Kufuatia kipigo cha vijana wake(M23), serikali ya Kigali imeonesha kughadhabishwa na hatua hiyo iliyo chukuliwa na serikali ya DRC ikisaidiwa na vikosi vya UN(Southafrica na Tanzania). Katika hali isio ya kawaida, taarifa za kipelelezi zinasema serikali ya kigali imekula njama na M23 ambapo waasi wa M23 hapo jana wamerusha kombora upande wa Rwanda na kusingizia vikosi vya DRC. Lengo ikiwa ni kuanzisha mtafaruku mpya kati ya Kigali na Kinshasa hvo kujenga uhalali wa Rwanda kuwasaidia ndugu zao M23 ambao wanaelekea kusambartika kufuatia mashambulizi yanayoendelej hivi sasa. Wachambuzi wanasema hali hii haina tofauti na wakati ule ambapo wapiganaji wa RPF wakiongozwa na Paul Kagame walitungua ndege ya rais mhutu wa wa Rwanda wakati huo na kujenga uhalali wa kuanzisha vita dhidi ya majeshi ya serikali na kuitumbukiza Rwanda katika mauaji ya kimbali.