Kachinjwa Mchana Kweupe ~ Moshi Bar

Kachinjwa Mchana Kweupe ~ Moshi Bar

Aisee watu hawana huruma, kuna jamaa anayedaiwa mwizi wa bodaboda kachinjwa Mchana huu pale Moshi Bar karibu Mazizini Dsm, ni kwamba jamaa alikamatwa maeneo ya Kigogo na madereva bodaboda, akapakizwa pikipiki watu 3 ye kawekwa katikati kaambiwa aelezee pikipiki alizoiba kaziweka wapi, bodaboda wakawa wanaitana kila wanapowaona wenzao, Wakaenda Kinondoni hawakuona pikipiki, jamaa akawaambia zipo maeneo ya gongolamboto Moshi bar, Wakaenda walipoona jamaa anawasumbua Wakaamua Kumchinja, mchana Kweupe.... Police wa Stakishari wamekuja kuuchukua mwili wake wameenda Muhimbili...

Tuache Wizi Jamani.... Tuache Makundi.
Please weka
Picha
 
Hawakupigwa picha? Hao waliofanya hivyo ni wahalifu pia, wanastahili adhabu ya kunyongwa, pengine jamaa hata sio mwizi alikuwa anawazungusha tu ku buy time ili aokolewe.

Jamaa akibuy time maana nasikia kuna sehemu alikuta washkaji zake akijaribu kupiga kelele kuomba msaada washkaji wakaogopa ile mob ya bodaboda... Siku ya kufa nyani
 
Ye angewaambia zipo kituo cha polisi tu akawapeleka kituoni tu
 
Nalaani walichokifanya bodaboda,ila hao bodaboda wanajifunza.........Polisi wetu wamekua wauaji wa raia mara kadhaa,na hatua zinazochukuliwa dhidi yao ni kama "0" tu.....Nao bodaboda wanapita mulemule.Lakini pia mchakato ungeenda mahakamani ungekua mrefu sana,jamani mahakama zetu si mnazijua?Mwisho wa siku hata kauli za viongozi zinachangia.Mnakumbuka kauli hizi.
1."Anayeua albino nae auawe"
2."Polisi waue tu majambazi"
3."Wapigwe tu,tushachoka"
Tusizichukulie powa hizi kauli,,,zinahamasisha sheria mkononi

Ni kweli mpendwa,

niongeze tu. kama bado mnakumbuka ukiukwaji wa waziwazi wa kanuni za bunge dhidi ya wapinzani wakati wa madam Makinda na Mr. Ndugai, wadau walikemea sana ila upande wa CCM walikuwa wakifurahi! hayo nayo yalikuwa ni matendo ya kujichukulia sheria mkononi!! naweza kusema kuwa pia yalihamasishwa matendo mengine ya kujichukulia sheria mkononi miongoni mwa wananchi.

RIP marehemu na pole nyingi kwa wafiwa

mbarikiwe sana wapendwa.

Golry to God!
 
Tatizo la bodaboda ni kufuata mkumbo, yani hili ni kundi hatari sana kwa usalama wasipodhibitiwa mapema. Wanaendesha bila kufuata sheria za barabarani wanasababisha ajali alafu wanachukua sheria mikononi bila kujali na chanzo cha ajali. Hata kama ni mwenzao akigonga gari kwa nyuma kosa linakua kwa mwenye gari wanachukua sheria mikononi nashangaa watu wanaunga mkono vitendo vya hovyo vya hawa bodaboda siku yakiwakuta ndo watajua hawana maana hawa
 
Nalaani walichokifanya bodaboda,ila hao bodaboda wanajifunza.........Polisi wetu wamekua wauaji wa raia mara kadhaa,na hatua zinazochukuliwa dhidi yao ni kama "0" tu.....Nao bodaboda wanapita mulemule.Lakini pia mchakato ungeenda mahakamani ungekua mrefu sana,jamani mahakama zetu si mnazijua?Mwisho wa siku hata kauli za viongozi zinachangia.Mnakumbuka kauli hizi.
1."Anayeua albino nae auawe"
2."Polisi waue tu majambazi"
3."Wapigwe tu,tushachoka"
Tusizichukulie powa hizi kauli,,,zinahamasisha sheria mkononi

Kweli kabisa kaka maana maneno huumba, kauli za viongozi wetu ndio zinazochangia haya mauaji
 
Ni kweli mpendwa,

niongeze tu. kama bado mnakumbuka ukiukwaji wa waziwazi wa kanuni za bunge dhidi ya wapinzani wakati wa madam Makinda na Mr. Ndugai, wadau walikemea sana ila upande wa CCM walikuwa wakifurahi! hayo nayo yalikuwa ni matendo ya kujichukulia sheria mkononi!! naweza kusema kuwa pia yalihamasishwa matendo mengine ya kujichukulia sheria mkononi miongoni mwa wananchi.

RIP marehemu na pole nyingi kwa wafiwa

mbarikiwe sana wapendwa.

Golry to God!
Huo wote ni ukiukwaji wa sheria,sasa unapotokea bungeni si kazi kuwa applied uraiani,uvamizi kwenye vituo vya polisi kwa sasa umekua wa hali ya juu,polisi kutandikwa na raia ni jambo la kawaida sana,,,,lakini pia hata watawala wetu huchukua sheria mkononi na huwa hawafanywi kitu ili jamii ijifunze...TUREJEE YULE MZEE ALOMTWANGA RISASI DEREVA WA DALADALA BAGAMOYO ROAD
 
kuna kijana kamaliza diploma ya usafirirshaji NIT nasikia ameuawa huko kivule kwa tetesi hizi hizi za wizi wa boda boda sijui ndie huyu?
 
kuna kijana kamaliza diploma ya usafirirshaji NIT nasikia ameuawa huko kivule kwa tetesi hizi hizi za wizi wa boda boda sijui ndie huyu?

Kama unamjua picha hizo hapo.. Angalia kabla mods hawajazitoa manake sio nzuri
 
Na tuache kujichukulia sheria mkononi.Kura moja hiyo imepotea

Duh! Labda ajira,labda tabia,labda makundi! Mmmh ila hii ya kuchinjana hapana asee!!

bodaboda inabidi wadhibitiwe kama kila mtu anajichukulia sheria mkononi hiiitakuwa sio nchi bahati mbaya wanasiasa wanawatumia kama mtaji wao kisiasa

Binafsi hata mimi nalaani matendo yoyote yanayoweza kusababisha uvunjifu wa amani lakini, tujiulize ni kwanini vijana hao wa bodaboda wanajichukulia sheria mkononi? jibu ni rahisi tu kuwa, sehemu inayotegemewa kutoa haki haitoi kabisa hiyo haki, na kama inatoa basi ni kwa kuchelewa! sasa hapo kumbe tatizo linaanzia kwa serikali yenyewe.
 
Ni kweli mpendwa,

niongeze tu. kama bado mnakumbuka ukiukwaji wa waziwazi wa kanuni za bunge dhidi ya wapinzani wakati wa madam Makinda na Mr. Ndugai, wadau walikemea sana ila upande wa CCM walikuwa wakifurahi! hayo nayo yalikuwa ni matendo ya kujichukulia sheria mkononi!! naweza kusema kuwa pia yalihamasishwa matendo mengine ya kujichukulia sheria mkononi miongoni mwa wananchi.

RIP marehemu na pole nyingi kwa wafiwa

mbarikiwe sana wapendwa.

Golry to God!

Glory not Golry my X
 
Sawa tu. Hapa kwetu mbagala kuu Jana mida ya saa moja jioni bodaboda alikodiwa na jamaa baada ya kuingia cjochoro jamaa akampiga nondo na mwizi akatokomea na boxer kwa spidi ya hatari. Tulipofikia pana tisha. Maana mjni mtu anafanyiwa uharamia mapema tena kweupe.
Nawapigwe tu maana hakuna namna!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom