Jussa: Mchezo umeisha Bunge La Katiba

Jussa: Mchezo umeisha Bunge La Katiba

Jaman wazanzibari wenzangu kama kweli tunaipenda zanziba, tuandae maandamano makubwa ambayo hayajawahi kutokea zanzibar kwa ajili ya kuwapokea mashujaa wetu hawa akina salma saidi na wenzake.
Pia tuwaandalie usafiri wa ndege ikiwezekana kutoka dodoma hadi zanzibar, siku hiyo washajiishwe wazanzibari wote wenye uchungu na nchi yao kike kwa kiume wakubwa wadogo watoke majumbani mwao wajipange barabarani kuanzia uanja wa ndege hadi mjini kuwalaki mashujaa hao.
Ndugu zangu wazanzibari tusipofanya hivyo tutakua hatukuwatendea haki wapiganaji hawa, na tutakua wanafiq kujidai kuwa tuaipigania zanzibar kumbe ni waongo kama vile mibunge ya ccm kjidai yanaipigainia zanzibar ilipofika dodoma ikatusaliti kwa vijisenti.
Nduguzangu wenzetu wameonesha kwa vutendo na sisi tuwaunge mkono, ushindi uko mikononi mwetu.
ZANZBAAAAAAA!!!!!!!!!!!!!!
 
Katiba Mpya bila Sitta inawezekana, Katiba mpya bila maridhiano haiwezekani............
 
Wameufyata sasa. Ukawa ndo habari ya mjini.
Ova
 
Eti anasema dua la kuku halimpati mwewe 6 unataka we mwewe likupate mara ngapi?
 
Sichangii mada mpk nione kile kibom, a.k.a kimemo

mkuu kibomu ninacho kwenye facebook ngoja kesho nikiwasha pc yangu nitakuwekea hapa ukisome. unafiki wa magamba umefika tamati.
 
Kilaza DR. MICHAEL FRANCIS----NDIYO
Kilaza DR. SUZAN KOLIMBA---------NDIYO
 
Jaman wazanzibari wenzangu kama kweli tunaipenda zanziba, tuandae maandamano makubwa ambayo hayajawahi kutokea zanzibar kwa ajili ya kuwapokea mashujaa wetu hawa akina salma saidi na wenzake.
Pia tuwaandalie usafiri wa ndege ikiwezekana kutoka dodoma hadi zanzibar, siku hiyo washajiishwe wazanzibari wote wenye uchungu na nchi yao kike kwa kiume wakubwa wadogo watoke majumbani mwao wajipange barabarani kuanzia uanja wa ndege hadi mjini kuwalaki mashujaa hao.
Ndugu zangu wazanzibari tusipofanya hivyo tutakua hatukuwatendea haki wapiganaji hawa, na tutakua wanafiq kujidai kuwa tuaipigania zanzibar kumbe ni waongo kama vile mibunge ya ccm kjidai yanaipigainia zanzibar ilipofika dodoma ikatusaliti kwa vijisenti.
Nduguzangu wenzetu wameonesha kwa vutendo na sisi tuwaunge mkono, ushindi uko mikononi mwetu.
ZANZBAAAAAAA!!!!!!!!!!!!!!

Mimi ni Tanganyika ila kwa hili najitolea kuungana na wazanzibar hawa kuwapongeza wamejitolea kutukomboa naomba nipate picha zao na majina yao niyabandike nyumbani kwangu hii itakuwa history yangu wanangu wajukuu wangu na vitukuu vyangu mungu ibariki kansa-nia
 
Kwa maccm usishangae kusikia akidi ya theluthi 2 imetimia kila upande wa muungano! Maana hawa wamezoea uchakachuaji!
 
Zanzibar kwanza.

Anamaanisha GAME OVER muheshimiwa Sitaunawaona hawa mbona wana tangaza nje ya bunge si walikuwemo humuhumu ,naomba tuwachukulie hatua mara moja ,sina zaidi ila mheshimiwa zile kura za waliokwenda Hija bado hatujazihesabu ila kule kwenye fax karatasi zimekwama ,ni hayo tu Muheshimiwa.

We unataka kupingana na hesabu rahisi hii tukuiteje kama sio div 5? Shame on you
 
The game is over! -by ISMAIL JUSSA LADHU

Kwa mujibu wa Samuel Sitta alivyotangaza jana, jumla ya Wabunge wote wa Bunge la Katiba = 629
Tanganyika = 419
Zanzibar = 210
2/3 ya 210 = 140
1/3 ya 210 = 70
Kwa hesabu ndogo tu hapo ni kwamba kuinyima Rasimu ya Vijisenti theluthi mbili (2/3) ya Zanzibar zilitakiwa zaidi ya kura 70 (kwa maana zikipatikana 71 itakuwa hapana 2/3 ya Zanzibar).
Sasa naomba tuhesabu pamoja. Miongoni mwa wajumbe 210 wa Bunge la Katiba wanaotoka upande wa Zanzibar:
Wawakilishi wa CUF = 33
Wabunge wa CUF ZNZ = 25
Wabunge wa Chadema ZNZ = 4
Wana UKAWA walotoka ZNZ miongoni mwa 67 = 5
Walopiga wazi HAPANA jana = 7
Wajumbe wawili (Mwanasheria Mkuu wa SMZ Othman Masoud na mjumbe Abdalla Abbas) hawakupiga kura = 2
Jumla = 76
Kuinyima two thirds ya Zanzibar ilitakiwa anything above 70 out of 210.
Hapa pana 76
Kwa lugha rahisi kufahamika ni kwamba Katiba inayopendekezwa haitopita maana haikupata theluthi mbili ya Zanzibar.
Hapa hatujui matokeo ya kura zilizopigwa SIRI. Pia wapo wale waliotajwa kwamba wameorodheshwa watapiga kura wakiwa nje ya Bunge Maalum. Lakini hata ukichukulia zote zitakuwa NDIO basi haziwezi kubadilisha uhalisi na ukweli wa kitakwimu uliopo hapo juu.
Kwa kifupi ni kwamba theluthi mbili ya kura za Wajumbe wote wa Bunge la Katiba wanaotoka Zanzibar HAIPO.
Sijui wale waliolazimisha kuendelea na Bunge Maalum la Katiba bila ya kupata maridhiano ya pamoja na wakapelekea kutumika mabilioni ya fedha za walipa kodi masikini wa Tanzania huku wakijua kwamba hawatopata theluthi mbili ya kura za Wabunge wote wa Zanzibar sasa watasemaje?

Source: MF

Hapa lazima tunyonge watu kwa Ubadhirifu wa Mali ya UMMA.
 
Back
Top Bottom