Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Jumuiya ya Madola imeipokea na kukubali dhamira ya Serikali ya Tanzania juu ya kupokea na kuwezesha ziara pamoja na kazi za Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo Dkt. Lazarus Chakwera ambaye pamoja na msafara wake utachunguza uminywaji wa kidemokrasia na kutofuatwa kwa utawala wa kisheria kufuatia matukio ya kabla na baada ya uchaguzi mkuu wa 2025.
Hayo yamesemwa baada ya kikao cha 72 cha Kamati Maalum ya Jumuiya ya Madola inayoshughulikia masuala ya demokrasia, utawala bora, na haki za binadamu miongoni mwa nchi wanachama(CMAG) ambapo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum) Professa Palamagamba Kabudi alikutana na kamati hiyo na kufanya mazungumzo.
Taarifa ya CMAG iliyotolewa baada ya kikao chake cha Machi 7, 2026 imesema “CMAG pia ilikaribisha dhamira ya Tanzania ya kumpokea na kuwezesha ziara pamoja na kazi za Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu mwezi Machi 2026.”
Disemba 2025 katika mkutano wake wa 71 wa CMAG ulioongozwa na Dkt. Ian Borg Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje na Utalii wa Malta uliamua kuiweka Tanzania katika ajenda maalum ya kikao cha machi yakizingatiwa masharti manne yaliyotolewa katika kikao kilichoijadili Tanzania Disemba 2025.
Tanzania ilitakiwa kutoa nafasi iliyokamilika bila kikwazo kwa Msafara Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola kuweza kukutana na wadau wote katika nafasi za mwanzo. Pia kuondolewa kwa vikwazo kwenye uhuru wa kukusanyika na kujieleza, makundi maalum na vyombo vya habari.
Pamoja na hayo masharti mengine ni Kufanyika kwa jukwaa la mashauriano kati ya vyama vya siasa ili kukubaliana mfumo wa pamoja wa hatua za kuendelea mbele kuelekea uchaguzi ujao. Uchukuaji wa hatua za kisheria na kiutawala zilizo wazi ili kuwawajibisha wahusika wa vitendo vya vurugu na athari zake, pamoja na kutoa fidia kwa waathirika pale inapofaa.
Ujumbe huo utakaoongozwa na Dkt. Lazarus Chakwera Rais Mstaafu wa Malawi unatarajiwa kufika nchini mwezi huu wa tatu huku miongoni mwa hadidu za rejea itakazotumia ikiwa ni taarifa ya Tume Huru ya Uchunguzi wa matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi ambayo imeundwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Pia Soma: Jumuiya ya Madola (Commonwealth) yasikitishwa na yanayoendelea Tanzania
Hayo yamesemwa baada ya kikao cha 72 cha Kamati Maalum ya Jumuiya ya Madola inayoshughulikia masuala ya demokrasia, utawala bora, na haki za binadamu miongoni mwa nchi wanachama(CMAG) ambapo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum) Professa Palamagamba Kabudi alikutana na kamati hiyo na kufanya mazungumzo.
Taarifa ya CMAG iliyotolewa baada ya kikao chake cha Machi 7, 2026 imesema “CMAG pia ilikaribisha dhamira ya Tanzania ya kumpokea na kuwezesha ziara pamoja na kazi za Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu mwezi Machi 2026.”
Disemba 2025 katika mkutano wake wa 71 wa CMAG ulioongozwa na Dkt. Ian Borg Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje na Utalii wa Malta uliamua kuiweka Tanzania katika ajenda maalum ya kikao cha machi yakizingatiwa masharti manne yaliyotolewa katika kikao kilichoijadili Tanzania Disemba 2025.
Tanzania ilitakiwa kutoa nafasi iliyokamilika bila kikwazo kwa Msafara Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola kuweza kukutana na wadau wote katika nafasi za mwanzo. Pia kuondolewa kwa vikwazo kwenye uhuru wa kukusanyika na kujieleza, makundi maalum na vyombo vya habari.
Pamoja na hayo masharti mengine ni Kufanyika kwa jukwaa la mashauriano kati ya vyama vya siasa ili kukubaliana mfumo wa pamoja wa hatua za kuendelea mbele kuelekea uchaguzi ujao. Uchukuaji wa hatua za kisheria na kiutawala zilizo wazi ili kuwawajibisha wahusika wa vitendo vya vurugu na athari zake, pamoja na kutoa fidia kwa waathirika pale inapofaa.
Ujumbe huo utakaoongozwa na Dkt. Lazarus Chakwera Rais Mstaafu wa Malawi unatarajiwa kufika nchini mwezi huu wa tatu huku miongoni mwa hadidu za rejea itakazotumia ikiwa ni taarifa ya Tume Huru ya Uchunguzi wa matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi ambayo imeundwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Pia Soma: Jumuiya ya Madola (Commonwealth) yasikitishwa na yanayoendelea Tanzania