Msee Lekasio
Member
- Mar 25, 2010
- 73
- 8
Nduku sanguni lidhe jambasi bado linatesa!!! Hii habari ni ya gaseti la mwananji
JESHI la PoIisi mkoani Arusha linamshikilia mfanyabiashara maarufu wa madini mkoani hapa, Justin Nyari kwa tuhuma za wizi wa madini ya Tanzanite pamoja na mamilioni ya fedha za kigeni.
Taarifa zilizothibitishwa na kamanda wa polisi mkoani Arusha, Matei Basilio zinasema kuwa Nyari alikuwa akisakwa na polisi tangu juzi na kukamatwa jana na kwamba mpaka saa 8:00 mchana Nyari alikuwa akihojiwa.
Kamanda Matei alisema kuwa wanamshikilia mfanyabiashara huyo na kumuhoji kutokana na tukio lililofanyika mapema mwezi Aprili mwaka huu wakati madini yenye thamani ya Sh36 milioni yalipoibwa pamoja na dola 42,000 za Kimarekani (sawa na Sh54.6 milioni za Kitanzania).
Inadaiwa kuwa fedha na madini ziliporwa kutoka kampuni moja inayojishughulisha na ununuzi na uuzaji wa madini aina ya Tanzanite iliyo mjini hapa na wahusika hawakuweza kufahamika kwa wakati huo.
Jeshi hilo lilidaiwa kuwa tangu kutokea kwa wizi huo, upelelezi umekuwa ukifanyika na watu watano walikamatwa na kuhojiwa na kwamba baadaye ilibainika kuwepo umuhimu wa kumuhoji mfanyabiashara huyo.
Kamanda Matei alisema kuwa ni kweli jeshi hilo lilipata taarifa juu ya mfanyabiashara huyo kuhusishwa na tuhuma hizo hivyo walimtafuta na kumpata na baadaye kumuhoji ili kujua kama kuna kosa la kujibu.
"Ni kweli yupo hapa... muda huu anahojiwa na mkuu wa upelelezi na suala la kuendelea kumshikilia ama kumwachia litategemea na uzito wa tuhuma zinazomkabili," alisema Kamanda Matei.
Mfanyabiashara huyo amekumbwa na tukio hilo wakati akitajwa kuwa miongoni mwa watu wanaotaka kuwania kiti cha udiwani wa Kata ya Mererani mkoani Manyara kwa tiketi ya CCM.
JESHI la PoIisi mkoani Arusha linamshikilia mfanyabiashara maarufu wa madini mkoani hapa, Justin Nyari kwa tuhuma za wizi wa madini ya Tanzanite pamoja na mamilioni ya fedha za kigeni.
Taarifa zilizothibitishwa na kamanda wa polisi mkoani Arusha, Matei Basilio zinasema kuwa Nyari alikuwa akisakwa na polisi tangu juzi na kukamatwa jana na kwamba mpaka saa 8:00 mchana Nyari alikuwa akihojiwa.
Kamanda Matei alisema kuwa wanamshikilia mfanyabiashara huyo na kumuhoji kutokana na tukio lililofanyika mapema mwezi Aprili mwaka huu wakati madini yenye thamani ya Sh36 milioni yalipoibwa pamoja na dola 42,000 za Kimarekani (sawa na Sh54.6 milioni za Kitanzania).
Inadaiwa kuwa fedha na madini ziliporwa kutoka kampuni moja inayojishughulisha na ununuzi na uuzaji wa madini aina ya Tanzanite iliyo mjini hapa na wahusika hawakuweza kufahamika kwa wakati huo.
Jeshi hilo lilidaiwa kuwa tangu kutokea kwa wizi huo, upelelezi umekuwa ukifanyika na watu watano walikamatwa na kuhojiwa na kwamba baadaye ilibainika kuwepo umuhimu wa kumuhoji mfanyabiashara huyo.
Kamanda Matei alisema kuwa ni kweli jeshi hilo lilipata taarifa juu ya mfanyabiashara huyo kuhusishwa na tuhuma hizo hivyo walimtafuta na kumpata na baadaye kumuhoji ili kujua kama kuna kosa la kujibu.
"Ni kweli yupo hapa... muda huu anahojiwa na mkuu wa upelelezi na suala la kuendelea kumshikilia ama kumwachia litategemea na uzito wa tuhuma zinazomkabili," alisema Kamanda Matei.
Mfanyabiashara huyo amekumbwa na tukio hilo wakati akitajwa kuwa miongoni mwa watu wanaotaka kuwania kiti cha udiwani wa Kata ya Mererani mkoani Manyara kwa tiketi ya CCM.