakobe aunga mkono UKAWA

Kakobe aunga mkono UKAWA

Kipenzi Changu

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
57,954
Reaction score
134,031
Mch.Zakaria Kakobe ameunga mkono kundi imara la UKAWA kusimamia msimamo wao wa kutorudi bungeni kama maoni ya wananchi hayatazingatiwa.Pia amewashangaa viongozi wa wengine dini kuwataka UKAWA kurudi bungeni bila kushauri namna ya kutatua mgogoro."Mbona hamuishauri CCM ijadili rasmi ya wananchi,mnawataka tu UKAWA kurudi bungeni" alisisitiza Mch.Kakobe.Source:Nipashe!
 
Kakobe siku zote ni mpiga debe wa wapinzani.
Ni kweli Mkuu. Nimemshangaa sana mleta uzi kwa kujitoa ufahamu. Ni huyu huyu Kakobe aliyewahubiria waumini wake kanisani juu ya umuhimu wa serikali tatu na kawadanganya eti ni chaguo la Mungu
 
kakobe alishapoteza mvuto aunge mkono asiunge impact yake ni ndogo sana
 
Ni kweli Mkuu. Nimemshangaa sana mleta uzi kwa kujitoa ufahamu. Ni huyu huyu Kakobe aliyewahubiria waumini wake kanisani juu ya umuhimu wa serikali tatu na kawadanganya eti ni chaguo la Mungu

Ufahamu uliokosa uhuru ni utumwa
 
Kakobe siku zote ni mpiga debe wa wapinzani.

Ni bora Kakobe anayepigia debe wapinzani kwa utashi wake mwenyewe kuliko viongozi wengine wa dini ambao baadhi yao wapo kwenye bunge la katiba wakipigia debe CCM kwa kuhongwa ili wachakachue maoni ya wananchi.
 
Ni kweli Mkuu. Nimemshangaa sana mleta uzi kwa kujitoa ufahamu. Ni huyu huyu Kakobe aliyewahubiria waumini wake kanisani juu ya umuhimu wa serikali tatu na kawadanganya eti ni chaguo la Mungu

Halafu mwaka 2010 aliwadanganya kondoo wake kuwa Mzee Slaa ni chaguo la Mungu hivyo wampe kura!
 
Ni bora Kakobe anayepigia debe wapinzani kwa utashi wake mwenyewe kuliko viongozi wengine wa dini ambao baadhi yao wapo kwenye bunge la katiba wakipigia debe CCM kwa kuhongwa ili wachakachue maoni ya wananchi.

Una uhakika gani kama Kokobe anafanya hivyo kwa utashi wake mwenyewe? juzi juzi tu hapa alikuwa analia lia na kumuandikia rais waraka kisa hakuchaguliwa kwenye bunge la katiba!
 
Move s3 ni ya majority. Inaweza kuzimwa tu na wachache kwa kutumia jeshi. Kwa mazingira ya kisiasa ya Tanzania jeshi halina mpango huo. Si muda mlefu mwafaka utapatikana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom