Kada mashuhuri wa CCM ajiunga CHADEMA

huyo mroho wa madaraka.. Pokeeni zigo hilo lenye wivu wa madaraka.
Ila mwisho wa siku atarudi CCM.

Gogo wivu,
fanya haraka uje huku kabla majimbo yoote hayajaisha. Huyu si mroho wa madaraka ni mtu aliyeona mbali. 2015 sio mbali, siku hazigandi bali zinayeyuka tu. Utastukia kura hiyooo nawe utakuwa upande wa wale walioambiwa na M/kiti wao kuwa wajiandae kisaikolojia. Wale ambao M/kiti wao aliwaombea huruma kuwa CDM ikichukua madaraka, wawasamehe makosa yao bure ka Mzee Madiba. Tamu hiyo.
Namuunga mkono M/kiti wako, nami namwomba Mh. Mbowe na Dr. Slaa wasirudishe baya kwa baya. Kariib Kamanda umevua gamba vaa Gwanda. Kwetu pazuuuri, nimesha pakumbuka...
 
Yawezekana mfululizo wa habari hizi ukawa wa kufurahisha na kushangiliwa leo. Lakini mbele kidogo uteuzi ndani ya vyama utakapoanza, furaha yote itageuka kuwa majonzi! Uhamiaji wa kasi mida hii ulipaswa kuchukuliwa kama ishara kwa Watendaji wa vyama vya Upinzani kuandaa mfumo bora amabo hautaleta migongano na mitafaruku wakati wa kupitisha wagombea ndani ya chama. Badala yake wanachama, wafuasi, viongozi na watazamaji sote tunashangilia kwa kuangalia mbele badala ya kutazama mbali!

Naomba kurejea huu mchango wangu wa siku za nyuma kwa Bw. Nyami2010:
 
Jamaa yupo fit! Nafikiri hii ni kazi nzuri ya mwenezi KAKOKO! bila kumsahau kamanda TALL pale Victoria.
 

Mapandikizi ya Mbowe hayo! Ameshakatiwa mabaki ya ruzuku, amuongeze nguvu kanda ya magharibi. Ngoja hela iishe utasikia tu.
 
Na bado,utaona mwakani itakavyokuwa.Walikuwa wanasubiri Chadema kusambaratika 2013 lakini mwaka umeisha bila mafanikio huku wakina Nchemba wakiwa wanakaribiwa na tuhuma za kulipua mabomu pale soweto
 

Njaa inamsumbua. Kwa hiyo hizo kero mbalimbali zinaweza kutatuliwa na Chadema? Toka lini Chadema ikatatua matatizo? Chadema ipo kuleta matatizo sio kuyatatua.
 
huyo mroho wa madaraka.. Pokeeni zigo hilo lenye wivu wa madaraka.
Ila mwisho wa siku atarudi CCM.

Amekimbia kumtoa kafara mwanae kwa lazima kama wanavyofanyiwa wenzake na Mwigulu kama alivyowafanyia wale wa Arusha.
 
Akienda Chadema nako atakutana na haya:
-Pesa ya Sabodo zimepigwa meno
-Wajanja wamekiuzia chama magari mabovu
-Wamejikopesha ruzuku za chama
-Millioni 140 alizokopa Dr. Slaa ziko wapi?
-Chama hakina ofisi ya maana
-Uchaguzi haufanyiki
-Ubaguzi umetapakaa kote.
-Kuna chadema chumbani na chadema sebuleni
 
Njaa inamsumbua. Kwa hiyo hizo kero mbalimbali zinaweza kutatuliwa na Chadema? Toka lini Chadema ikatatua matatizo? Chadema ipo kuleta matatizo sio kuyatatua.

Hahahaha maneno ya mkosaji haya, mpaka mwishoni mwa 2014 ccm mtabaki nyie na wake zenu tu, watanzania watakuwa tayari kwenda kwa wajanja chadema.
 
Umashuhuri wenyewe uko wapi mbona siuoni?

Kwani umashuhuri kwa tafsiri yako ni upi?!! Umashuhuri umeanza kuonwa kwa macho tangu lini. Ama kweli kusoma si kuelemika. !!!!
 
Hahahaha maneno ya mkosaji haya, mpaka mwishoni mwa 2014 ccm mtabaki nyie na wake zenu tu, watanzania watakuwa tayari kwenda kwa wajanja chadema.

Wake zao ndo tunaanza nao mkuu, watabaki wao tu na pesa walizotuibia.
 
Ni uamuzi wa busara,tumpokee ila aenende katika misingi ya chama:israel:
 
Dr karibu tumekusamehe dhambi zako zote njoo huku ni kazi tu baba tutakupa ushirikiano ulio tukuka
 

Amejitambua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…