Jukwaa la Wahariri(TEF), lataka majeruhi ajali ya moto Morogoro washitakiwe

Nasikia kuna ajali.nyingine ya lori la mafuta Kilimanjaro, raia wametimuliwa na polisi
 
Ili liwe fundisho hata kwa ajali zingine za barabarani maana huo ni wizi kama wizi mwingine ule.

Ikibidi watiwe bangili humo humo wodini.

Naungana na TEF.
 
Balile anajipendekeza, bila shaka anatafuta uteuzi. Kwa umaskini wa watanzania uliopo ktk awamu hii alitegemea wananchi wafanye nn?

Ama kweli mwenye shibe hamjui mwenye njaa!
Leo lori la mafuta,kesho utapinduka na bus badala ya kusaidia watakuja kukuibia na kukuacha ufe.
 
Sasa utajuaje aliyejeruhiwa alienda kuiba mafuta na hakuenda kumsaidia dereva, au kwa udadisi wa kutaka kujua kilichotokea tu.

Are we about to blame the victim here?

Is this a case of keeping people poor, then when they scavenge out of sheer opportunism, instead of wondering what kind of person woyld do that, what are the moral, educational, economical concerns, we simply want to jail them?

To jail someone, one needs evidence beyond reasonable doubt. Simply being at the scene of an accident is hardly even probable cause.

Tutatengeneza mazingira ya watu kuogopa kusaidia wanaopatwa na ajali, kwa kuhofia kufungwa.
 
Nadhabi Balile hayuko sawa. Ni vema watu wakamweleza ukweli hadharani. Kibaya ni kwamba he is dragging the whole TEF into this shit!

Anaimomonyoa bila kujua, huku akijitukuza. He doesn't notice his weakness.

Heshima ya TEF imefia mikononi mwa Balile. No one takes it seriously anymore. Ni kwa sababu ya poor judgment za aina hii ambazo sasa zinavalishwa joho la TEF nzima!

TEF wenyewe wameona anavyocharazwa mitandaoni kuhusu kauli yake hii ya kutaka majeruhi wote washitakiwe lakini hakuna anayejitokeza kusimama naye. Unajua kwanini? Wanaona hicho asichoona yeye katika andiko LAKE. Wana aibu, ila hawataki kuonekana wanapingana naye majukwaani. Utatoane statement hii katikati ya maombolezo ya kitaifa? Majeruhi wote walikuwa ni wezi? Ndicho Balile anataka tuamini?

Hii ni andiko la Balile, typical of his pattern thinking - kipolisipolisi - lakini, kwa bahati mbaya sana, lina signature ya TEF! They are sinking with him!!!!
 
Jeshi la polisi wawe wanafanya mazoezi ya utayari kwa kutengeneza ajali kwenye miji tofauti tofauti hata kila baada ya muda fulani then wanatembeza kichapo cha mbwa koko.

Kusikia kwa kenge ni mpaka aone damu puani.
 
......nyie TEF, ni mapema sana kutoa kauli kama hizi.
Na msiishie tu katika kusema washitakiwe majeruhi, semeni pia na suala la kukosekana kwa vifaa vya kutosha vya zimamoto, madereva kutotoa nafasi ili ambulance ipite.

Umaskini (usifikirie ukosefu wa chakula na ajira tu, bali umaskini kwa maana ya kukosa taarifa muhimu kwa mtu mmoja mmoja na umma wote).

.....hili janga halitakuwa la mwisho na likitokea tena, watu wataenda 'kuokota' mafuta. Kama mkate hunapatikana kwa shida, wachache watatafuta makombo
Kuna mengi sana ya kusema ambayo ni ya wazi. Wamefanya uvivu wa kufikiri kuandika jambo linaloweza kuitwa "blaming the victim".

Hata hawakuuliza kwa nini mambo haya yanatokea Tanzania na si Uswizi?
 
We uko na majonzi gani saa hizi? Au umepoteza nini mpaka washtakiwe?
Una kipimo cha kupimia majonzi? Walichokuwa wanakifanya kilikuwa halali? Roho zilizopotea zilihitajika sana kwenye nyuvu kazi ya taifa! Majeruhi wanapaswa kuwajibishwa hata kama hawakujua kwamba walichokua wakikifanya ni uhalifu!
 
Kwa sababu wao ni watu wa habari and they nothing about volatile fuels kama petrol ndo maana kaongea hayo.

Kwa mliosikiliza live coverage ya TBC kuna mtu aliungua hadi kufa na alikuwepo eneo la tukio kwa lengo la kuwaokoa waliokuwa wamekwama kwenye cabin.

Anyway unapomshtaki mtu kikubwa ni ushahidi wala hamna kingine.
 
Pale ni njiani, kuna wapita njia, kuna walioenda kuona ajali, kuna walioenda kuokoa wapendwa wao n.k.
 
Una kipimo cha kupimia majonzi? Walichokuwa wanakifanya kilikuwa halali? Roho zilizopotea zilihitajika sana kwenye nyuvu kazi ya taifa! Majeruhi wanapaswa kuwajibishwa hata kama hawakujua kwamba walichokua wakikifanya ni uhalifu!
Vipi waliokuwa wanawaokoa waliokuwa ndani ya cabin? vp wapita njia?
 
vipi kuhusu majeruhi wapita njia ambao tukio la mlipuko limewakuta wakiwa njiani kuelekea kwenye mambo yao na sio wizi wa mafuta baada ya lorry kuanguka? Kutakua na namna ya kuwatambua kabla ya mashitaka?
 
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limeeleza kushtushwa na taarifa za vifo vya Watanzania zaidi ya 60 walioungua moto wakati wakichota mafuta kutoka katika lori lililopata ajali eneo la Msamvu, Morogoro, jana Agosti 10, 2019 likitaka waliojeruhia kushitakiwa watakapopona majeraha yao.

Taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana usiku Jumamosi na Kaimu Mwenyekiti Jukwaa hilo, Deodatus Balile ilisema vifo hivyo vimetokana na tabia mbaya iliyojengeka kwa baadhi ya watu kuchukulia ajali kama fursa ya kujipatia mali kwa njia haramu iliyoanza miaka ya hivi karibuni.

“Tumeshuhudia picha za watu waliofariki kwa kuungua moto zikirushwa kwenye mitandao ya kijamii kinyume cha maadili ya taaluma ya uandishi wa habari na upashanaji habari. Tunakemea tabia hii na kuitaka jamii iache mara moja tabia hii ya kinyama isiyo ya utu,” alisema Balile.

Balile pia alizungumzia watu zaidi ya 70 waliojeruhiwa katika ajali hiyo akisema wakipona wajiepushe na tabia hii ya uporaji.

“Ikilazimu, wote watakaopona katika ajali hii washitakiwe kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho kwao na wengine kuwa ikitokea ajali tunapaswa kusaidia majeruhi na kuokoa mali zao badala ya kupora,” alisema.

“Tunaomba viongozi wa dini, wazazi, viongozi wa kisiasa na jamii kwa ujumla itumie ajali hii kufundisha watoto na vijana maadili mema ya kuwa watu wa msaada mtu anapopata ajali kwa kusaidia majeruhi na kuokoa mali za waliopata ajali badala ya kuwapora,” aliongeza.

Hadi jana usiku, watu 64 walikuwa wameripotiwa kufariki huku 70 wakijeruhiwa ambapo baadhi ya majeruhi wamelazwa Hospitali ya Morogoro na wengine wakihamishiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.

Chanzo: Mwananchi
Huo ndoukweli tubadilike
 
Siyo majeruhi wote walienda kuiba mafutu wengine walikuwa wapita njia ,wengine walienda kutoa msaada , wengine walienda kushangaa tu nao ni miongoni mwa majeruhi.
 
Back
Top Bottom