K_lynn asema anamkumbuka sana mumewe

K_lynn asema anamkumbuka sana mumewe

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2017
Posts
1,605
Reaction score
1,957
Jumatano wiki hii ilikuwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa ya tajiri maarufu nchini Tanzania Reginald Mengi. Hata hivyo, tajiri huyo huyo alifariki wiki nne kabla jijini Dubai, Falme za Kiarabu.
Katika kuadhimisha siku hiyo ya kuzaliwa kwake, mkewe Bi Jacqueline Mengi ametumia mtandao wake wa kijamii wa twitter kumuomboleza mumewe na kusema kuwa yeye na watoto wao wanamkumbuka sana.
Mapenzi baina ya Mengi na mkewe yalishamiri katika siku za mwishoni za mzee Mengi, na walikuwa ni moja ya wapenzi maarufu mitandaoni kutokea Tanzania mpaka nchi jirani ya Kenya.
"Leo (Jumatano) tungelikuwa tukikusherehekea. Nikifumba macho yangu naona namna ambavyo ungetabasamau wakati tukikuimbia mwimbo wa kushereheakea kuzaliwa kwako. Hakuna maneno yanayojitosheleza kueleza jinsi gani mimi na watoto tunavyokukumbuka, tukiamka kila siku bila wewe. Heri ya siku ya kuzaliwa mpenzi wangu wa ukweli, milele mioyoni mwetu."
Ruka ujumbe wa Twitter wa @JNtuyabaliwe
Today we would have been celebrating you,if I close my eyes I can see how you would have smiled when we sing happy birthday to you. There are no words to describe how much I and the kids miss you,waking up each day without you.Happy birthday my true love,forever in our hearts. pic.twitter.com/rGBOSy56gf
— Jacqueline N Mengi (@JNtuyabaliwe) 29 Mei 2019
Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @JNtuyabaliwe
Ujumbe huo ndio ulikuwa wa kwanza kwa Bi Mengi maarufu kwa jina lake la kisanii kama K-Lynn kuchapisha mtandaoni toka alipofiwa na mumewe mwanzoni mwa Mwezi huu.
Wawili hao walifunga ndoa mwaka 2015 na mwezi Machi mwaka huu waliadhimisha miaka minne ya ndoa yao.
 
Back
Top Bottom