Wanabodi,
Baada ya figisu figusu za uchaguzi wa marudio wa madiwani, nimebahatika ya kufanya mahojiano na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Ramadhani Kailima, yaliyofanyika ofisini kwake jioni hii, kuhusu uchaguzi huo, katika kipindi cha Habari Zaidi ya Habari na PPR, ambacho kinarushwa kupitia Vituo 5 vya TV, TBC, ITV, STAR TV, Channel Ten, Azam TV, Clouds TV na kwenye Youtube.
Hizi ni Baadhi ya Dondoo za Mahojiano Hayo.
- Zoezi la Uchaguzi limekwenda vizuri kwa asilimia 95%, hakukuwa na kasoro yoyote kubwa kuathiri uchaguzi huo, hivyo uchaguzi umekamilika na taarifa rasmi, itatolewa punde itakapokamilika.
- Uchaguzi huo ulikuwa ni uchaguzi huru na wa haki, licha ya kutokea mapungufu madogo madogo, lakini matokeo ni matokeo halali, aliyeshinda ameshinda kihalali kwa haki, aliyeshindwa, pia ameshindwa kihalali kwa haki.
- Hakuna hata chama kimoja, kilicholalamikia jambo lolote kuhusu uchaguzi huo, mpaka sasa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi, haijapokea malalamiko yoyote, kutoka chama chochote, au mgombea yoyote kwa mujibu wa utaratibu wa kujaza fomu za malalamiko.
- Hakuna chama kilichojitoa rasmi, ila kama ilivyo kushiriki uchaguzi ni hiyari, vivyo hivyo vyama viko huru kujitoa wakati wowote, lakini mpaka zoezi la uchaguzi linamalizika, hakuna chama kilichojitoa rasmi kwa mujibu wa taratibu za kujitoa.
- Mawakala wa vyama, wanapatikana kwa mujibu wa sheria, taratkanuni, mtu ambaye hajakidhi taratibu za uchaguzi, hawezi kuruhusiwa
- Ameelezea kuwa Tume yake ni Tume huru, inayoendesha chaguzi kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, hakuna chama chochote, kimewahi kulalamikia kipengele chochote cha uchaguzi kinachonyima haki, kitakachoifanya tume isiwe huru.
- Amesisitiza Tume yake haijawahi kuingiliwa na chombo chochote, wala kupokea maagizo au maelekezo kutoka kwa yeyote.
- Tume yake haijawahi kufanya upendeleo wowote kwa chama chochote, hata CCM nayo pia inailalamikia tume yake, hata uchaguzi wa Madiwani CCM Arusha wamelalamika.
- Pia nimeuliza kuhusu Mkurugenzi, Mwenyekiti wa NEC na makashna kuteuliwa na rais ambaye ni mwenyekiti wa chama kimoja, wataweza kutenda haki?, pia amelijibu.
My Take.
Its high time vyama tuanze kutake responsibilities kwa matokeo ya utendaji wa vyama vyetu kwenye chaguzi, kwa pale ambapo uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, tukubali kushindwa kihalali, asiyekubali kushindwa sio mshindani, badala ya kutafuta visingizio.
Kama hali ya uwezo wa ushindani kwa vyama vyetu vya upinzani nchini Tanzania, jee hali itakuwaje uchaguzi wa 2020?. Kama wapinzani hawatabadili strategies, za namna ya kushindana na CCM kwenye sanduku la kura, kuna hatari ya CCM, kuyarejesha majimbo yote ya upinzani mwaka 2020, hivyo Tanzania kuanza safari ya kuelekea kuwa ni nchi ya vyama vingi jina tuu, lakini ukweli tunaelekea kuwa nchi ya chama kimoja.
NB. Kipindi kikiwa tayari, nitakipandisha humu umsikilize mwenyewe.
Wasalaam.
Paskali
Update 1.
Mkuu Joka Kuu, kwanza asante sana, kwa sababu tangu bandiko hili limepanda hadi kufikia michango 537, mchango wako ndio the most deep, the most objective, the most professional and the best analysis of the contents, kwa sababu it is the content that matters, japo the clip ni just 10 min clip, ni watu wachache sana wameiangalia na kumsikiliza, but wewe you did. Thanks for this.
On Professionalism
Uko very right one one interviews program zinahitaji 3 cameras, ya interviewer, ya interviewee na ya wide ili kuyaonyesha maswali, majibu na setting.
Hata kama zimekosekana kamera 3, then kupitia camera moja ilibidi kuyauliza maswali on camera, na kuisert majibu, na kupiga cutaways. Hivyo ni kweli kabisa the interview was unprofessional. Nakubali makosa.
On Preparation na Research.
Kabla ya kufanya any good interview, inakubidi ufanye a little research and gether all the facts, ufanye a background check on your subject who is Kailima, elimu yake, ametokea wapi hadi kuibukia NEC, uwezo wake na utendaji wake, Jee ana uwezo, ana deliver etc. Hili halikufanyika, huu pia ni udhaifu on my part.
Interview Questions.
Ilibidi nitayarishe maswali ya msingi yanayoitwa leading questions at least matano kuhusu uchaguzi huo yakifuatiwa na follow-up questions.
Kila mwandishi analo eneo la strength na weaknesses zake, hivyo kiukweli kwa upande wangu, my strength ni kwenye interviewing haswa kwenye ku shoot maswali ya kushtukiza, lakini kwenye interview hii, hili pia halikufanyika, ni kama nimempa Kailima mteremko he just flow, hili ni kosa on my part ila ni kwa sababu, for a reason!.
The Reality And The Truth Kuhusu Hii Interview.
Kwanza naomba kukiri wazi hii interview, was impromptu, haikupangwa. Nimekutana na Kailima kwenye ngazi akielekea ofisini kwakwe, nikamuomba news interview ya just 5 minutes kuhusu uchaguzi wa marudio wa madiwani, akakubali. Hivyo there was no time for preparations, kutayarisha camera mbili, wala hakukuwa na maswali yoyote yaliyotayarishwa, maswali yote yalitoka kichwani, na majibu yote ya Kailima yalitoka kichwani.
Kwa Nini Nilimuuliza Maswali Rahisi Rahisi Bila Follow-up Questions?.
Kusema ukweli kupata chance ya impromptu interview na Mkurugenzi wa Uchaguzi Tanzania, was like a favour to me, not a right, hivyo kiukweli Kailima ameniheshimu sana kunikubalia interview ile hivyo hata maswali yangu ilikuwa lazima ya reciprocate favours niliyoipata, kwa kuto mbo bombard na maswali magumu, ili kumjengea mazingira mazuri ya future interviews kuelekea 2020. Ukiaminiwa, Jiaminishe, niliaminiwa na Kailima, ilinibidi tuu niwe mdogo to start with lakini kuna good things kuhusu Tume ya Uchaguzi vinakuja in future. Keep waiting, keep watching.
Paskali