Kabla ya kumshangaa Paul Biya na Ally Bongo tumshangae Tundu Lissu

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Ndugu zangu,

tuite koleo,koleo, nimekuwa kwenye kundi sogozi la watsapp ghafla zikaanza kurushwa picha nyingi za baadhi ya wanasiasa wa nchi za ng'ambo hususani Africa na kwingineko. Wengi walionekana kukerwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa kung'ang'ania madaraka hata pale wanapokuwa hospitalini wakiuguzwa kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Kwa sababu jambo hilo lilitokea katikati ya mkutano wa SADC mwingine akarukia ''angalia hata huyu Mswati hana msaada wowote kwa taifa lake lakini anatawala milele'' hawa waliotawala mjadala huu wanajiita ''wanamabadiliko'' wanataka kuona Afrika na Tanzania inatawaliwa na vyama tofauti na vile vya ukombozi.

Ndugu mmoja alinitumia ujumbe binafsi akitaka asikie maoni yangu nikamwambia kijana wangu jiulize haya maswali kwanza;
  1. Je Tundu Lisu si mgonjwa zaidi ya mwaka? mbona yeye hatajwi? je si Tundu Lissu ndiye alisema bado hajapata ruhusa toka kwa daktari wake akimjibu spika ndugai?
  2. Hivi unajua malkia Elizabeth katawala uingereza toka mwaka 1952?
  3. Unakumbuka kuwa katiba ya pendekezwa ya Jaji Warioba ilipendekeza kuwa mbunge akiugua miezi sita mfululizo aachishwe na Tundu Lissu anaiunga mkono? unakumbuka JK alipojaribu kushauri kuwa ''hii itasababisha wabunge waende majimboni na dripu'' Tundu Lissu walimtukana huku wakimbeza kwa maradhi Mh.JK aliyokuwa akiugua (tezi dume)?
  4. Unakumbuka Tundu Lissu ndiye alikuwa kinara kupinga wajumbe wa Tume ya Warioba wasilipiwe bima ya afya?
Nilihitimisha kwa kusema muda unaenda kasi sana.
 
Tuweke siasa za majitaka pembeni. Naomba niambie ni kwa namna gani sanaa na utamaduni unachangia pato la Taifa na namna ambavyo sera zenu zinawawezesha wasanii kunufaika na kazi yao na hatimaye kuwa kiwanda chenye manufaa makubwa kwa msanii mmoja mmoja,makundi na Taifa kwa ujumla.
Kuisema CHADEMA na wapinzani kila dakika hauwatendei haki wale uliopewa uwaongoze.
 
Mleta mada una hoja dhaifu Sana .

Hivi tangu 1952 mpaka sasa hivi wamepita mawaziri wakuu wangapi hapo Uingereza. Unaleta hoja huku ukiwa haufahamu kuwa mtendaji mkuu wa shughuli za kiserikali pale uingereza sio huyo Malikia.

Lisu alitoa wazo likakataliwa ila sidhani kama ingekuwa sehemu ya katiba yetu kama ilivyopendekezwa na rasimu ile ya Warioba angeenda kuipinga mahakamani.

Wakati mwingine haihitaji kutumia hadubini ili kujua kuwa hii ni mimba na hiki ni kitambi.
 
Tuweke siasa za majitaka pembeni. Naomba niambie ni kwa namna gani sanaa na utamaduni unachangia pato la Taifa na namna ambavyo sera zenu zinawawezesha wasanii kunufaika na kazi yao na hatimaye kuwa kiwanda chenye manufaa makubwa kwa msanii mmoja mmoja,makundi na Taifa kwa ujumla.
Kuisema CHADEMA na wapinzani kila dakika hauwatendei haki wale uliopewa uwaongoze.
Nje ya mada hili ni jukwaa la siasa
 
Ukitaka kujua UKILAZA wa mtu we mpe uwanja tu wa kujieleza. Wewe kichwa tupu, Malkia Elizabeth sio Head of British Government/ Executive. Serikali ya Uingereza inaongozwa na WAZIRI MKUU na kamwe haijawahi kuhodhiwa. Mimi tangu nipate akili nimewajua mawaziri wakuu kadhaa,
James Callaghan
Margareth Thatcher
Sir John Major
Tony Blair
David Cameron
Gordon Brown
Theresa May na sasa Borris Johnson. Unaweza kuniambia ni lini Malkia Elizabeth alitawala Uingereza? Kuna siku ulishasikia jambo fulani la kiserikali linasubiri uamuzi wa malkia?
 
Back
Top Bottom