propagandist
Member
- Aug 12, 2011
- 93
- 9
Naibu katibu mkuu wa zanzibar Ismail jussa Ladhu ameongoza timu ya mawaziri na wabunge wa CUF kuelekea Igunga kwa ajili kuongeza nguvu za kampeni za chama hicho, akiongea kaimu katibu mkuu Julius mtatiro amesema tokea uzinduzi wa kampeni uliozinduliwa na Prof Lipumba tarehe 13.09.2011 chama hicho kimekuwa kikifanya mikutano 36 tukiwa na timu 6 za kampeni, kuanzia leo tutakuwa tukifanya mikutano 45 kwa siku, kwa kweli tumeisha shinda tunasubiri kulinda kura kwa sababu mgombea wetu anakubalika amezaliwa hapa, amesoma hapa, na amefanya kazi hapa alisema mtatiro kuwaambia waandishi wa habari mjini Igunga. Gazeti la mwanainchi. 21.09.2011.