Just stay away from me girl

Just stay away from me girl

Kuveta

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2014
Posts
1,154
Reaction score
636
Hali zenu waungwana wenzangu.

Kama kawaida mi huwa naleta thread za mambo yanayohusu maisha yangu ya kila siku ili mnisaidie ushauri. Nlipokuwa bongo nlikuwa na girl friand wangu aliekuwa anaitwa Martha.Huyu msichana tulishibana sana na hasa ukizingatia mi ndo kumtoa bikra, kwahiyo alinipenda vilivyo na mimi nilimpenda pia kadri niwezavyo.

Basi baada ya hali ya maisha bongo kuwa fucked up ikabidi nikatafuta njia na kufanikiwa kuingia kwa weupe queen Elizabeth land.Ila kabla ya kuondoka tukawa tushapanga kuwa endapo naondoka ila yeye ndio atakuwa mke wangu, na yeye akaniahidi kuwa endapo naondoka ila atanivumilia ili aje kuwa mke wangu.

Basi bwana baada ya kufika kwa weupe tukawa tunawasiliana sana.Tunapeana moyo, mara siku kadhaa za mbele mawasiliana yakaanza kupungua nikimuuliza sababu ananilisha polojo tu, simu ilikuwa mbovu,
mambo yake nilienda kwa ma mdogo nikasahau simu nyumbani.

Alafu kilichoniuma zaidi nlikuwa namtumia ela za kufanyia huku nkijiandaa kuleta mahari. Baada ýa siku kadhaa nkapata taarifa km dem ashajazwa na mjinga flan toka South afrika.

Mwanzo nlipomuuliza dem alipinga mwishoni akaja kukubali basi tukaachana nkampotezea. Akaendelea na msouth wake mara msouth akaingia gizani na kumwacha kwenye mataa.Msichana akalea mimba adi akajifungua na kuntumia picha ya mwanae, nikampongeza kwa kuzaa na tukawa kama marafiki wa kawaida tu.

Sasa kila siku zinavyozidi kwenda mwenzangu anazidi kujisogeza kwangu tena mara aombe msamaha ata kama sijamuuliza swala hilo mara aonekane kujuta ila mimi sikuwa na mpango wa kurudiana nae tena, kuna kipindi alikuwa anaenda hadi nyumbani kuwasaidia wazee wangu kazi.

Hadi wazee nikawasafirisha akakosa njia nyingine ya kunibembeleza ila akawa ananambia atafanya juu chini hadi turudiane, nikamwambia hiyo ni ndoto anayoota mtu anaetembea mchana kweupe. Sasa mimi nina fiance wangu ambae natarajia kufunga nae ndoa huku na nshamwambia.

Cha kushangaza juzi kanitumia message eti ameshasikia kuwa kweli mi nataka kuowa huku na kwamba mi nikishaowa huku ndo itakuwa mwisho wetu mi na yeye na pengine ata Afrika sitorudi tena, kwahiyo bora yeyeajiuwe na mimi ili asiendelee kuteseka ajili yangu.

Mi nikamjibu we ukitaka kujiuwa jiuwe ila mimi sihusiki na kifo chako maana sijakuchangia ata sh 5 ya kununua sumu kwahiyo kifo hicho kitakuhusisha mwenyewe na shetani wako.Toka nimjibu hivo haja reply na mimi sihitaji kujua kinachoendelea kwake.

Nyinyi wana maoni wenzangu mnasemaje kuhusu uamuzi wangu na majibu nliyompa yanafaanimefanya kosa kumjibu hivyo.Karibuni tumjadili huyu mpenzi wangu wa zamani.
 
Duh! Mkuu mbona unamuita mpuuzi/marehemu mtarajiwa?

Hata kama ana makosa lakini u should have mercy on her. Msaheme lakini kama huwez kurudiana nae usimnyanyase. She will live with it. Just the matter of time.
 
ndo maajabu ya baadh ya akina dada hayo. Huwa wajichanganya tu then wanakuja kujutia milele. Btw nadhan hajajiua ameamua awe mpole aone next move utakayofanya. Ukikaa kimya inawezekana akakutafuta tena so jiandae kwa hlo.
 
Duh! Mkuu mbona unamuita mpuuzi/marehemu mtarajiwa?

Hata kama ana makosa lakini u should have mercy on her. Msaheme lakini kama huwez kurudiana nae usimnyanyase. She will live with it. Just the matter of time.

Samahani labda mimi mgumu kuelewa, sijasoma sehemu ya manyanyaso hapo labda nieleweshe wapi amemnyanyasa?
 
Tukushaur Nin Na Unategemea Kufunga Ndoa? Mludie Martha
 
Yani hata usigeuke. Mimi nilizaa nae na mtoto nikabeba, yani hata akifa siendi.
 
Duh! Mkuu mbona unamuita mpuuzi/marehemu mtarajiwa?

Hata kama ana makosa lakini u should have mercy on her. Msaheme lakini kama huwez kurudiana nae usimnyanyase. She will live with it. Just the matter of time.

Sikumnyanyasa mkuu, isipokuwa yy mwenyewe ndio kaamua kujinyanyasa kwa kutembea na m2 ambae hakuwa anamjua vzr. Matokeo yake kamdunga zigo na kutokomea kusikojulikana. Na kuhusu kumsamehe mbona msamaha wa kawaida nshaufanya na tukawa marafiki sasa hili swala la kutaka tena kuniingilia ktk maisha yangu ya ndoa linatoka wap? Yeye kafanya yake nikamlaum yakaisha, na mm aniachie nifanye yangu alaumu yaishe, lkn c kunipiga mkwala wa kifo ili niachane na anaenipenda kweli na kurudiana na huyu mpuuzi. I could never allowed her 2 spoil my future, coz she alrd spoil her own. That's y I need her 2 stay away frm me. But thanx 4 ur advice bingwa!
 
alivyoenda kwa msouth HAKUDHANI NAWEWE UNGEJIUA!!?? labda.. bob hizo mbinu zake tu mkazie.. nani alimwambia atoe mkojo kwa msouth
 
Hata ujafanya kosa kwa hayo majibu mbona tena n malaini tu ungempa magumu zaidiii ilii akafe kwelii yaani hawa wanawakee hawaa cjui watafunguka Lin akilii na ahadi zote bado hakuridhika piga chin mkuu
 
Huwa nawahurumia sana wadada ambao wametelekezwa na jamaa zao baada ya kuzaa nao. Wanaonekana kama rejects vile, it's like they don't have right to love and be loved....!
 
Sikumnyanyasa mkuu, isipokuwa yy mwenyewe ndio kaamua kujinyanyasa kwa kutembea na m2 ambae hakuwa anamjua vzr. Matokeo yake kamdunga zigo na kutokomea kusikojulikana. Na kuhusu kumsamehe mbona msamaha wa kawaida nshaufanya na tukawa marafiki sasa hili swala la kutaka tena kuniingilia ktk maisha yangu ya ndoa linatoka wap? Yeye kafanya yake nikamlaum yakaisha, na mm aniachie nifanye yangu alaumu yaishe, lkn c kunipiga mkwala wa kifo ili niachane na anaenipenda kweli na kurudiana na huyu mpuuzi. I could never allowed her 2 spoil my future, coz she alrd spoil her own. That's y I need her 2 stay away frm me. But thanx 4 ur advice bingwa!

Tenaa n mpuuziiii kabisa narudia n mpuuzii mshenzi mkubwaa mkuu tenaa ungemsaidia hiyoo hela ya kukununua sumu pumbavuu kabisaa
 
Back
Top Bottom