Great Thinkers,
Ni mshangao ilioje kwa baadhi yetu kushindwa hapa kuona hoja ya msingi zaidi vile! Heshima ya Jaji Warioba wala haina maswali LAKINI ukweli wa mambo ni kwamba uteuzi wake ni wa kisheria na utendaji wake kazi vile vile utafuata mkondo huo huo.
La kujiuliza hapa ni kwamba NANI huyo anayempa mwongozo wa kazi katika tume ile? Naam, swala hapa si IMANI TU na mtu gani atakayekalia kiti hicho bali swala zima la kukodolea ma ni je HADIDU ZA REJEA atakazotumia kama mwongozo wake wa kazi zinapatikana kutoka kwa nani?
Ni kutoka kwa SISI WANANCHI au ni kutoka kwa SERIKALI kwa maana ya CCM?
Kwa upendeleo huu wa KIDINI JK atarajie upinzani kwa wakristo.
Kwa upendeleo huu wa KIDINI JK atarajie upinzani kwa wakristo.
Jmushi1,
Issa Shivji kwa weledi wake asingestahili kuachwa. Jenerali Ulimwengu, Kibamba kutoka asasi za kiraia na Prof. Abdala Safari wasingeachwa. Labda tuungane nao nje ya Tume ili tuunde parallel commission ya kuikosoa tume iliyoteuliwa
hapa waislamu wataingiza sana udini wao kwani ni wengi mno. sijapenda.
Wapi prof Safari, Shivji, Jenerali Ulimwengu, Ananilea Nkya kidogo hawa hawana nidhamu ya woga ila sio mbaya is a good begining... Na je waislamu tutapata haki yetu? Kwa tume sidhani! Ila sijui
Haki gani tena mnayotaka waislamu jamani? Hapa tunachotaka ni maslahi ya nchi kwa wananchi wote bila kujali dini ya mtu. Assumption ni kuwa nchi haina dini ila wananchi wake wana dini zao. Waachwe wapange mipango yako wenyewe, waabudu kwa uhuru bila kubughudhiwa ila wasivunje sheria, na dini za mashetani zenye kuhatarisha amani na usalama wa raia zisiruhusiwe.
Sasa mbona wazee tupu?
tena ndio wale wale waliotufikisha hapa tulipo..
Wapi prof Safari, Shivji, Jenerali Ulimwengu, Ananilea Nkya kidogo hawa hawana nidhamu ya woga ila sio mbaya is a good begining... Na je waislamu tutapata haki yetu? Kwa tume sidhani! Ila sijui
mbona ww umeanza huo udin hapa kabla yao?
Dada ya Asha Rose Migiro...M2wantum Malale ni Mkuu wa chuo cha Kislamu Morogoro na aliwahi kuwa katibu mkuu mara kadhaa. Ni swahiba mkubwa wa JK pamoja na mumewe Mzee malale ambaye pia aliwahi kuwa katibu mkuu wizara kadhaa
Yes, team ya juu ya kigoda cha mwl nyerere bado na heshima, hata jaji agustino naye jembe pia, hope they stay undefiled