Kaka zangu wametembea na mwanamke mmoja

Kaka zangu wametembea na mwanamke mmoja

Midekoo

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2015
Posts
47,775
Reaction score
257,516
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza,

Kwakweli niko njia panda mimi kama dada au mama wa familia nimeshindwa kulitatua, nimeshindwa kumshirikisha mtu yoyote hata ubavu wangu wa pili nimeshindwa kumshirikisha naona aibu nitawavua nguo kaka zangu ila humu naona ni mahala sahihi naweza kupata mwanga kidogo.

Picha linaanza hivi, hapa mjini tunakibanda chetu cha urithi familia tukaamua akae mama pamoja na kaka mkubwa na familia yake uwani kuna vyumba vitatu yupo mpangaji kutokana na changamoto za ndoa kaka na mke wake kwa sasa wana mgogoro wa ndoa yao mke amerudi kwao kwa muda.

Huyu mpangaji yeye anaishi na mke wake lakini yeye ni mganga wa kienyeji shughuli zake anafanyia Arusha pale kabaki mke wake tu.

Kwa mara ya kwanza alivohamia huyu mke wa mganga alitongozwa na mtoto wa jirani akampa taarifa mume wake, kilichotokea mganga alimpigia simu bi mkubwa, yule bwana akatoa mkwara mzito sana, kwa yoyote atakaye toka na mke wake litakalomkuta asije akajuta baadae hili likapita.

Sasa huyu dada kwa kifupi alitoa tu taarifa kwa mumewe kujikosha kumbe kiwembe ukimpa safari tatu na elfu kumi unajisevia vya kutosha mtaani wauza magenge, wauza mabucha, bodaboda wanajisevia.

Sasa miezi kazaa nina kaka angu mwingine makazi yake ni nje ya Dar alikuja mapumziko kumuona mama kilichotokea huyu dada alitembea nae sikujua kama aliijua tabia yake ila ndio hivyo ila muda wa mapumziko ulipoisha aliondoka.

Sasa hivi nimepewa taarifa tena kaka mkubwa ameanza kutembea nae na mchezo wote unafanyika ndani ya nyumba wakati wa usiku kwenye chumba cha huyo dada. Huyu dada mpangaji ana urafiki na mtoto wa mama angu mdogo anaishi hapo nyumbani kwahiyo kila analofanya anamwambia huyu ndugu yangu ndipo habari nazipata

Maswali nayojiuliza je kaka zangu wanajijua wameshashare mapenzi kwa mwanamke mmoja?
Je, kama huyu dada ameathirika inakuwaje?
Je, mume wake akifahamu atafanya nini?
Nimwambie mama mzazi kinachoendelea? (Baba amefariki)
Inaniuma ufuska unafanyika ndani ya nyumba cha kufanya sina kaka zangu nawaona kama baba zangu na wao wananiona mama wa familia sijui pakuwaanzia kuwaeleza hili jambo.

Na uwezo wa kuwashawishi ndugu zangu tumpe notice je nikiulizwa chanzo nini? Kwenye kulipa kodi wako vizuri hawasumbui.

Naombeni ushauri nifanyeje jamani roho naniuma sana japo kuna watu watanishangaa kwanini niumie ila ndio hivyo binadamu tuko tofauti.
 
Pole sana ndugu ungemueleza uyo wa Dar tu kua aache tabia yake na umwambie kua ndugu yake nae alipitia apo anapopitia yeye sasa hivii kwahyo aache iyo tabiaa.
 
Kama kuna baba wadogo washirikishe waongeee na huyo bro wa hapo home,ikishindikana hata mama mwambie amkanye kakako mke wa mtu sumu na ukimwi unaua.
 
Pole sana hapo ukiwaambia kaka zako itakuwa km unawavunjia heshima!
ni kosa kutembea na mke wa mtu lakini tatizo linaonyesha ni mke wa mganga itakuwa hajiheshimu ni arage la mbeya huyo!dawa mwambie mama amfukuze akapange kwingine moja ya sababu ya kumtimua nyumba itarudisha heshima na mabro wako wataamua sasa wamfuate huko aliko au wapotezeee tu.
 
Kwa sisi wanaume hilo siyo tatizo, usijali.
 
Itakuwa mnaishi serious sana na kaka zako, unashindwa hata kuwatania tania!!! Jifanye Kama unatania tu, ujumbe utawafikia na wataulizana wao, na wataweka kila kitu Sawa.
 
.....Kama kuna baba wadogo washirikishe waongeee na huyo bro wa hapo home,ikishindikana hata mama mwambie amkanye kakako....mke wa mtu sumu na ukimwi unaua..
Kabisa kwakweli, sisi mjini ndugu baba zetu wadogo na wakubwa wote wapo nje ya Dar marehemu baba Pekee ndio alikuwa anaishi Dar.
 
Pole sana.
Hapo ukiwaambia kaka zako itakuwa km unawavunjia heshima!
Ni kosa kutembea na mke wa mtu lakini tatizo linaonyesha ni mke wa mganga.itakuwa hajiheshimu ni arage la mbeya huyo!dawa mwambie mama amfukuze akapange kwingine.moja ya sababu ya kumtimua nyumba itarudisha heshima.na mabro wako wataamua sasa wamfuate huko aliko au wapotezeee tu.
Asante sana kwa ushauri wako.
 
January wamelipa kodi ya awamu ya pili.
mwambie bi mkubwa yeye anaweza ongea nao maana ndo mama lakini ishu kubwa hapo ni je huyo dada yuko salama maana umedai ye sio mchoyo


Long distance ilikuwa kwenye local distance trade(kwenye ukoloni) na sio kwenye relationship
 
Unakaa vp mbali na mkeo?!


Kama yeye mganga kweli angejua kama mkewe anachia nyapu kwa kila mtu
Huyu anaweza akawa mganga tapeli ila ukweli utabaki palepale mke wa mtu sumu mwenyewe akijua hatujui uamuzi atakaochukua.
 
Fanya yanayo kuhusu mama mengine achana nayo kwao hao ni watoto wadogo

ukifuata ya watu yako utachelewa kuyafanya mjini hapo. oooh
Japo hayo ila ndio baba zangu baya litakalowakuta litaniathiri mimi pia kwa aina moja au nyingine
 
Huyu anaweza akawa mganga tapeli Ila ukweli utabaki palepale mke wa mtu sumu Mwenyewe akijua Hatujui uamuzi atakaochukua.

Mwanaume wa kweli ukijua mkeo au mpenzi wako analiwa solition na kumuacha tu hayo mambo mengine utapoteza mida tu
 
Hapa kwa jinsi ulivyoandika, kama mganga yuko hapa JF, atakuwa ashaelewa story yote kwamba anazungumziwa mkewe, tena na hivyo wamelipa kodi mwezi January!....Kama kuna watu wazima kama wajomba, ungeweza kuongea nao ukawaelezea wakaweza kuongea na kaka zako, kama inakuwa shida wewe kuongea na kaka zako.
 
Back
Top Bottom