Uhusiano wetu na Kenya ni wa machale sana hasa ukichagizwa na tamaduni. Kenya wana aina ya superiority complex waliyokuwa nayo bila kujali kuwa ime expire katika zama hizi
Viongozi wamejaribu kurudisha mahusiano kama ulivyoshudia wakati wa uchaguzi uliopita akina Kenyatta na Odinga walikuwa hawaishi kukanyaga Dar es Salaam
Tena watu hawafahamu kuwa katika viongozi waliomtetea sana Uhuru JK ni mmoja, vinginevyo mataifa yalishaweka ngumu asigombee. Nadhani unakumbuka kila mwezi walikuwa Magogoni.
Hilo ndilo eneo la foreign policy pamoja na lile la kusuluhisha vita niyaonayo wamefanyakazi pamoja
Kwa upande mwingine mambo ya uchumi yanazidi kuwa magumu hasa baada ya vita ya pembe za ndovu Qatar na mradi wa bara bara wa Serengeti. Nakubaliana kabisa nawe kwa hilo, kwamba kunahitajika improvement
Kuna kitu kinaitwa Ukenya, kwa maana urafiki na mkenya lazima uwe na faida kwake baada ya hapo hakuna urafiki tena na hilo ndilo chanzo cha machale ya Tanzania.
Sasa hivi kuna triple K inayoendelea na EAC.
Kenya wanaangalia uchumi tu baada ya dili kukamilika utaona wanarejea Tanzania.
Watarejea TZ na kuwatosa wenzao kwasababu katika EAC sisi ndio wenye mpaka mkubwa, trade kubwa na Kenya na wao ni second investors katika TZ. Mfano, single entry visa na Kagame itamsaidiaje Mkenya! lakini akiwa na TZ ni dili. In short urafiki wa Kenya ni wa 'convinience'