Juma Duni mgombea mwenza UKAWA yuko wapi?

Juma Duni mgombea mwenza UKAWA yuko wapi?

Umslopagazi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2013
Posts
1,737
Reaction score
935
Nauliza tu maana sijamsikia kitambo sasa na kampeni zinayoyoma.

Jibu kwa hekima.


JUMA DUNI KAPOTELEA WAPI?

Mgombea mwenza Ukawa Babu Duni amekata tamaa kabisa ya kutoendelea na mikutano ya kampeni kutokana na zomeazomea kuendelea kuikabili Ukawa.

Hata hivo kuna uwezekano Babu Duni akawa amesoma upepo mapema hivo kuamua kijiondoa ili kupunguza upotevu wa gharama.

Mbali na hivyo kwa taarifa za ndani kutoka CUF inasemekana anatakiwa arudi CUF kwasababu Ukawa wamekiuka makubaliano yaliyoafikiwa juu ya usawa wa vyama shiriki ukawa hivyo anatakiwa kujiondoa haraka Chadema arudi CUF na huo ndio utakua mwisho wa Ukawa

========================

Updates; 01 Oct 2015


Mgombea mwenza wa urais wa tanzania kupitia chama cha demokrasia na maendeleo ( CHADEMA ),anayeungwa mkono na vyama washirika vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi ( UKAWA ),Mh.Juma Duni Haji amesema kuwa mji wa utete wilayani rufiji ambao ulianzishwa mwaka 1899, zaidi ya karne moja iliyopita haukupaswa kudumaa kimaendeleo kutokana na kuwa na bonde la mto rufiji lenye rutuba kwa kilimo,pori la akiba la Serou pamoja na maporomoko ya maji ambayo yangetumika kuzalisha umeme.

Mh. Juma Duni Haji amehutubia mkutano wa hadhara wa kampeni katika mji wa Utete na kueleza kusikitishwa kwake na hali ya maendeleo ilivyo kwa kipindi cha miaka 53 tangu nchi ipate uhuru toka kwa wakoloni wa kiingereza.

Aidha, mgombea mwenza huyo wa Chadema akiongea kwa uchungu mkubwa amewahakikishia huduma bora za kujifungua akinamama wajawazito ambao wamekuwa wakipoteza maisha yao njiani wakati wakivuka mto rufiji kwenda kujifungua katika vituo vya afya na zahanati.

John Guninita,miaka 25 iliyopita aliwahi kuhudumu kama mkuu wa wilaya ya rufiji anaeleza hali ilivyokuwa wakati huo na sasa,huku makamu mwenyekiti wa chadema taifa kutoka Zanzibar Said Issa Mohammed akihoji kitendo cha uongozi wa serikali wilayani humo kuzuia madawati zaidi ya 100 yaliyotengenezwa kwa maelekezo ya waziri mkuu mstaafu Mh.Edward Lowassa yasitumiwe na wanafunzi wanaoendelea kukaa chini sakafuni.
 
Last edited by a moderator:
Jana alikuwepo Mbagala Zhakem mkuu,alianza kuzungumza Mbatia,Duni,Sumaye,Mbowe Lowasa akamalizia mkuu.
 
Naona kama ana wasiwasi na maamuzi yake anaonekana kimagumashi!
 
nafkiri leo alikuwa kigamboni mkuu
 
Amejiondoa maana amejipima ameona hafai, ubalozi wa nyumba 10 eti ndo unamfaa
 
Zomeazomea inayoendelea kuwakumba viongozi wandamizi wa UKAWA, mgombea mwenza wake Juma Duni ameonekana kukata tamaa ghafla kutokana na kile anachofanyiwa yeye na wafuasi wa CHADEMA wanaojiita wazalendo wa CHADEMA.
 
Hana jipya huyo. Aende kwa waganga wao wa kienyeji wakawasaidie kama ilivyo kawaida ya CCM
 
Babu Duni atajuta kukurupukia pesa za Lowassa...na CUF wamesema hawatamkubali
 
Ccm mwaka ndo wamekuwa kama wapinzabi angalia hata mada wanazoanzisha ni za kiupinzani zaidi
 
muheshima Juma popote ulipo njo uendelea na kampeni tumeshawaambia wananchi waache zomea zome zao njo uendee bana na kampeni maana siku zenyewe zinakwisha, mbona mama azomewi!!
 
Back
Top Bottom