Juhudi bila kuzingatia kanuni ni kujitesa tu

GRAMAA

JF-Expert Member
Nov 1, 2014
1,155
3,399
Juhudi bila ya kufuata sheria na kanuni za juhudi hizo ni kujitesa tu.

Vijana wengi wanapambana sana usiku na mchana kufanya Biashara mbalimbali ili wajikwamue kiuchumi ila waliowengi wanatoka patupu. Zaidi wanaambulia madeni mazito sana na kufilisiwa.

Jamani ndugu zanguni jitahidini mtoke kwenye huo usingizi mzito mliolala wa kuamini utafanikiwa kibiashara kwa bahati na juhudi binafsi.

Jamani eee biashara ni zaidi ya mtaji ulionao,ubora wa bidhaa ulionao au eneo zuri ulilofungua biashara hiyo.

Biashara ni roho yenye uhai hivyo basi ili unfanikiwe inabidi ujue na uzingatie sheria na kanuni za roho hai ya biashara.

Kama unafanya Biashara bila ya kujua hili basi ndugu yangu hutoboi ng'oooooo hata ufanye nini. Yaani hata uwe na frem kariakoo bila ya kufuata sheria za roho hai ya biashara huchomoki dogo.

Aisee hivi unajua kama biashara nayo inapenda,inachukia,inafurahi,inaumwa,inaiba,inalala,inapumzika,inatamaa,inamawazo n.k. Yaani naomba nieleweke sizungumzii mfanyabiashara ninazungumzia Biashara yenyewe.

Sasa ngoja nikusanue kidogo ili akili ikukae sawa. Wengi mmefungua biashara zenye roho zifuatazo ndio maana hamtoboi

i/ Biashara yenye roho ya chuki. Sifa ya biashara hii inakuwa inakuchukua sana wewe uliyeifungua. Kila ukipambana kuiweka sawa inagoma. Biashara haikupendi inakuchukia kinoma ila wewe unakaza tu bila kujielewa. Sanuka dogo unapoteza muda bure.

ii/ Biashara yenye roho ya wizi. Watu wengi sana humu mmefungua biashara zenye roho ya wizi ndiyo maana mnaibiwa sana mitaji yenu na biashara hizi. Kila ukiwekeza mtaji wako kwenye biashara, biashara inakuibia mtaji wote. Kazi yako inakuwa kila mara ni kuongeza mtaji kila siku. Daaah huruma sana.

iii/ Biashara yenye roho ya utasa. Biashara ina miaka kibao haizai. Wengi mnabiashara zenye roho ya utasa. Yaani kila ukipambana biashara haizai kabisa. Unashindwa kuelewa kuwa biashara yako ni tasa unaendelea kukomaa kizembe tu. Duuuuuh poleni sana.
.
iv/ Biashara yenye roho ya tamaa. Kijana kama Biashara yako inaroho ya tamaa huchomoki mzee. Biashara zenye roho ya tamaa ni mbaya sana na zinawafirisi wengi sana hapa duniani. Ukiona biashara inakumalizia hela na sio kukuingizia hela hiyo biashara inatamaa achana nayo haraka sana

v/ biashara yenye roho ya ukorofi na utovu wa nidhamu. Ukifungua biashara hii kila siku utakuwa unashinda kwa mwenyekiti wa mtaa au polisi kutatua kesi zinazosababishwa na biashara yako uliyoifungua. Mara gari yako ya biashara imegonga mtu,Mara ukuta wa mgahawa wako umedondokea wateja na mengine mengi. Hahahahaa balaa sana

vi/ Na mengine mengi

Sasa kutatua yote haya ni kazima urudi kwenye sheria za roho hai za biashara ambazo kwa bahati mbaya wanazifahamu watu wachache sana na zinabaki kuwa siri kwa watu wachache sana.

Sanuka wewe ili utoboe acha ujuaji.
 
Biashara=Akili+Busara+Nguvu za kiroho

Mleta mada umeongelea upande wa nguvu za kiroho. Ni kweli bila nguvu za koroho hutoboi. Wewe unafungua biashara hiyo hiyo na wengine kibao wanaifanya katika eneo hilo hilo! Kwanini waje kununua kwako wasiende kwa mwingine! Kama nyote mnatumia Akili + Busara sawa za kufanya hiyo biashara, basi atakayeuza ni yule anayetumia nguvu za Mungu aliye hai au yule anayetumia nguvu za shetani.
Kuhusu Akili ebu niongelee jambo moja kuhusu wauza mafuta ya kula kwenye chupa za kupima nusu lita, lita, lita mbili na kuendelea. Ukiwa unafanya biashara hii wewe ni mjasiriamali tu mwenye mtaji chini ya laki moja (100,000). Ukumbuke wateja wako wengi kiasi cha hela walichonacho ni buku (1,000). Inakuwaje unajaza mchupa ya buku mbili (2,000) unaacha robo lita ya buku (1,000)???. Unataka utajiri wa haraka?? Wateja wako unaowaendea ni masikini kwahiyo weka kipimo wanachokimudu! Vivyohivyo kwa mama lishe! Weka chakula cha buku hata kama ni kidogo asiposhiba ataongeza kwasababu lengo lako liwe kupata hiyo buku yake! Kalaghabao!
 
Biashara=Akili+Busara+Nguvu za kiroho

Mleta mada umeongelea upande wa nguvu za kiroho. Ni kweli bila nguvu za koroho hutoboi. Wewe unafungua biashara hiyo hiyo na wengine kibao wanaifanya katika eneo hilo hilo! Kwanini waje kununua kwako wasiende kwa mwingine! Kama nyote mnatumia Akili + Busara sawa za kufanya hiyo biashara, basi atakayeuza ni yule anayetumia nguvu za Mungu aliye hai au yule anayetumia nguvu za shetani.
Kuhusu Akili ebu niongelee jambo moja kuhusu wauza mafuta ya kula kwenye chupa za kupima nusu lita, lita, lita mbili na kuendelea. Ukiwa unafanya biashara hii wewe ni mjasiriamali tu mwenye mtaji chini ya laki moja (100,000). Ukumbuke wateja wako wengi kiasi cha hela walichonacho ni buku (1,000). Inakuwaje unajaza mchupa ya buku mbili (2,000) unaacha robo lita ya buku (1,000)???. Unataka utajiri wa haraka?? Wateja wako unaowaendea ni masikini kwahiyo weka kipimo wanachokimudu! Vivyohivyo kwa mama lishe! Weka chakula cha buku hata kama ni kidogo asiposhiba ataongeza kwasababu lengo lako liwe kupata hiyo buku yake! Kalaghabao!
Nguvu za kiroho, uko sahihi.
 
Ndio mana mi mwanzon nikipataga laki tano kushuka nakura yote mdogo mdogo mpaka fyaa hapo nahaso ilikuwa kupata nyngn mpaka mwaka uishe bas huku nikiamin nikipata milion mbili natoboa na kwel siku nilipata m2 ndio nikapanda kimafanikio so imani yako inakutuma wapi? Anzia hapo
 
Juhudi bila ya kufuata sheria na kanuni za juhudi hizo ni kujitesa tu.

Vijana wengi wanapambana sana usiku na mchana kufanya Biashara mbalimbali ili wajikwamue kiuchumi ila waliowengi wanatoka patupu. Zaidi wanaambulia madeni mazito sana na kufilisiwa.

Jamani ndugu zanguni jitahidini mtoke kwenye huo usingizi mzito mliolala wa kuamini utafanikiwa kibiashara kwa bahati na juhudi binafsi.

Jamani eee biashara ni zaidi ya mtaji ulionao,ubora wa bidhaa ulionao au eneo zuri ulilofungua biashara hiyo.

Biashara ni roho yenye uhai hivyo basi ili unfanikiwe inabidi ujue na uzingatie sheria na kanuni za roho hai ya biashara.

Kama unafanya Biashara bila ya kujua hili basi ndugu yangu hutoboi ng'oooooo hata ufanye nini. Yaani hata uwe na frem kariakoo bila ya kufuata sheria za roho hai ya biashara huchomoki dogo.

Aisee hivi unajua kama biashara nayo inapenda,inachukia,inafurahi,inaumwa,inaiba,inalala,inapumzika,inatamaa,inamawazo n.k. Yaani naomba nieleweke sizungumzii mfanyabiashara ninazungumzia Biashara yenyewe.

Sasa ngoja nikusanue kidogo ili akili ikukae sawa. Wengi mmefungua biashara zenye roho zifuatazo ndio maana hamtoboi

i/ Biashara yenye roho ya chuki. Sifa ya biashara hii inakuwa inakuchukua sana wewe uliyeifungua. Kila ukipambana kuiweka sawa inagoma. Biashara haikupendi inakuchukia kinoma ila wewe unakaza tu bila kujielewa. Sanuka dogo unapoteza muda bure.

ii/ Biashara yenye roho ya wizi. Watu wengi sana humu mmefungua biashara zenye roho ya wizi ndiyo maana mnaibiwa sana mitaji yenu na biashara hizi. Kila ukiwekeza mtaji wako kwenye biashara, biashara inakuibia mtaji wote. Kazi yako inakuwa kila mara ni kuongeza mtaji kila siku. Daaah huruma sana.

iii/ Biashara yenye roho ya utasa. Biashara ina miaka kibao haizai. Wengi mnabiashara zenye roho ya utasa. Yaani kila ukipambana biashara haizai kabisa. Unashindwa kuelewa kuwa biashara yako ni tasa unaendelea kukomaa kizembe tu. Duuuuuh poleni sana.
.
iv/ Biashara yenye roho ya tamaa. Kijana kama Biashara yako inaroho ya tamaa huchomoki mzee. Biashara zenye roho ya tamaa ni mbaya sana na zinawafirisi wengi sana hapa duniani. Ukiona biashara inakumalizia hela na sio kukuingizia hela hiyo biashara inatamaa achana nayo haraka sana

v/ biashara yenye roho ya ukorofi na utovu wa nidhamu. Ukifungua biashara hii kila siku utakuwa unashinda kwa mwenyekiti wa mtaa au polisi kutatua kesi zinazosababishwa na biashara yako uliyoifungua. Mara gari yako ya biashara imegonga mtu,Mara ukuta wa mgahawa wako umedondokea wateja na mengine mengi. Hahahahaa balaa sana

vi/ Na mengine mengi

Sasa kutatua yote haya ni kazima urudi kwenye sheria za roho hai za biashara ambazo kwa bahati mbaya wanazifahamu watu wachache sana na zinabaki kuwa siri kwa watu wachache sana.

Sanuka wewe ili utoboe acha ujuaji.
hivi kwa mfano biashara ya makampuni, public companies roho inakuwaje. mfano mabenki inakuwaje roho
 
sema nini. kuna wachawi sana kwenye mafanikio
Ukiwa unapambana katika hali ya ufahamu wa kibanadamu alafu ukashtuka kuwa kuna kitu hapa hakijakaa sawa! Basi hapo umekutana na mapambano ya kiroho! Mapambano ya kiroho kuyashinda unahitaji Mungu (tena Mungu wa walokole, sio mungu wa kwenye dini! mungu wa kwenye dini hana maajabu) au nenda kwa shetani. Hila nakuonya! Usicheze na shetani!
 
Ukiwa unapambana katika hali ya ufahamu wa kibanadamu alafu ukashtuka kuwa kuna kitu hapa hakijakaa sawa! Basi hapo umekutana na mapambano ya kiroho! Mapambano ya kiroho kuyashinda unahitaji Mungu (tena Mungu wa walokole, sio mungu wa kwenye dini! mungu wa kwenye dini hana maajabu) au nenda kwa shetani. Hila nakuonya! Usicheze na shetani!
Mungu wa walokole Ndio yupi huyo hebu muelezee sifa zake upate kueleweka kwa uwazi Bado umetumia fumbo.
 
Juhudi bila ya kufuata sheria na kanuni za juhudi hizo ni kujitesa tu.

Vijana wengi wanapambana sana usiku na mchana kufanya Biashara mbalimbali ili wajikwamue kiuchumi ila waliowengi wanatoka patupu. Zaidi wanaambulia madeni mazito sana na kufilisiwa.

Jamani ndugu zanguni jitahidini mtoke kwenye huo usingizi mzito mliolala wa kuamini utafanikiwa kibiashara kwa bahati na juhudi binafsi.

Jamani eee biashara ni zaidi ya mtaji ulionao,ubora wa bidhaa ulionao au eneo zuri ulilofungua biashara hiyo.

Biashara ni roho yenye uhai hivyo basi ili unfanikiwe inabidi ujue na uzingatie sheria na kanuni za roho hai ya biashara.

Kama unafanya Biashara bila ya kujua hili basi ndugu yangu hutoboi ng'oooooo hata ufanye nini. Yaani hata uwe na frem kariakoo bila ya kufuata sheria za roho hai ya biashara huchomoki dogo.

Aisee hivi unajua kama biashara nayo inapenda,inachukia,inafurahi,inaumwa,inaiba,inalala,inapumzika,inatamaa,inamawazo n.k. Yaani naomba nieleweke sizungumzii mfanyabiashara ninazungumzia Biashara yenyewe.

Sasa ngoja nikusanue kidogo ili akili ikukae sawa. Wengi mmefungua biashara zenye roho zifuatazo ndio maana hamtoboi

i/ Biashara yenye roho ya chuki. Sifa ya biashara hii inakuwa inakuchukua sana wewe uliyeifungua. Kila ukipambana kuiweka sawa inagoma. Biashara haikupendi inakuchukia kinoma ila wewe unakaza tu bila kujielewa. Sanuka dogo unapoteza muda bure.

ii/ Biashara yenye roho ya wizi. Watu wengi sana humu mmefungua biashara zenye roho ya wizi ndiyo maana mnaibiwa sana mitaji yenu na biashara hizi. Kila ukiwekeza mtaji wako kwenye biashara, biashara inakuibia mtaji wote. Kazi yako inakuwa kila mara ni kuongeza mtaji kila siku. Daaah huruma sana.

iii/ Biashara yenye roho ya utasa. Biashara ina miaka kibao haizai. Wengi mnabiashara zenye roho ya utasa. Yaani kila ukipambana biashara haizai kabisa. Unashindwa kuelewa kuwa biashara yako ni tasa unaendelea kukomaa kizembe tu. Duuuuuh poleni sana.
.
iv/ Biashara yenye roho ya tamaa. Kijana kama Biashara yako inaroho ya tamaa huchomoki mzee. Biashara zenye roho ya tamaa ni mbaya sana na zinawafirisi wengi sana hapa duniani. Ukiona biashara inakumalizia hela na sio kukuingizia hela hiyo biashara inatamaa achana nayo haraka sana

v/ biashara yenye roho ya ukorofi na utovu wa nidhamu. Ukifungua biashara hii kila siku utakuwa unashinda kwa mwenyekiti wa mtaa au polisi kutatua kesi zinazosababishwa na biashara yako uliyoifungua. Mara gari yako ya biashara imegonga mtu,Mara ukuta wa mgahawa wako umedondokea wateja na mengine mengi. Hahahahaa balaa sana

vi/ Na mengine mengi

Sasa kutatua yote haya ni kazima urudi kwenye sheria za roho hai za biashara ambazo kwa bahati mbaya wanazifahamu watu wachache sana na zinabaki kuwa siri kwa watu wachache sana.

Sanuka wewe ili utoboe acha ujuaji.
Juhudi bila ya kufuata sheria na kanuni za juhudi hizo ni kujitesa tu.

Vijana wengi wanapambana sana usiku na mchana kufanya Biashara mbalimbali ili wajikwamue kiuchumi ila waliowengi wanatoka patupu. Zaidi wanaambulia madeni mazito sana na kufilisiwa.

Jamani ndugu zanguni jitahidini mtoke kwenye huo usingizi mzito mliolala wa kuamini utafanikiwa kibiashara kwa bahati na juhudi binafsi.

Jamani eee biashara ni zaidi ya mtaji ulionao,ubora wa bidhaa ulionao au eneo zuri ulilofungua biashara hiyo.

Biashara ni roho yenye uhai hivyo basi ili unfanikiwe inabidi ujue na uzingatie sheria na kanuni za roho hai ya biashara.

Kama unafanya Biashara bila ya kujua hili basi ndugu yangu hutoboi ng'oooooo hata ufanye nini. Yaani hata uwe na frem kariakoo bila ya kufuata sheria za roho hai ya biashara huchomoki dogo.

Aisee hivi unajua kama biashara nayo inapenda,inachukia,inafurahi,inaumwa,inaiba,inalala,inapumzika,inatamaa,inamawazo n.k. Yaani naomba nieleweke sizungumzii mfanyabiashara ninazungumzia Biashara yenyewe.

Sasa ngoja nikusanue kidogo ili akili ikukae sawa. Wengi mmefungua biashara zenye roho zifuatazo ndio maana hamtoboi

i/ Biashara yenye roho ya chuki. Sifa ya biashara hii inakuwa inakuchukua sana wewe uliyeifungua. Kila ukipambana kuiweka sawa inagoma. Biashara haikupendi inakuchukia kinoma ila wewe unakaza tu bila kujielewa. Sanuka dogo unapoteza muda bure.

ii/ Biashara yenye roho ya wizi. Watu wengi sana humu mmefungua biashara zenye roho ya wizi ndiyo maana mnaibiwa sana mitaji yenu na biashara hizi. Kila ukiwekeza mtaji wako kwenye biashara, biashara inakuibia mtaji wote. Kazi yako inakuwa kila mara ni kuongeza mtaji kila siku. Daaah huruma sana.

iii/ Biashara yenye roho ya utasa. Biashara ina miaka kibao haizai. Wengi mnabiashara zenye roho ya utasa. Yaani kila ukipambana biashara haizai kabisa. Unashindwa kuelewa kuwa biashara yako ni tasa unaendelea kukomaa kizembe tu. Duuuuuh poleni sana.
.
iv/ Biashara yenye roho ya tamaa. Kijana kama Biashara yako inaroho ya tamaa huchomoki mzee. Biashara zenye roho ya tamaa ni mbaya sana na zinawafirisi wengi sana hapa duniani. Ukiona biashara inakumalizia hela na sio kukuingizia hela hiyo biashara inatamaa achana nayo haraka sana

v/ biashara yenye roho ya ukorofi na utovu wa nidhamu. Ukifungua biashara hii kila siku utakuwa unashinda kwa mwenyekiti wa mtaa au polisi kutatua kesi zinazosababishwa na biashara yako uliyoifungua. Mara gari yako ya biashara imegonga mtu,Mara ukuta wa mgahawa wako umedondokea wateja na mengine mengi. Hahahahaa balaa sana

vi/ Na mengine mengi

Sasa kutatua yote haya ni kazima urudi kwenye sheria za roho hai za biashara ambazo kwa bahati mbaya wanazifahamu watu wachache sana na zinabaki kuwa siri kwa watu wachache sana.

Sanuka wewe ili utoboe acha ujuaji.
🙄💭
 
Uko sahihi kwenye makampuni au mashirika mengi yanayo stawi ni yake yenye tamaduni/imani nzuri ( Good organisation culture).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom