tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Jeshi la Polisi mkoani Kagera limewakamata baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa tuhuma za kuhusika na kupanga mikutano na maandamano kinyume cha sheria.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Brasius Chatanda, amethibitisha kukamatwa kwa viongozi hao na kueleza kuwa uchunguzi unaendelea ili kubaini ukweli wa madai hayo
Soma pia: Jeshi la Polisi lajipanga kudhibiti vurugu siku ya Uchaguzi
Amesema “Ni kweli tunawashikilia viongozi hawa pamoja na wanachama wengine watatu wa chama, wanatuhumiwa kuchochea machafuko ya umma kwa kuandaa maandamano, ni miongoni mwa watu 17 tuliowashikilia katika kipindi chote cha kampeni za uchaguzi,” alisema Kamanda Chatanda.
Imeelezwa viongozi hao wanadaiwa kuhusika katika kuhamasisha wafuasi wa chama hicho kushiriki maandamano yaliyopangwa kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini.
Aidha, Kamanda Chatanda amesema hatua zaidi zitachukuliwa mara baada ya uchunguzi kukamilika. Jeshi hilo pia limewataka wananchi kuwa watulivu na kufuata sheria wakati wa kipindi hiki cha kisiasa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Brasius Chatanda, amethibitisha kukamatwa kwa viongozi hao na kueleza kuwa uchunguzi unaendelea ili kubaini ukweli wa madai hayo
Soma pia: Jeshi la Polisi lajipanga kudhibiti vurugu siku ya Uchaguzi
Amesema “Ni kweli tunawashikilia viongozi hawa pamoja na wanachama wengine watatu wa chama, wanatuhumiwa kuchochea machafuko ya umma kwa kuandaa maandamano, ni miongoni mwa watu 17 tuliowashikilia katika kipindi chote cha kampeni za uchaguzi,” alisema Kamanda Chatanda.
Imeelezwa viongozi hao wanadaiwa kuhusika katika kuhamasisha wafuasi wa chama hicho kushiriki maandamano yaliyopangwa kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini.
Aidha, Kamanda Chatanda amesema hatua zaidi zitachukuliwa mara baada ya uchunguzi kukamilika. Jeshi hilo pia limewataka wananchi kuwa watulivu na kufuata sheria wakati wa kipindi hiki cha kisiasa.