Ncha Kali
JF-Expert Member
- Sep 19, 2019
- 14,515
- 27,006
Rejea tena kichwa cha mada hapo juu.
Muda unakimbia kwa kasi na mengi yanatokea na kupita, kumbukumbu huwa zinabaki.
Huenda sina kumbukumbu za kutosha, lakini kwa kadri ya 'hansadi' zangu sikumbuki mtu aliyewahi kuteuliwa kwenye ulaji na akagoma ili kulinda kile kinachoitwa msimamo wa chama.
Kama yupo/wapo basi tukumbushane, na pia tuhusianishe sababu zao kugomea uteuzi na mazingira halisi ya nyakati zao.
Ninaowakumbuka mimi ni wale waliokuwa mstari wa mbele, lakini ghafla wamekuwa watiifu na wachapakazi kweli kweli.
Mifano ipo mingi, sina haja kuitaja hapa labda ikihitajika.
Sasa basi, mara paap Rais JPM akaamua kuwajumuisha kwenye serikali yake hawa watu ambao leo wanaonekana mwiba na mahiri kuwashambulia wabunge walioapishwa.
Ni nani atagoma?
Hakuna asiyeijua njaa ilivyo kali huku nchi kavu, nguvu ya mamba ni maji. Sio Halima pekee mwenye njaa au hicho kinachoitwa tamaa, pengine tunawaonea wivu kwamba ni ganda la ndizi.
Yule mtu angeweza kususia uteuzi na awe wa kwanza kuwanyooshea kidole hawa wabunge.
Ncha kali.
Muda unakimbia kwa kasi na mengi yanatokea na kupita, kumbukumbu huwa zinabaki.
Huenda sina kumbukumbu za kutosha, lakini kwa kadri ya 'hansadi' zangu sikumbuki mtu aliyewahi kuteuliwa kwenye ulaji na akagoma ili kulinda kile kinachoitwa msimamo wa chama.
Kama yupo/wapo basi tukumbushane, na pia tuhusianishe sababu zao kugomea uteuzi na mazingira halisi ya nyakati zao.
Ninaowakumbuka mimi ni wale waliokuwa mstari wa mbele, lakini ghafla wamekuwa watiifu na wachapakazi kweli kweli.
Mifano ipo mingi, sina haja kuitaja hapa labda ikihitajika.
Sasa basi, mara paap Rais JPM akaamua kuwajumuisha kwenye serikali yake hawa watu ambao leo wanaonekana mwiba na mahiri kuwashambulia wabunge walioapishwa.
Ni nani atagoma?
Hakuna asiyeijua njaa ilivyo kali huku nchi kavu, nguvu ya mamba ni maji. Sio Halima pekee mwenye njaa au hicho kinachoitwa tamaa, pengine tunawaonea wivu kwamba ni ganda la ndizi.
Yule mtu angeweza kususia uteuzi na awe wa kwanza kuwanyooshea kidole hawa wabunge.
Ncha kali.