KAMPUNI YA FUJIANI YATANGAZA RASMI KUANZA UCHIMBAJI WA MADINI YA CHUMA MAGANGA MATITU LUDEWA
Kampuni ya Fujiani imeitangaza rasmi kuanza uchimbaji wa madini ya chuma Maganga Matitu, katika eneo la Maganga Matitu lililopo Wilaya ya Ludewa, mkoani Njombe. Uchimbaji huu unatarajiwa kuanza kabla ya mwezi wa tano mwaka 2025. Kampuni hiyo imeeleza kuwa mradi huu utaleta manufaa makubwa kwa wakazi wa Ludewa, ikiwemo fursa za ajira na kuimarisha uchumi wa eneo hilo na taifa kwa ujumla.