Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Pamoja na nchi kulalamikia mgao wa umeme unaoendelea baadhi ya watu walioishi hapa Kagera kwa muda mrefu wanashangaa nikiwemo mimi niliyehamia mwaka mmoja uliopita Kutoona hata siku moja ukiacha tatizo la kiufundi eti umeme wa mgao!! Huku masaa yote umeme upo tu. Ikabidi niulize inakuwaje? Nikaambiwa aaahhh umeme wa hapa unatoka hapo nchi jirani Uganda japo bili unalipia Tanesco. Sasa nikaanza kufikiri kuwa hao wenye viwanda mbaimbali waliosotisha uzalishaji sababu ya kukosa umeme, walete huku mitambo yao maana umeme full time loh!! Kazi yao iwe ni kusafirisha mali ghafi au kufanya taratibu ya kuzizalisha hapa, maana mkoa huu almost kila zao kwa mfano wale wa mafuta, linaota isipokuwa watu wa huku wavivu ile mbaya. Ardhi ina maji kibao lakini loh!! nani alime mpunga, mpaka wasukuma wachache ndo wameshtukia dili wanaanza kulima na wanavuna mpunga mnene kinoma. Ebwanae mwenye Capital aje tufanye business. Huku natoa tahadhari kwa mgombea yeyote katika ahadi zake asiongelee kuwa kuna kero ya umeme labda kuufikisha mahali usipo. Pia nimeshangaa hadi migombani umeme unawaka, nyumba chache tu kwenye kijiji ambacho kuna nshomile aliyeko out au Proffessors, umeme utakwenda tu loh. Haya jamani njooni huku muwekeze maana utadhani sio Tanzania hapa!!!!>