Jux ameachia Ngoma mpya baada ya kimya kirefu

Jux ameachia Ngoma mpya baada ya kimya kirefu

Kadhakan

Senior Member
Joined
Jul 20, 2026
Posts
115
Reaction score
176
Msanii wa muziki kutoka Tanzania, Juma Mkambala maarufu kama Jux, (@juma_jux ) ameachia wimbo mpya unaoitwa “Sexy & Bad” ambao amemshirikisha Staa wa muziki kutoka Ghana, Stonebwoy (@stonebwoy )

Wimbo huo umetoka siku chache baada ya Jux kuibua gumzo kwenye mitandao ya Kijamii kutokana na mabadiliko ya mwonekano wake, ambapo mashabiki wameendelea kumjadili baada ya kuonekana amepungua uzito.

Soma pia: PostGE2025 Jux ashusha ngoma zake mpya alizoziachia hivi karibuni baada ya Gen z kuacha kusupport wasanii machawa

Akizungumzia mwonekano wake mpya, Jux aliambatanisha picha zake na ujumbe uliosomeka, “Sex, bad, confident, proud the mission was simple, look sex and bad, we understood the assignment,” akieleza kwa ufupi kuhusu dhana ya mwonekano wake mpya unaolenga kujiamini, kuvutia na kuonekana mwenye hadhi.

Kwa sasa, Mashabiki wa muziki wanaweza kusikiliza na kutazama “Bad & Sex” kupitia majukwaa mbalimbali ya muziki ya kidijitali ya Jux.


 
Back
Top Bottom